< Job 10 >

1 ESTÁ mi alma aburrida de mi vida: daré yo suelta á mi queja sobre mí, hablaré con amargura de mi alma.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 Diré á Dios: no me condenes; hazme entender por qué pleiteas conmigo.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 ¿Parécete bien que oprimas, que deseches la obra de tus manos, y que resplandezcas sobre el consejo de los impíos?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 ¿Tienes tú ojos de carne? ¿ves tú como ve el hombre?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 ¿Son tus días como los días del hombre, ó tus años como los tiempos humanos,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 Para que inquieras mi iniquidad, y busques mi pecado,
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 Sobre saber tú que no soy impío, y que no hay quien de tu mano libre?
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 Tus manos me formaron y me compusieron todo en contorno: ¿y así me deshaces?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Acuérdate ahora que como á lodo me diste forma: ¿y en polvo me has de tornar?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 ¿No me fundiste como leche, y como un queso me cuajaste?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 Vestísteme de piel y carne, y cubrísteme de huesos y nervios.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 Vida y misericordia me concediste, y tu visitación guardó mi espíritu.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Y estas cosas tienes guardadas en tu corazón; yo sé que esto está cerca de ti.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 Si pequé, tú me has observado, y no me limpias de mi iniquidad.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 Si fuere malo, ¡ay de mí! y si fuere justo, no levantaré mi cabeza, estando harto de deshonra, y de verme afligido.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 Y subirá de punto, [pues] me cazas como á león, y tornas á hacer en mí maravillas.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 Renuevas contra mí tus plagas, y aumentas conmigo tu furor, remudándose sobre mí ejércitos.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 ¿Por qué me sacaste de la matriz? Habría yo espirado, y no me vieran ojos.
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 Fuera, como si nunca hubiera sido, llevado desde el vientre á la sepultura.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 ¿No son mis días poca cosa? Cesa pues, y déjame, para que me conforte un poco.
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 Antes que vaya para no volver, á la tierra de tinieblas y de sombra de muerte;
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 Tierra de oscuridad, lóbrega como sombra de muerte, sin orden, y que aparece como [la] oscuridad [misma].
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >