< Књига пророка Данила 6 >

1 Свиде се Дарију те постави над царством сто и педесет управитеља да буду над свим царством;
Ilimpendeza Dario kuchagua juu ya ufalme magavana wa majimbo 120 ambao wangetawala juu ya ufalme wote.
2 А над њима три старешине, од којих један беше Данило, којима ће управитељи давати рачуне да не би цару било штете.
Juu yao kulikuwa na watawala wakuu watatu, na Daniel alikuwa mmoja wao. Hawa watawala waliwekwa ili waweze kuwasimamia magavana wa majimbo, ili kwamba mfalme asipate hasara.
3 А тај Данило надвишиваше старешине и управитеље, јер у њему беше велик дух и цар мишљаше да га постави над свим царством својим.
Danieli alipambanuliwa juu ya watawala wakuu na juu ya magavana wa majimbo kwasababu alikuwa na roho isiyo ya kawaida. Mfalme alikuwa akipanga kumweka juu ya ufalme wote.
4 Тада старешине и управитељи гледаху како би нашли шта да замере Данилу ради царства; али не могаху наћи забаве ни погрешке, јер беше веран, и не налажаше се у њега погрешке ни мане.
Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo walitafuta makosa katika kazi ambazo Danieli alizifanya kwa ufalme, lakini hawakuweza kuona ufisadi au kushindwa katika majukumu yake kwasababu alikuwa mwaminifu. Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake.
5 Тада рекоше они људи: Нећемо наћи на тог Данила ништа, ако не нађемо шта на њ ради закона Бога његовог.
Kisha watu hawa wakasema, “Hatukuweza kupata sababu yoyote ya kumshitaki huyu Danieli isipokuwa tukitafuta kitu fulani dhidi yake kuhusiana na sheria za Mungu wake.'”
6 Тада дођоше старешине и управитељи к цару, и рекоше му овако: Дарије царе, да си жив довека!
Ndipo watawala hawa na magavana walileta mpango mbele ya mfalme. Walimwambia, “Mfalme Dario, uishi milele!
7 Све старешине у царству, поглавари и управитељи, већници и војводе договорише се да се постави царска наредба и оштра забрана да ко би се год замолио за шта коме год богу или човеку за тридесет дана осим теби, царе, да се баци у јаму лавовску.
Watawala wote wakuu wa ufalme, magavana wa mikoa, na magavana wa majimbo, washauri, na magavana wameshauriana kwa pamoja na kuamua kuwa wewe, mfalme, unapaswa kupitisha amri na kuitekeleza, ili kwamba mtu yeyote anayefanya dua kwa mungu yeyote au mtu kwa siku thelathini, isipokuwa wewe mfalme, mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba.
8 Зато, царе, постави ту забрану и напиши да се не може променити, по закону мидском и персијском, који је непроменљив.
Sasa mfalme, litoe agizo na utie saini nyaraka ili kwamba isije ikabadilika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi, hivyo haiweze ikabatilishwa.
9 И цар Дарије написа књигу и забрану.
Basi, mfalme Dario alitia saini nyaraka kwa kuifanya amri kuwa sheria.
10 А Данило кад дозна да је књига написана, отиде својој кући, где беху отворени прозори у његовој соби према Јерусалиму, и падаше на колена своја три пута на дан и мољаше се и хвалу даваше Богу свом као шта чињаше пре.
Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria, alienda ndani ya nyumba yake (madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu), na alipiga magoti yake, kama alivyokuwa akifanya mara tatu kwa siku, na aliomba na kushukuru mbele ya Mungu wake, kama alivyofanya hapo kabla.
11 Тада се сабраше они људи, и нађоше Данила где се моли и припада Богу свом.
Kisha watu hawa walikuwa wameunda hila kwa pamoja walimwona Danieli akiomba na kutafuta msaada kutoka kwa Mungu.
12 И отидоше те рекоше цару за царску забрану: Ниси ли написао заповест, да ко би се год замолио коме год богу или човеку за тридесет дана, осим теби, царе, да се баци у јаму лавовску? Цар одговори и рече: Тако је по закону мидском и персијском, који је непроменљив.
Ndipo walipomwendea mfalme na kuongea naye kuhusiana na amri yake: “Je haukuweka amri kwamba mtu yeyote akayefanya maombi kwa mungu mwingine au kwa binadamu ndani ya siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, mfalme, lazima mtu huyo atupwe katika tundu la simba? Mfalme akajibu, “Jambo hili ni la hakika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi; ambazo haziwezi zikabatilishwa.”
13 Тада одговорише и рекоше цару: Данило, који је између робља Јудина, не хаје за те, царе, ни за забрану коју си написао, него се моли три пута на дан својом молитвом.
Kisha wakamjibu mfalme, “Mtu yule Daniel, ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda, hakutii wewe, mfalme wala maagizo yako uliyoyasaini. Yeye humwomba Mungu wake mara tatu kwa siku.”
14 Тада цар чувши то ожалости се врло, и науми да избави Данила, и труђаше се до захода сунчаног да га избави.
Mfalme aliposikia haya, alisikitishwa sana, alitumia akili jinsi ya kumwokoa kutoka katika utawala huu. Alisumbuka sana mpaka wakati wa kuzama kwa jua akijaribu kumwokoa Danieli.
15 Тада они људи сабраше се код цара и рекоше цару: Знај, царе, да је закон у Мидијана и Персијана да се никаква забрана и наредба коју постави цар, не мења.
Kisha watu hawa waliokuwa wamepanga njama walikusanyika kwa pamoja na mfalme, na wakamwambia, “Ujue mfalme kwamba ni sheria ya Wamedi na Waajemi kwamba hakuna amri au sanamu ambayo mfalme anaipitisha yaweza kubadilishwa.”
16 Тада цар рече те доведоше Данила и бацише га у јаму лавовску; и цар проговори и рече Данилу: Бог твој, коме без престанка служиш, нека те избави.
Ndipo mfalme alitoa agizo, na walimleta ndani Danieli, na kisha wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.''
17 И донесоше камен и метнуше јами на врата, и цар га запечати својим прстеном и прстеном својих кнезова да се ништа не промени за Данила.
Jiwe lililetwa katika mlango wa tundu, na mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake ili kwamba chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli.
18 Тада отиде цар у свој двор, и преноћи не једавши нити допустивши да му се донесе шта чим би се развеселио, и не може заспати.
Basi mfalme alienda kwenye ikulu yake na usiku ule alikuwa na mfungo. Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake, nao usingizi ulimkimbia.
19 Потом цар уста ујутро рано и отиде брже к јами лавовској.
Kisha katika mapambazuko mfalme aliamka na kwa haraka alienda kwenye tundu la simba.
20 И кад дође к јами, викну Данила жалосним гласом; и проговори цар и рече Данилу: Данило, слуго Бога Живога, Бог твој, коме служиш без престанка, може ли те избавити од лавова?
Na alipokaribia kwenye tundu, alimwita Danieli kwa sauti ya huzuni, akimwambia Danieli, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je Mungu wako ambaye anamtumkia daima ameweza kukuokoa kutoka katika simba?
21 Тада Данило рече цару: Царе, да си жив довека!
Ndipo Danieli akamwambia mfalme, “Mfalme, uishi milele!
22 Бог мој посла анђела свог и затвори уста лавовима, те ми не наудише; јер се нађох чист пред Њим, а ни теби царе, не учиних зла.
Mungu wangu amemtuma mjumbe na amevifunga vinywa vya simba, na hazijaweza kunidhuru. Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote mbele yake na pia mbele yako, ewe mfalme, na sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru.”
23 Тада се цар веома обрадова том, и заповеди да изваде Данила из јаме. И извадише Данила из јаме, и не нађе се ране на њему, јер верова Богу свом.
Basi mfalme alikuwa na furaha sana. Alitoa agizo kwamba wanatakiwa wamtoe Danieli nje ya tundu. Hivyo Danieli aliondolewa kutoka katika tundu. Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake, kwa kuwa alikuwa amemtumainia Mungu wake.
24 Потом заповеди цар, те доведоше људе који беху оптужили Данила, и бацише у јаму лавовску њих, децу њихову и жене њихове; и још не дођоше на дно јами, а лавови их зграбише и све им кости потрше.
Mfalme alitoa agizo, waletwe wale watu waliomshitaki Danieli na kisha akawatupa wao katika tundu la simba - wao, na watoto wao, na wake zao. Kabla hawajafika sakafuni, simba waliwararua na kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande.
25 Тада цар Дарије писа свим народима и племенима и језицима што живљаху у свој земљи: Мир да вам се умножи.
Kisha mfalme Dario aliandika ujumbe kwa watu wote, mataifa na lugha ambazo ziliishi katika dunia yote: “Amani na iongezeke kwenu.
26 Од мене је заповест да се у свој држави царства мог свак боји и страши Бога Даниловог, јер је Он Бог живи, који остаје довека, и царство се Његово неће расути, и власт ће Његова бити до краја;
Ninaagiza kwamba katika utawala wote wa ufalme wangu watu watetemeka na kumcha mbele ya Mungu wa Danieli, kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele, na ufalme wake hauwezi kuharibiwa; utawala wake utakuwepo hadi mwisho.
27 Он избавља и спасава, и чини знаке и чудеса на небу и на земљи, Он је избавио Данила од силе лавовске.
Yeye anatuhifadhi salama na kutuokoa, na anafanya ishara na maajabu mbinguni na duniani; amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.”
28 И тај Данило беше срећан за царовања Даријевог и за царовања Кира Персијанца.
Na hivyo basi, Danieli alifanikiwa katika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi.

< Књига пророка Данила 6 >