< Galatians 3 >

1 O foolish Galatians, who hath bewitched you, that ye should not obey the truth, before whose eyes Jesus Christ hath been evidently set forth, crucified among you?
Wagalatia wajinga, ni jicho gani ovu lililowaharibu? Je Yesu Kristo hakuoneshwa kama msulubiwa mbele ya macho yenu?
2 This only would I learn from you, Received ye the Spirit by the works of the law, or by the hearing of faith?
Mimi nataka tu kufahamu hili kutoka kwenu. Je mlimpokea Roho kwa matendo ya sheria au kwa kuamini kile mlichosikia?
3 Are ye so foolish? having begun in the Spirit, are ye now made perfect by the flesh?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hiki? Je mlianza katika Roho ili mmalize katika mwili?
4 Have ye suffered so many things in vain? if [it is] yet in vain.
Je mliteseka kwa mambo mengi bure, kama kweli yalikuwa ya bure?
5 He therefore that ministereth to you the Spirit, and worketh miracles among you, [doeth he this] by the works of the law, or by the hearing of faith?
Je yeye atoaye Roho kwenu na kutenda matendo ya nguvu kati yenu hufanya kwa matendo ya sheria au kwa kusikia pamoja na imani?
6 Even as Abraham believed God, and it was accounted to him for righteousness.
Abraham “Alimwamini Mungu akahesabiwa kuwa mwenye haki”.
7 Know ye therefore, that they who are of faith, the same are the children of Abraham.
Kwa namna ile ile eleweni kwamba, wale ambao wanaamini ni watoto wa Abrahamu.
8 And the scripture foreseeing that God would justify the heathen through faith, preached before the gospel to Abraham, [saying], In thee shall all nations be blessed.
Andiko lilitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa mataifa kwa njia ya imani. Injili ilihubiriwa kwanza kwa Abrahamu: “katika wewe mataifa yote yatabarikiwa”.
9 So then they who are of faith are blessed with faithful Abraham.
Ili baadaye wale ambao wana imani wabarikiwe pamoja na Abrahamu, ambaye alikuwa na imani.
10 For as many as are of the works of the law, are under the curse: for it is written, Accursed [is] every one that continueth not in all things which are written in the book of the law to do them.
Wale ambao wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu ambaye hashikamani na mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria, kuyatenda yote.”
11 But that no man is justified by the law in the sight of God, [is] evident: for, The just shall live by faith.
Sasa ni wazi kwamba Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria, kwa kuwa “Mwenye haki ataishi kwa imani”.
12 And the law is not of faith: but, The man that doeth them shall live by them.
Sheria haitokani na imani, lakini badala yake “Ambaye hufanya mambo haya katika sheria, ataishi kwa sheria.”
13 Christ hath redeemed us from the curse of the law, being made a curse for us: for it is written, Accursed [is] every one that hangeth on a tree:
Kristo alitukomboa sisi kutoka katika laana ya sheria wakati alipofanyika laana kwa ajili yetu. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti.”
14 That the blessing of Abraham might come on the Gentiles through Jesus Christ; that we might receive the promise of the Spirit through faith.
Lengo lilikuwa kwamba, baraka ambazo zilikuwa kwa Ibrahimu zingekuja kwa watu wa mataifa katika Kristo Yesu, ili kwamba tuweze kupokea ahadi ya Roho kupitia imani.
15 Brethren, I speak after the manner of men; Though it is but a man's covenant, yet [if it is] confirmed, no man disannulleth or addeth to it.
Ndugu, ninazungumza kwa namna ya kibinadamu. Hata wakati ambapo agano la kibinadamu limekwisha kuwekwa imara, hakuna awezaye kupuuza au kuongezea.
16 Now to Abraham and his seed were the promises made. He saith not, And to seeds, as of many; but as of one, And to thy seed, which is Christ.
Sasa ahadi zilisemwa kwa Ibrahim na kwa kizazi chake. Haisemi, “kwa vizazi,” kumaanisha wengi, bali badala yake kwa mmoja pekee, “kwa kizazi chako,” ambaye ni Kristo.
17 And this I say, [that] the covenant that was confirmed before by God in Christ, the law, which was four hundred and thirty years after, cannot disannul, that it should make the promise of no effect.
Sasa nasema hivi, sheria ambayo ilikuja miaka 430 baadaye, haiondoi agano la nyuma lililowekwa na Mungu.
18 For if the inheritance [is] by the law, [it is] no more by promise: but God gave [it] to Abraham by promise.
Kwa kuwa kama urithi ungelikuja kwa njia ya sheria, usingekuwa tena umekuja kwa njia ya ahadi. Lakini Mungu aliutoa bure kwa Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
19 What purpose then [serveth] the law? It was added because of transgressions, till the seed should come to whom the promise was made; [and it was] ordained by angels in the hand of a mediator.
Kwa nini sasa sheria ilitolewa? Iliongezwa kwa sababu ya makosa, mpaka mzao wa Ibrahimu aje kwa wale ambao kwao alikuwa ameahidiwa. Sheria iliwekwa katika shinikizo kupitia malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Now a mediator is not a [mediator] of one; but God is one.
Sasa mpatanishi humaanisha zaidi ya mtu mmoja, bali Mungu ni mmoja peke yake.
21 [Is] the law then against the promises of God? By no means: for if there had been a law given which could give life, verily righteousness would have been by the law.
Kwa hiyo je sheria iko kinyume na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa kama sheria iliyokuwa imetolewa ilikuwa na uwezo wa kuleta uzima, haki ingepatikana kwa sheria.
22 But the scripture hath concluded all under sin, that the promise by faith of Jesus Christ might be given to them that believe.
Lakini badala yake, andiko limefunga mambo yote chini ya dhambi. Mungu alifanya hivi ili kwamba ahadi yake ya kutuokoa sisi kwa imani katika Yesu Kristo iweze kupatikana kwa wale wanao amini.
23 But before faith came, we were kept under the law, shut up to the faith which should afterwards be revealed.
Lakini kabla ya imani katika Kristo haijaja, tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria hadi uje ufunuo wa imani.
24 Wherefore the law was our school-master [to bring us] to Christ, that we might be justified by faith.
Kwa hiyo sheria ilifanyika kiongozi wetu hadi Kristo alipokuja, ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
25 But after faith is come, we are no longer under a school-master.
Sasa kwa kuwa imani imekuja, hatuko tena chini ya mwangalizi.
26 For ye are all children of God by faith in Christ Jesus.
Kwa kuwa ninyi nyote ni watoto wa Mungu kupitia imani katika Kristo Yesu.
27 For as many of you as have been baptized into Christ, have put on Christ.
Wote ambao mlibatizwa katika Kristo mmejivika Kristo.
28 There is neither Jew nor Greek, there is neither bond nor free, there is neither male nor female: for ye are all one in Christ Jesus.
Hakuna Myahudi wala Myunani, mtumwa wala huru, mwanaume wala mwanamke, kwa kuwa ninyi nyote ni mmoja katika Kristo Yesu.
29 And if ye [are] Christ's, then are ye Abraham's seed, and heirs according to the promise.
Kama ninyi ni wa Kristo, basi ni uzao wa Ibrahimu, warithi kwa mujibu wa ahadi.

< Galatians 3 >