< Job 34 >

1 ADEMÁS respondió Eliú, y dijo:
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 Oid, sabios, mis palabras; y vosotros, doctos, estadme atentos.
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 Porque el oído prueba las palabras, como el paladar gusta para comer.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 Escojamos para nosotros el juicio, conozcamos entre nosotros cuál [sea] lo bueno:
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 Porque Job ha dicho: Yo soy justo, y Dios me ha quitado mi derecho.
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 ¿He de mentir yo contra mi razón? Mi saeta es gravosa sin [haber yo] prevaricado.
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 ¿Qué hombre hay como Job, que bebe el escarnio como agua?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 Y va en compañía con los que obran iniquidad, y anda con los hombres maliciosos.
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 Porque ha dicho: De nada servirá al hombre el conformar su voluntad con Dios.
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 Por tanto, varones de seso, oidme: Lejos esté de Dios la impiedad, y del Omnipotente la iniquidad.
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 Porque él pagará al hombre según su obra, y él le hará hallar conforme á su camino.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 Sí, por cierto, Dios no hará injusticia, y el Omnipotente no pervertirá el derecho.
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 ¿Quién visitó por él la tierra? ¿y quién puso en orden todo el mundo?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 Si él pusiese sobre el [hombre] su corazón, y recogiese así su espíritu y su aliento,
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 Toda carne perecería juntamente, y el hombre se tornaría en polvo.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 Si pues [hay en ti] entendimiento, oye esto: escucha la voz de mis palabras.
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 ¿Enseñorearáse el que aborrece juicio? ¿y condenarás tú al que es tan justo?
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 ¿Hase de decir al rey: Perverso; y á los príncipes: Impíos?
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 ¿[Cuánto menos á] aquel que no hace acepción de personas de príncipes, ni el rico es de él más respetado que el pobre? porque todos son obras de sus manos.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 En un momento morirán, y á media noche se alborotarán los pueblos, y pasarán, y sin mano será quitado el poderoso.
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 Porque sus ojos están sobre los caminos del hombre, y ve todos sus pasos.
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 No hay tinieblas ni sombra de muerte donde se encubran los que obran maldad.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 No carga pues él al hombre más [de lo justo], para que vaya con Dios á juicio.
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 El quebrantará á los fuertes sin pesquisa, y hará estar otros en su lugar.
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Por tanto él hará notorias las obras de ellos, cuando los trastornará en la noche, y serán quebrantados.
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 Como á malos los herirá en lugar donde sean vistos:
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 Por cuanto así se apartaron de él, y no consideraron todos sus caminos;
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 Haciendo venir delante de él el clamor del pobre, y que oiga el clamor de los necesitados.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 Y si él diere reposo, ¿quién inquietará? si escondiere el rostro, ¿quién lo mirará? [Esto] sobre una nación, y lo mismo sobre un hombre;
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 Haciendo que no reine el hombre hipócrita para vejaciones del pueblo.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 De seguro conviene se diga á Dios: Llevado he ya [castigo], no [más] ofenderé:
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 Enséñame tú lo que yo no veo: que si hice mal, no lo haré más.
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 ¿[Ha de ser eso] según tu mente? El te retribuirá, ora rehuses, ora aceptes, y no yo: di si no, lo que tú sabes.
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Los hombres de seso dirán conmigo, y el hombre sabio me oirá:
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 Que Job no habla con sabiduría, y que sus palabras no son con entendimiento.
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 Deseo yo que Job sea probado ampliamente, á causa de sus respuestas por los hombres inicuos.
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 Porque á su pecado añadió impiedad: bate las manos entre nosotros, y contra Dios multiplica sus palabras.
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”

< Job 34 >