< Књига пророка Данила 7 >

1 Прве године Валтасара, цара вавилонског, усни Данило сан и виде утвару главе своје на постељи; тада написа сан и приповеди укратко.
Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza mfalme wa Babelli, Danieli alikuwa na ndoto na maono katika akili zake wakati alipokuwa amelala kitandani kwake. Kisha akayaandika yale aliyoyaona katika ndoto. Aliandika matukio ya muhimu sana:
2 Данило проговори и рече: Видех у утвари својој ноћу, а то четири ветра небеска ударише се на великом мору.
Danieli alieleza, “Usiku katika ndoto zangu niliona pepo nne za mbinguni zilikuwa zinaitikisa bahari kuu.
3 И четири велике звери изиђоше из мора, свака другачија.
Wanyama wakubwa wanne, kila mmoja alikuwa tofauti na mwenzake, walitoka katika bahari.
4 Прва беше као лав, и имаше крила орлова; гледах докле јој се крила поскубоше и подиже се са земље и стаде на ноге као човек, и срце људско даде јој се.
Mnyama wa kwanza alikuwa kama simba, lakini alikuwa na mabawa ya tai. Nilipokuwa natazama, mabawa yake yalikuwa yamepasuka na alikuwa ameinuliwa katika ardhi na alikuwa amesimama kwa miguu miwili kama mtu. Na alipewa akili za kibinadamu.
5 Потом, гле, друга звер беше као медвед, и стаде с једне стране, и имаше три ребра у устима међу зубима својим, и говораше јој се: Устани, једи много меса.
Na kulikuwa na mnyama wa pili, alikuwa kama dubu, na alikuwa ameinama, alikuwa na mbavu tatu katikati ya meno yake katika mdomo wake. Aliambiwa, 'Inuka na umeze watu wangi.'
6 Потом видех, и гле, друга, као рис, имаше на леђима четири крила као птица, и четири главе имаше звер, и даде јој се власт.
Baada ya hili, niliangalia tena. Kulikuwa na mnyama mwingine ambaye alionekana kama chui. Mgongoni mwake alikuwa na mabawa manne kama mabawa ya ndege, na alikuwa na vichwa vinne. Alipewa mamlaka ya kutawala.
7 Потом видех у утварама ноћним, и гле, четврта звер, које се требаше бојати, страшна и врло јака, и имаше велике зубе гвоздене, јеђаше и сатираше, и гажаше ногама остатак, и разликоваше се од свих звери пређашњих, и имаше десет рогова.
Baada haya, niliona usiku katika ndoto yangu mnyama wa nne, mwenye kuogofya, na kutisha na mwenye nguvu. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; aliteketeza, na kuvunja vunja katika vipande, na kusaga saga katika miguuni pake kile kilichosalia. Alikuwa ni wa tofauti na wanyama wengine, na alikuwa na pembe kumi.
8 Гледах рогове, и гле, други мали рог израсте међу онима, а три прва рога ишчупаше се пред њим; и гле, очи као очи човечије беху на том рогу, и уста која говораху велике ствари.
Na wakati nilipokuwa natafakari juu ya pembe, nilitazama na niliona pembe nyingine ndogo ilichipuka katikati ya pembe zingine. Mizizi ya pembe tatu kati ya pembe za mwanzo iling'olewa. Niliona katika pembe hii macho kama macho ya mtu na mdomo ambao ulikuwa ukijivuna kwa mambo makubwa.
9 Гледах докле се поставише престоли, и старац седе, на коме беше одело бело као снег, и коса на глави као чиста вуна, престо Му беше као пламен огњени, точкови Му као огањ разгорео.
Na nilipotazama, viti vya enzi vilikuwa vimewekwa, na Mtu wa siku za kale alikaa sehemu yake. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theruji, na nywele zake katika kichwa chake zilikuwa safi kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa na miali ya moto, na magurudumu yake yalikuwa yanawaka moto.
10 Река огњена излажаше и течаше испред Њега, хиљада хиљада служаше Му, и десет хиљада по десет хиљада стајаху пред Њим; суд седе, и књиге се отворише.
Mto wa moto ulitiririka kutoka mbele yake, na mamilioni ya watu walimtumikia, na wengine mia moja milioni walikuwa wamesimama mbele yake. Na mahakama iliitishwa, na vitabu vilifunguliwa.
11 Тада гледах ради гласа великих речи које говораше онај рог; и гледах докле не би убијена звер и тело јој се рашчини и даде се да изгори огњем.
Niliendelea kuangalia kwasababu ya maneno ya kiburi yaliyosemwa na pembe. Nilitazama wakati mnyama anauliwa, na mwili wake uliharibiwa, na ulitolewa kwa ajili ya kuchomwa moto.
12 И осталим зверима узе се власт, јер дужина животу беше им одређена до времена и до рока.
Na kwa wale wanyama wanne waliosalia, mamlaka yao yalitwaliwa mbali, lakini maisha yao yaliendelezea kwa kipindi fulani cha muda.
13 Видех у утварама ноћним, и гле, као Син човечији иђаше са облацима небеским, и дође до старца и стаде пред Њим.
Katika maono yangu usiku ule, nilimwona mtu mmoja anakuja katika mawingu ya mbinguni alikuwa kama mwana wa mtu; alikuja kwa Mzee wa Siku na aliletwa mbele zake.
14 И даде Му се власт и слава и царство да Му служе сви народи и племена и језици; власт је Његова власт вечна, која неће проћи, и царство се Његово неће расути.
Naye alipewa mamlaka ya kiutawala na utukufu na mamlaka ya kifalme ili kwamba watu wote, na mataifa na lugha ziweze kumtumikia yeye. Mamlaka yake ya kutawala ni mamlaka ya milele ambayo hayatapita, na ufalme wake ni ule ambao hautaangamizwa.
15 Мени Данилу пренеможе дух мој у телу мом, и утваре главе моје узнемирише ме.
Na kwangu mimi, Danieli, roho yangu ilihuzunishwa ndani yangu, na maono niliyoyaona katika akili zangu yalinisumbua.
16 Приступих к једном од оних који стајаху онде, и замолих га за истину од свега тога. И проговори ми и каза ми шта то значи:
Nilimsogelea mmoja wa hawa walikuwa wamesimama hapo na nikamwomba anioneshe maana ya mambo haya.
17 Ове четири велике звери јесу четири цара, који ће настати на земљи.
Hawa wanyama nne wakubwa ni wafalme wanne ambao watatoa katika nchi.
18 Али ће свеци Вишњег преузети царство, и држаће царство на век и довека.
Lakini watu watakatifu wa Mungu aliyejuu wataupokea ufalme na wataumiliki milele na milele.'
19 Тада зажелех знати истину о четвртој звери, која се разликоваше од свих и беше врло страшна, и имаше зубе гвоздене и нокте бронзане, и јеђаше и сатираше, а остатак ногама гажаше,
Ndipo nilipotaka kujua zaidi juu ya mnyama wa nne, ambaye alikuwa tofauti sana na wengine na alikuwa wa kutisha pamoja na meno yake ya chuma na makucha ya shaba; alimeza, na alivunja vipande vipande, na alisaga saga kwa miguu yake kile kilichokuwa kimesalia.
20 И о десет рогова шта јој беху на глави, и о другом који израсте и три отпадоше пред њим, о рогу који имаше очи и уста која говораху велике ствари и беше по виђењу већи од других.
Nilitaka kujua juu ya pembe kumi katika kichwa chake, na kuhusu pembe nyingine iliyochomoza, na ambayo mbele yake pembe zingine tatu zilianguka chini. Nilitaka kujua kuhusu pembe yenye macho na kuhusu mdomo uliokuwa unajisifu kwa mambo makubwa na ambayo ilionekana kuwa ni kubwa kuliko zingine.
21 Гледах, и тај рог војеваше са свецима и надвлађиваше их,
Na nilipotazama, pembe hii iliinua vita dhidi ya watu watakatifu na ilikuwa inawawashinda mpaka pale
22 Докле дође старац, и даде се суд свецима Вишњег, и приспе време да свеци преузму царство.
Mzee wa Siku alipokuja, na watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu Sana. Ndipo wakati ulipowadia ambapo watu watakatifu waliupokea ufalme.
23 Овако рече: Четврта звер биће четврто царство на земљи, које ће се разликовати од свих царстава, и изјешће сву земљу и погазити и сатрти.
Hiki ndicho mtu yule alichokisema, 'Kwa habari ya mnyama wanne, utakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia ambao utakuwa tofauti na falme zingine zote. Utaimeza dunia yote, na utaikanyaga yote chini na kuivunja vunja vipande vipande.
24 И десет рогова јесу десет царева, који ће настати из тог царства, а после њих настаће други, и он ће се разликовати од пређашњих, и покориће три цара.
Na kuhusu pembe kumi, kutoka katika ufalme huu, wafalme kumi watainuka, na mwingine atainuka baada yao. Atakuwa wa tofauti na wale waliomtangulia, na atawashinda wale wafalme watatu.
25 И говориће речи на Вишњег, и потираће свеце Вишњег, и помишљаће да промени времена и законе; и даће му се у руке за време и за времена и за по времена.
Atazungumza maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu sana na atawatesa watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu. Atajaribu kuzibadili sikukuu na sheria. Mambo haya atapewa mikononi mwake kwa mwaka mmoja, miaka miwili na nusu mwaka.
26 Потом ће сести суд, и узеће му се власт, те ће се истребити и затрти сасвим.
Lakini kikao cha mahakama kitaitishwa, na watazichukua nguvu zake za kifalme ili mwisho aweza kuharibiwa na kuteketezwa.
27 А царство и власт и величанство царско под свим небом даће се народу светаца Вишњег; Његово ће царство бити вечно царство, и све ће власти Њему служити и слушати Га.
Ufalme na utawala, ukubwa wa falme chini ya mbingu yote, watapewa watu walio wa watu watakatifu wa Yeye Aliye juu Sana. Ufalme wake ni ufalme wa milele, na falme zingine zote zitamtumikia na kumtii yeye.'
28 Овде је крај овој речи. А мене, Данила врло узнемирише мисли моје, и лице ми се све промени; али реч сачувах у срцу свом.
Na huu ndio mwisho wa mambo. Na kuhusu mimi, Danieli, mawazo yangu yanihuzunisha sana mimi na mwonekano wa uso wangu ulibadilika. Lakini mambo haya niliyahifadhi mimi mwenyewe.”

< Књига пророка Данила 7 >