< Ézéchiel 15 >

1 Et la parole du Seigneur me vint, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Dis, fils de l'homme, qu'est-ce que le bois de la vigne, en comparaison des arbres qui se trouvent dans les forêts?
“Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
3 Prendra-t-on le bois pour le rendre propre à être mis en œuvre? En fera- t-on des chevilles pour y suspendre quelque objet?
Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
4 Il n'est bon qu'à être jeté au feu et consumé; le feu chaque année consume le sarment qu'on ôte à la vigne en la taillant, et finalement il n'en reste rien; est-ce qu'il est propre à être mis en œuvre?
Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
5 Et même lorsqu'il est encore entier, il ne peut servir à aucune œuvre: si donc le feu l'a entièrement consumé, sera-t-il propre à être mis en œuvre?
Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
6 À cause de cela, dis-leur: Ainsi parle le Seigneur: De même que j'ai abandonné au feu, pour être consumé, le bois de la vigne parmi les arbres de la forêt; ainsi j'ai abandonné les habitants de Jérusalem.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
7 Et je tournerai contre eux mon visage; ils sortiront du feu, et cependant le feu les dévorera, et ils sauront que je suis le Seigneur, lorsque j'aurai tourné mon visage contre eux.
Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
8 Et je livrerai leur terre à la désolation pour les punir de leurs transgressions, dit le Seigneur.
Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 15 >