< Job 9 >

1 Y respondió Job, y dijo:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Ciertamente yo conozco que es así: ¿y como se justificará el hombre con Dios?
“Naam, najua hili ni kweli. Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
3 Si quisiere contender con él, no le podrá responder a una cosa de mil.
Ingawa mtu angetaka kushindana naye, asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.
4 El es sabio de corazón, y fuerte de fuerza: ¿quién fue duro contra él, y quedó en paz?
Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. Ni nani aliyempinga naye akawa salama?
5 Que arranca los montes con su furor, y no conocen quien los trastornó.
Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.
6 Que remueve la tierra de su lugar, y hace temblar sus columnas.
Aitikisa dunia kutoka mahali pake na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.
7 Que manda al sol, y no sale; y a las estrellas sella.
Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; naye huizima mianga ya nyota.
8 El que solo extiende los cielos, y anda sobre las alturas de la mar.
Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
9 El que hizo el Arcturo, y el Orión y las Pléyades, y los lugares secretos del mediodía.
Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, na Orioni, Kilimia, na makundi ya nyota za kusini.
10 El que hace grandes cosas, e incomprensibles, y maravillosas sin número.
Hutenda maajabu yasiyopimika, miujiza isiyoweza kuhesabiwa.
11 He aquí, que él pasará delante de mí, y yo no le veré; pasará, y no le entenderé.
Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; apitapo mbele yangu, simtambui.
12 He aquí, arrebatará: ¿quién le hará restituir? ¿Quién le dirá: Qué haces?
Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’
13 Dios no tornará atrás su ira, y debajo de él se encorvan los que ayudan a la soberbia.
Mungu hataizuia hasira yake; hata jeshi kubwa la Rahabu lenye nguvu linajikunyata miguuni pake.
14 ¿Cuánto menos le responderé yo, y hablaré con él palabras estudiadas?
“Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye?
15 Que aunque yo sea justo, no responderé: antes habré de rogar a mi juez.
Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie.
16 Que si yo le invocase, y él me respondiese, aun no creeré que haya escuchado mi voz.
Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.
17 Porque me ha quebrado con tempestad, y ha aumentado mis heridas sin causa.
Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.
18 Que aun no me ha concedido que tome mi aliento, mas háme hartado de amarguras.
Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.
19 Si habláremos de su poder, fuerte ciertamente es: si de su juicio, ¿quién me lo emplazará?
Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?
20 Si yo me justificare, mi boca me condenará: si me predicare perfecto, él me hará inicuo.
Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.
21 Si yo me predicare acabado, no conozco mi alma: condenaré mi vida.
“Ingawa mimi sina kosa, haileti tofauti katika nafsi yangu; nauchukia uhai wangu.
22 Una cosa resta, es a saber, que yo diga: Al perfecto y al impío, él los consume.
Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’
23 Si es azote, mate de presto, él se rie de la tentación de los inocentes.
Wakati pigo liletapo kifo cha ghafula, yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa.
24 La tierra es entregada en manos de los impíos, y él cubre el rostro de sus jueces. Sino es él que lo hace, ¿dónde está? ¿quién es?
Wakati nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, yeye huwafunga macho mahakimu wake. Kama si yeye, basi ni nani?
25 Mis días fueron más ligeros que un correo: huyeron, y nunca vieron bien.
“Siku zangu zapita mbio kuliko mkimbiaji; zinapita upesi bila kuona furaha hata kidogo.
26 Pasaron con los navíos de Ebeh: o como el águila que se abate a la comida.
Zinapita upesi kama mashua ya mafunjo, mfano wa tai ayashukiaye mawindo kwa ghafula.
27 Si digo: Olvidaré mi queja, dejaré mi saña, y esforzarme he:
Kama nikisema, ‘Nitayasahau malalamiko yangu, nitabadili sura ya uso wangu na kutabasamu,’
28 Temo todos mis trabajos: sé que no me perdonarás.
bado ninahofia mateso yangu yote, kwa kuwa ninajua hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Si yo soy impío, ¿para que trabajaré en vano?
Kwa kuwa nimeonekana mwenye hatia, kwa nini basi nitaabishwe bure?
30 Aunque me lave con aguas de nieve, y aunque limpie mis manos con la misma limpieza;
Hata kama ningejiosha kwa sabuni na kutakasa mikono yangu kwa magadi,
31 Aun me hundirás en la huesa: y mis propios vestidos me abominarán.
wewe ungenitupa kwenye shimo la utelezi kiasi kwamba hata nguo zangu zingenichukia sana.
32 Porque no es hombre como yo, para que yo le responda, y vengamos juntamente a juicio.
“Yeye si mwanadamu kama mimi ili niweze kumjibu, ili kwamba tuweze kushindana naye mahakamani.
33 No hay entre nosotros árbitro que ponga su mano sobre nosotros ambos.
Laiti angelikuwepo mtu wa kutupatanisha kati yetu, aweke mkono wake juu yetu sote wawili,
34 Quite de sobre mí su verdugo, y su terror no me perturbe;
mtu angeliiondoa fimbo ya Mungu juu yangu, ili utisho wake usiendelee kunitia hofu.
35 Y hablaré, y no le temeré: porque así no estoy conmigo.
Ndipo ningenena naye, bila kumwogopa, lakini kama ilivyo kwangu sasa, sitaweza.

< Job 9 >