< Proverbios 10 >

1 El hijo sabio alegra al padre; y el hijo insensato es tristeza de su madre.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Los tesoros de maldad no serán de provecho; mas la justicia libra de la muerte.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Jehová no dejará tener hambre al alma del justo: mas la iniquidad lanzará a los impíos.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 La mano negligente hace pobre: mas la mano de los diligentes enriquece.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 El que recoge en el verano, es hombre entendido; el que duerme en el tiempo de la segada, hombre confuso.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Bendita es la cabeza del justo: mas la boca de los impíos cubrirá iniquidad.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 La memoria del justo será bendita: mas el nombre de los impíos se pudrirá.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 El sabio de corazón recibirá los mandamientos: mas el insensato de labios caerá.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 El que camina en integridad, anda confiado: mas el que pervierte sus caminos, será quebrantado.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 El que guiña del ojo, dará tristeza; y el insensato de labios será castigado.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 Vena de vida es la boca del justo: mas la boca de los impíos cubrirá la iniquidad.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 El odio despierta las rencillas: mas la caridad cubrirá todas las maldades.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 En los labios del prudente se halla sabiduría, y es vara a las espaldas del falto de entendimiento.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Los sabios guardan la sabiduría: mas la boca del insensato es calamidad cercana.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 Las riquezas del rico son su ciudad fuerte; y el desmayo de los pobres es su pobreza.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 La obra del justo es para vida: mas el fruto del impío es para pecado.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Camino a la vida es guardar la corrección; y el que deja la reprensión yerra.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 El que encubre el odio tiene labios mentirosos; y el que echa mala fama es insensato.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 En las muchas palabras no falta rebelión: mas el que refrena sus labios es prudente.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 Plata escogida es la lengua del justo: mas el entendimiento de los impíos es como nada.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Los labios del justo apacientan a muchos: mas los insensatos con falta de entendimiento mueren.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 La bendición de Jehová es la que enriquece, y no añade tristeza con ella.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Es como risa al insensato hacer abominación: mas el hombre entendido sabe.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Lo que el impío teme, eso le vendrá: mas Dios da a los justos lo que desean.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Como pasa el torbellino, así el malo no es: mas el justo, fundado para siempre.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Como el vinagre a los dientes, y como el humo a los ojos, así es el perezoso a los que le envían.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 El temor de Jehová aumentará los días: mas los años de los impíos serán acortados.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 La esperanza de los justos es alegría; mas la esperanza de los impíos perecerá.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Fortaleza es al perfecto el camino de Jehová: mas espanto es a los que obran maldad.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 El justo eternalmente no será removido, mas los impíos no habitarán la tierra.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 La boca del justo producirá sabiduría: mas la lengua perversa será cortada.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Los labios del justo conocerán lo que agrada: mas la boca de los impíos perversidades.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< Proverbios 10 >