< Job 10 >

1 Mi alma es cortada en mi vida: por tanto yo soltaré mi queja sobre mí, y hablaré con amargura de mi alma.
“Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
2 Diré a Dios: No me condenes: házme entender por qué pleitéas conmigo.
Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
3 ¿Parécete bien que oprimas, y que deseches la obra de tus manos, y que favorezcas el consejo de los impíos?
Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
4 ¿Tienes tú ojos de carne? ¿ves tú como el hombre?
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
5 ¿Tus días son como los días del hombre? ¿tus años son como los tiempos humanos,
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
6 Que inquieras mi iniquidad, y busques mi pecado?
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
7 Sobre saber tú que yo no soy impío: y que no hay quien de tu mano libre.
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
8 Tus manos me formaron, y me hicieron todo al derredor: ¿y hásme de deshacer?
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
9 Acuérdate ahora que como a lodo me hiciste: ¿y hásme de tornar en polvo?
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
10 ¿No me fundiste como leche, y como un queso me cuajaste?
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
11 Vestísteme de piel y carne, y cubrísteme de huesos y nervios.
ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
12 Vida y misericordia hiciste conmigo; y tu visitación guardó mi espíritu.
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
13 Y estas cosas tienes guardadas en tu corazón: yo sé que esto está cerca de ti.
“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
14 Si yo pequé acecharme has tú, y no me limpiarás de mi iniquidad.
Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
15 Si fuere malo; ¡ay de mí! y si fuere justo, no levantaré mi cabeza, harto de deshonra, y de verme afligido.
Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
16 Y vas creciendo, cazándome como león: tornando, y haciendo en mí maravillas:
Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
17 Renovando tus llagas contra mi, y aumentando conmigo tu furor, remudándose sobre mí ejércitos.
Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
18 ¿Por qué me sacaste del vientre? Muriera yo, y no me vieran ojos.
“Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
19 Fuera, como si nunca hubiera sido, llevado desde el vientre a la sepultura.
Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
20 ¿Mis días no son una poca cosa? cesa pues, y déjame, para que me esfuerce un poco,
Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
21 Antes que vaya, para no volver, a la tierra de tinieblas y de sombra de muerte:
kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
22 Tierra de oscuridad y tenebrosa sombra de muerte, donde no hay orden; y que resplandece como la misma oscuridad.
nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”

< Job 10 >