< Proverbios 9 >

1 La sabiduría edificó su casa; labró sus siete columnas:
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 Mató a su víctima, templó su vino, y puso su mesa.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 Envió sus criadas, clamó sobre lo más alto de la ciudad:
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 Cualquiera simple, venga acá. A los faltos de entendimiento dijo:
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 Veníd, coméd mi pan; y bebéd del vino que yo he templado.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Dejád las simplezas, y vivíd; y andád por el camino de la inteligencia.
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 El que castiga al burlador, afrenta toma para sí; y el que reprende al impío, su mancha.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 No castigues al burlador, porque no te aborrezca: castiga al sabio, y amarte ha.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Da instrucción al sabio, y será más sabio: enseña al justo, y añadirá enseñamiento.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 El temor de Jehová es el principio de la sabiduría; y la ciencia de los santos es inteligencia.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 Porque por mí se aumentarán tus días; y años de vida se te añadirán.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 Si fueres sabio, para ti lo serás; mas si fueres burlador, tú solo pagarás.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 La mujer insensata es alborotadora, es simple, y no sabe nada:
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 Asiéntase sobre una silla a la puerta de su casa, en lo alto de la ciudad;
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 Para llamar a los que pasan por el camino: que van por sus caminos derechos:
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 Cualquiera simple, venga acá. A los faltos de entendimiento, dijo:
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 Las aguas hurtadas son dulces; y el pan encubierto es suave.
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 Y no saben, que allí están los muertos; y sus convidados están en los profundos de la sepultura. (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbios 9 >