< Marko 6 >

1 Na kaaboka palyo ni kuyenda ukaasabe, ni benefunzi bake kabankota.
Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
2 Sabato kuika, katumbwa kuyegana mmasinagogi. Bandu banyansima paban'yowa na kabakanganya. Kabakoya agapatike kwako gano mafundisho? “Hekima gani yeno bampayi? “Atenda buli miujiza kati gano mumaboko gake?”
Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
3 Yono si ywa fundi selemala mwana'ge Mariamu nlongo wabe Yakobo, Yose, Yuda ni Simoni? Alombo bake si batama papano ni twenga?” Na bapulaiswe kwaa ni Yesu.
“Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
4 Yesu abakokeya nabii akosa kwaa heshima, ispokuwa pansengo wake, ni baadhi ya alon go bake ni munyumba yake.”
Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
5 Awesike kwa kutenda miujiza hapo, ila kaabeka maboko kwa mminye asunu kubaponiya.
Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
6 Atekanganywa mwalwakele bakotoka kwamini kwabe. kaayenda misengo yapambwega nipalyo nikuyegana.
Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
7 Kaakema balyo benefunzi komi ni ibele katumbuwa kubatuma abele abele, kabapaya ngupu kunani ya nsela,
Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
8 Ni kuwakokeya kana bapotwe kilebe ila lukongoso bai. Kna batole nkate, nkwisi, wala pwela pakitondo;
na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
9 Lakini bawale ilatu, na sio nganzu ibele.
lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
10 Na kaakeya nnyumba eyo muilingiya kana mpite mpaka uboka.
Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
11 Nnema wowote mana bakani kubapokiya ni ku8bapekanya, muboke apo, ni mupate liu mumagolo ginu, ibe usaidi kwabe.”
Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
12 Ni bembe kabayenda ni kuwakoya bandu babuye kwa Nnongo ni bstubu masambi gabe.
Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
13 Baabengike nsela banyansima, kabapaka mauta abinye kabapona.
Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
14 Mpwalume Herode ayowine ago, kuba liina lya Yesu lyatanganike muno. Benge kabakoya “Yohana mbatizaji ayokike, mwalo ogo ngupu ya miujiza itenda kasi nkati yake”.
Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
15 Benge nkati yabe kabakoya “yono ni Eliya” Benge kabakoya, “yono nabii kati balyo manabii basamani.”
Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
16 Herode ayowine kakoya, “Yohana ywa ninkatike mutwe ayokike.”
Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
17 Mwene Herode atelagiya Yohyana aboyolwe nikutabwa gerezani mwalwa Herodia (nyumbo wa mwasage Philipo) mwalo ywembwe abi nnyumbowe(amtweti).
Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
18 Kwa maana Yohana atekunkokweya Herode, “si halali kuntola nnyumbo wa mwasago”.
Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
19 Herodia atumbwi kunchukia ni kupala kum'bualaga lakinin awesike kwaa.
Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
20 Maana Herode ate kunnyogopa Yohana; atangike kwamba ni mundu mwene abi ni haki ni ntakatifu, kanneka salama. Palyo ayendelile kumpekanya ahuzunike muno, lakini apulaike kumpekanya.
maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
21 Palyo iike wakati mwafaka wa kubelekwa Herode kabaandaliya maofisa bake kalamu ni makamanda ni viongozi wa Galilaya.
Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
22 Mwana nwawa wa Hrode kayingiya ni kuina kulonge yabe, kampulaisa Herode ni ageni batami kabalya kilalyo sa kitamunyo. Mpwealume kankokeya ywa mwenza, “niyope sosote sa upala nami nakupaya.”
Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
23 Kalapiya na kukoya, sosote sa waniyopa, na kupaya, hata mana nnusu ya upwalume wango.”
Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
24 Kapita panza kannokiya mao bake, “niyope kele?” Kaankokeya, “Mutwe wa Yohana m'batizaji.”
Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
25 Mara yimo kwa Mpwalume nikunkeya, “nipala mutwe wa Yohana m'batizaji musahani.”
Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
26 Mpwalume atesikitishwa muno, lakini mwalowa kilapo ni ugeni awesike kwaa kukana sa ayopike ywa mwanza.
Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
27 Mpwalume kabatuma asikali kati ya balyo alinzi bake ni kubalagiya bayende kunnetia mutwe wa Yohana. Mlinzi ayei kunkata mutwe aii kifungoni.
Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
28 Kaleta mutwe wabii musahani ni kumpeya ywa muenza ni muenza ni ywembe kumpeya mao bake.
Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
29 Anafunzi bake kabayowa, kabayenda kuntola mwili wake kabayenda kuusika mmakaburi.
Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
30 Mitume, bakusanyike kulonge ya Yesu, kabankokeya yote agabatei ni ago kabayegana.
Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
31 Naye kababakiya, “muise mwabenge pandu pa kiiyo, tupomoli kwa muda” bandu banyansima baisi ni kuboka, hata bapatike kwaa kulya.
Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
32 Kaba kwela ngalaba kabayenda pandu pafaragha yika yabe.
Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
33 Lakini bababweni kababoka ni benge baatangike kwa pamwepe babatwike ni magolo nnemausima, Ni bembe baike kabla yabe.
Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
34 Kuika pwani babweni kipenga sa bandu, kababonia kiya, mana babi kati ngondo bakosike nsuka. Ni katumbwa kubayegana mambo ganmyansima.
Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 Muda yaugendelile benepunzi baisi kabankokeya, “pano mahala pa faragha ni m uda uyendelil.
Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
36 Ubalage bayende ijiji ya jirani balkapemi kilalyo.”
Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
37 Kabayangwa kakoya.”mwapeyi mwenga kilalyo.”Kabankokeya “Tuwesa kuyenda kupema mikate yenyen thamani ya dinari mia ibele ni kuapayaa balye?
Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
38 Kabakokeya,'m'bi ni mikate ilenga? yendaye mkalole.” palyo bapatike kaba mwalya “Mikate mitano ni omba abele.”
Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
39 Kabaakokeya bandu batami ipungu ipungu kunani ya manyei mabee.
Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
40 Kabaataminya ipungu ipungu ya bandu mia kwa hamsini.
Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
41 Katola mikate mitano ni omba abele, ni kulola kunani, kaibariki kuapaya benepunzi babeke kulongeya ipungu ni kubagana omba kwa bandu bote.
Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
42 Kabalya bote ni kuyukuta.
Walikula wote hadi wakatosheka.
43 Kabakusanya ipande ya mikate ya iigile kuitwelya itondo komi ni ibele, ni ipande ya omba pia.
Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
44 Ni bai analome elfu tano balii mikate.
Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
45 Kabaakokeya bakwele mmashua bayende kundo kwenge, hadi Bethsaida, wakati ywembe kabalaga makutano.
Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
46 Palyo baboi ayei ukiogolo kuyopa.
Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
47 Kitamunyo, mashua yabe yaii katikati ya bahari, nin ywembe aiyika nchi kavu.
Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
48 Kabaabona kabakunda masaka kupiga kasia mwalo upepo wainkale. Karibu ya bwamba kabakata,
Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
49 Lakini kabatyanga kunani ya mmase, na apaikuwapeta. Palyo bamweni katyanga kunani ya mase kabayingiwa ni masaka balongwage misimu kabaguta.
Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
50 Kwasababu bamweni kabatwelya masaka, mara kabaakokeye 'mube majasiri.”nenga. kana m'be ni masaka”
kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
51 Kayingia mmashua, ni upepo kautolya, ni bembe kaba nkanganya muno.
Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
52 Eyo batangite kwa maana ya ile mikate, malango gabe gabii masunu.
Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
53 Balokike upande wanyaibele, baike nnema wa Genesareti mashua yayei nanga.
Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
54 Kupita kunza ya mashua, kabantanga.
Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
55 Kababutuka mkoa nsima kutangaza, kabatumbua kubaleta abinye mmasela palyo bayowine andoisa.
Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
56 Palyo ayingii ukijiji, mjin au nnema, abinye bababei pa'lisoko ni kaban'yopa bakamwe lipendo lya ngobo yake awatei, ni bate balyo bakamwile baponi.
Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.

< Marko 6 >