< Ézéchiel 14 >

1 Et quelques-uns des anciens du peuple d'Israël vinrent me trouver, et ils s'assirent devant moi.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 Fils de l'homme, ces hommes ont conçu leurs pensées en leurs cœurs, et ils ont mis devant leur visage la punition de leurs iniquités: que dois-je leur répondre?
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 Parle et dis-leur: Voici ce que dit le Seigneur: Tout homme, un homme d'Israël, qui aura conçu des pensées en son cœur et qui aura mis devant son visage la punition de son iniquité, et qui viendra devant le prophète, moi le Seigneur je lui répondrai selon les engagements de sa pensée.
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 Car il désire tromper la maison d'Israël, pour qu'elle se laisse entraîner par ses convoitises et qu'elle éloigne son cœur de moi.
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 À cause de cela, dis à la maison d'Israël: Ainsi parle le Seigneur: Convertissez-vous et détournez-vous de vos mauvaises œuvres et de toutes vos iniquités, et détournez-en vos visages.
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Car tout homme, un homme de la maison d'Israël, et tout étranger prosélyte en Israël, qui se sera éloigné de moi et aura conçu des pensées en son cœur et aura mis devant son visage la punition de son iniquité, et qui viendra ensuite au prophète pour le questionner sur moi, moi le Seigneur, je lui répondrai selon les engagements où il est lui-même.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 Et je tournerai mon visage contre cet homme, et je le livrerai à la solitude et à l'extermination, et je l'effacerai du milieu de mon peuple, et vous saurez que je suis le Seigneur.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Et si un prophète s'est égaré, et s'il a parlé, c'est moi le Seigneur qui ai égaré ce prophète; et j'étendrai la main sur lui, et je l'exterminerai du milieu de mon peuple d'Israël.
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 Et ils porteront la peine de leur iniquité, selon l'iniquité de celui qui aura interrogé, laquelle sera punie de la même manière que l'iniquité du prophète;
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 Afin que la maison d'Israël ne s'égare plus en s'éloignant de moi, qu'elle ne se souille plus par ses péchés; de sorte qu'elle soit mon peuple, et que je sois son Dieu, dit le Seigneur.
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 Fils de l'homme, la terre qui aura péché contre moi en ses transgressions, j'étendrai la main sur elle; je briserai la force du pain, je lui enverrai la famine, et je détruirai les hommes et son bétail.
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 Et si, au milieu d'elle, se trouvent trois hommes comme Noé, Daniel et Job, ils seront sauvés à cause de leur justice, dit le Seigneur.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 Et si j'amène les bêtes farouches sur cette terre, et si je la punis, et si elle est désolée, et que nul ne la traverse en face des bêtes farouches;
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 Si ces trois hommes s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ni leurs fils ni leurs filles ne seront sauvés; eux seuls seront sauvés, mais la terre sera détruite.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Ou bien encore, si je promène le glaive sur cette terre, et si je dis: Que le glaive sillonne toute cette terre, et j'en ôterai les hommes et le bétail;
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 Et si ces trois hommes s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ils ne sauveront ni leurs fils ni leurs filles; eux seuls seront sauvés.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Ou bien encore, si j'envoie la peste en cette terre, et si je verse sur elle ma colère, avec le sang, pour détruire ses hommes et son bétail,
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 Et si Noé, Daniel et Jacob s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ni leurs fils ni leurs filles n'échapperont; eux seuls, à cause de leur justice, auront sauvé leurs âmes.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Voici ce que dit le Seigneur: Si j'envoie contre Jérusalem les quatre fléaux: le glaive, la famine, les bêtes farouches et la peste, pour y détruire les hommes et le bétail;
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 Voilà qu'il restera quelques hommes; et ceux-là seront sauvés; et ils emmèneront de la ville leurs fils et leurs filles; puis voilà qu'ils viendront à vous, et vous verrez leurs voies et leurs pensées; et le repentir vous pénètrera, à cause des maux que j'aurai fait tomber sur Jérusalem, à cause de toutes les afflictions que je lui aurai envoyées.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 Et ils vous consoleront, parce que vous verrez leurs voies et leurs pensées; et vous reconnaîtrez que ce n'est point à tort que j'ai fait tout ce que j'ai fait contre elle, dit le Seigneur.
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 14 >