< Job 29 >

1 Y VOLVIÓ Job á tomar su propósito, y dijo:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 ¡Quién me tornase como en los meses pasados, como en los días que Dios me guardaba,
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Cuando hacía resplandecer su candela sobre mi cabeza, á la luz de la cual yo caminaba en la oscuridad;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Como fué en los días de mi mocedad, cuando el secreto de Dios estaba en mi tienda;
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Cuando aun el Omnipotente estaba conmigo, y mis hijos alrededor de mí;
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Cuando lavaba yo mis caminos con manteca, y la piedra me derramaba ríos de aceite!
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Cuando salía á la puerta á juicio, y en la plaza hacía preparar mi asiento,
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Los mozos me veían, y se escondían; y los viejos se levantaban, y estaban en pie;
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Los príncipes detenían sus palabras, ponían la mano sobre su boca;
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 La voz de los principales se ocultaba, y su lengua se pegaba á su paladar:
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Cuando los oídos que me oían, me llamaban bienaventurado, y los ojos que me veían, me daban testimonio:
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Porque libraba al pobre que gritaba, y al huérfano que carecía de ayudador.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 La bendición del que se iba á perder venía sobre mí; y al corazón de la viuda daba alegría.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Vestíame de justicia, y ella me vestía como un manto; y mi toca era juicio.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Yo era ojos al ciego, y pies al cojo.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 A los menesterosos era padre; y de la causa que no entendía, me informaba con diligencia:
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Y quebraba los colmillos del inicuo, y de sus dientes hacía soltar la presa.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Y decía yo: En mi nido moriré, y como arena multiplicaré días.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Mi raíz estaba abierta junto á las aguas, y en mis ramas permanecía el rocío.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Mi honra se renovaba en mí, y mi arco se corroboraba en mi mano.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 Oíanme, y esperaban; y callaban á mi consejo.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Tras mi palabra no replicaban, y mi razón destilaba sobre ellos.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Y esperábanme como á la lluvia, y abrían su boca [como] á la lluvia tardía.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Si me reía con ellos, no lo creían: y no abatían la luz de mi rostro.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Calificaba yo el camino de ellos, y sentábame en cabecera; y moraba como rey en el ejército, como el que consuela llorosos.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Job 29 >