< Job 30 >

1 MAS ahora los más mozos de días que yo, se ríen de mí; cuyos padres yo desdeñara ponerlos con los perros de mi ganado.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Porque ¿para qué yo habría menester la fuerza de sus manos, en los cuales había perecido con el tiempo?
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Por causa de la pobreza y del hambre [andaban] solos; huían á la soledad, á lugar tenebroso, asolado y desierto.
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Que cogían malvas entre los arbustos, y raíces de enebro para calentarse.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Eran echados de entre [las gentes], y todos les daban grita como al ladrón.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 Habitaban en las barrancas de los arroyos, en las cavernas de la tierra, y en las rocas.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Bramaban entre las matas, y se reunían debajo de las espinas.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Hijos de viles, y hombres sin nombre, más bajos que la misma tierra.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Y ahora yo soy su canción, y he sido hecho su refrán.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Abomínanme, aléjanse de mí, y aun de mi rostro no detuvieron su saliva.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Porque [Dios] desató mi cuerda, y me afligió, por eso se desenfrenaron delante de mi rostro.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 A la mano derecha se levantaron los jóvenes; empujaron mis pies, y sentaron contra mí las vías de su ruina.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Mi senda desbarataron, aprovecháronse de mi quebrantamiento, contra los cuales no hubo ayudador.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Vinieron como por portillo ancho, revolviéronse á [mi] calamidad.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Hanse revuelto turbaciones sobre mí; combatieron como viento mi alma, y mi salud pasó como nube.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 Y ahora mi alma está derramada en mí; días de aflicción me han aprehendido.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 De noche taladra sobre mí mis huesos, y mis pulsos no reposan.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Con la grande copia [de materia] mi vestidura está demudada; cíñeme como el cuello de mi túnica.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Derribóme en el lodo, y soy semejante al polvo y á la ceniza.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Clamo á ti, y no me oyes; preséntome, y no me atiendes.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Haste tornado cruel para mí: con la fortaleza de tu mano me amenazas.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Levantásteme, é hicísteme cabalgar sobre el viento, y disolviste mi sustancia.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Porque yo conozco que me reduces á la muerte; y á la casa determinada á todo viviente.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Mas él no extenderá la mano contra el sepulcro; ¿clamarán [los sepultados] cuando él los quebrantare?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 ¿No lloré yo al afligido? Y mi alma ¿no se entristeció sobre el menesteroso?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Cuando esperaba yo el bien, entonces vino el mal; y cuando esperaba luz, la oscuridad vino.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Mis entrañas hierven, y no reposan; días de aflicción me han sobrecogido.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Denegrido ando, y no por el sol: levantádome he en la congregación, y clamado.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 He venido á ser hermano de los dragones, y compañero de los buhos.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Mi piel está denegrida sobre mí, y mis huesos se secaron con ardentía.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Y hase tornado mi arpa en luto, y mi órgano en voz de lamentadores.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< Job 30 >