< Ézéchiel 13 >

1 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils de l'homme, prophétise contre les prophètes d'Israël, prophétise et dis-leur: Écoutez la parole du Seigneur.
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
3 Voici ce que dit le Seigneur: Malheur à ceux qui prophétisent d'après leur cœur, et ne considèrent aucune chose!
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
4 Israël, tes prophètes sont comme des renards dans le désert,
Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
5 Ils ne s'appuient sur rien, et ils ont rassemblé de menus troupeaux contre la maison d'Israël. Ils ne se sont pas levés, le jour du Seigneur, ceux qui parlent,
Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
6 Ayant des visions fausses, prédisant des choses vaines, disant: Le Seigneur dit; mais le Seigneur ne les a pas envoyés, et ils ont pris sur eux de confirmer leur propre parole.
Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
7 N'avez-vous pas eu de fausses visions? n'avez-vous point prédit des choses vaines?
Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
8 À cause de cela, dis-leur: Ainsi parle le Seigneur: En punition de ce que vos paroles sont fausses, et vos prédictions vaines, voilà que je suis contre vous, dit le Seigneur.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
9 Et j'étendrai la main sur les prophètes qui ont des visions fausses, et qui disent des choses vaines; ils ne seront pas pour l'instruction de mon peuple; ils ne seront pas inscrits parmi la maison d'Israël; ils n'entreront pas dans l'héritage d'Israël, et ils sauront que je suis le Seigneur,
Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
10 En punition de ce qu'ils ont égaré mon peuple, disant: La paix, quand il n'y a point de paix: mon peuple bâtit un mur, ils le crépissent, et le mur tombera.
“‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
11 Dis à ceux qui le crépissent: Le mur tombera; aura de la pluie pour le faire crouler. Je lancerai des pierres sur ses jointures, et elles tomberont; et sur lui, un grand vent, et il se fendra.
kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
12 Et voilà que le mur est tombé, et ils ne diront pas: Où est le plâtre avec lequel nous l'avons crépi?
Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
13 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Je ferai éclater un souffle qui détruira avec fureur, et il y aura en ma colère une pluie qui débordera; et je lancerai en mon courroux des pierres qui détruiront jusqu'à l'anéantissement;
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
14 Et j'abattrai le mur que vous avez crépi, et il tombera; et je le coucherai sur la terre, et ses fondations seront à découvert, et il tombera; et vous périrez au milieu d'outrages, et vous saurez que je suis le Seigneur.
Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
15 Et j'assouvirai ma colère sur le mur, et sur ceux qui l'ont crépi; il tombera. Et comme je vous l'ai dit: Le mur n'est plus, ni ceux qui l'ont crépi.
Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
16 C'étaient les prophètes d'Israël qui prophétisaient pour Jérusalem, et qui en leurs. visions voyaient pour elle la paix, quand il n'y a point de paix, dit le Seigneur.
wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
17 Et toi, fils de l'homme, tourne la face contre les filles de ton peuple, contre celles qui prophétisent d'après leur cœur, et qui prophétisent contre elles-mêmes.
“Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
18 Et dis-leur: Ainsi parle le Seigneur: Malheur à celles qui cousent des coussins pour les mettre sous les deux coudes, et qui en font des oreillers pour toute tête de tout âge, afin de pervertir les âmes. Les âmes de mon peuple ont été perverties, et ces femmes conservaient ces âmes;
na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
19 Et elles m'ont profané devant mon peuple pour une poignée d'orge et pour un morceau de pain, afin de tuer des âmes qui ne devaient point mourir, et conserver la vie à des âmes qui ne devaient point vivre; c'est pour cela, ô filles, que vous avez prononcé devant mon peuple qui vous écoutait des prédictions vaines.
Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
20 À cause de cela, ainsi dit le Seigneur maître: Voilà que je suis contre ces coussins sur lesquels vous ramassez les âmes; je les mettrai en pièces sous vos bras, et je disperserai les âmes que vous avez perverties.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
21 Et je déchirerai vos oreillers, et je délivrerai mon peuple de vos mains, et ils ne seront plus ramassés par vous; et vous saurez que je suis le Seigneur.
Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
22 En punition de ce que vous pervertissez le cœur du juste que je n'avais point perverti, de ce que vous avez fortifié les mains du méchant pour qu'il fût entièrement incapable de revenir de sa voie mauvaise et de vivre;
Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
23 À cause de cela vous n'aurez plus vos visions fausses; vous ne prophétiserez plus vos mensonges, et je délivrerai mon peuple de vos mains; et vous saurez que je suis le Seigneur.
kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”

< Ézéchiel 13 >