< Job 18 >

1 Y respondió Baldad Sujita, y dijo:
Bildadi Mshuhi akajibu:
2 ¿Cuándo pondréis fin a las palabras? Entendéd, y después hablemos.
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3 ¿Por qué somos tenidos por bestias? ¿en vuestros ojos, somos viles?
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4 Oh tú que despedazas tu alma con tu furor, ¿será dejada la tierra por tu causa, y serán traspasadas las peñas de su lugar?
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5 Ciertamente la luz de los impíos será apagada, y la centella de su fuego no resplandecerá.
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6 La luz se oscurecerá en su tienda, y su candil se apagará sobre él.
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7 Los pasos de su potencia serán acortados, y su mismo consejo le echará a perder.
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8 Porque red será echada en sus pies, y sobre red andará.
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 Lazo prenderá su calcañar: esforzará contra él a los sedientos.
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 Su cuerda está escondida en la tierra, y su orzuelo sobre la senda.
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11 De todas partes le asombrarán temores; y con sus mismos pies le ahuyentarán.
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12 Su fuerza será hambrienta, y a su costilla estará aparejado quebrantamiento.
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 Comerá los ramos de su cuero, y el primogénito de la muerte tragará sus miembros.
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 Su confianza será arrancada de su tienda, y le harán llevar al rey de los espantos.
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 En su misma tienda morará como si no fuese suya: piedrazufre será esparcida sobre su morada.
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16 Abajo se secarán sus raíces, y arriba serán cortados sus ramos.
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17 Su memoria perecerá de la tierra, y no tendrá nombre por las calles.
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18 De la luz será lanzado a las tinieblas, y será echado del mundo.
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19 No tendrá hijo ni nieto en su pueblo, ni sucesor en sus moradas.
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20 Sobre su día se espantarán los por venir, y a los antiguos tomarán pavor.
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21 Ciertamente tales son las moradas del impío, y este es el lugar del que no conoció a Dios.
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

< Job 18 >