< Galatians 6 >

1 Brethren, if a man be overtaken in a fault, ye who are spiritual, restore such one in the spirit of meekness; considering thyself, lest thou also be tempted.
Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
2 Bear ye one another's burdens, and so fulfill the law of Christ.
Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
3 For if a man thinketh himself to be something, when he is nothing, he deceiveth himself.
Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
4 But let every man prove his own work, and then shall he have rejoicing in himself alone, and not in another.
Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
5 For every man shall bear his own burden.
Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
6 Let him that is taught in the word communicate to him that teacheth in all good things.
Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
7 Be not deceived; God is not mocked: for whatever a man soweth, that shall he also reap.
Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
8 For he that soweth to his flesh shall from the flesh reap corruption: but he that soweth to the Spirit, shall from the Spirit reap life everlasting. (aiōnios g166)
Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios g166)
9 And let us not be weary in well-doing: for in due season we shall reap, if we faint not.
Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
10 As we have therefore opportunity, let us do good to all [men], especially to them who are of the household of faith.
Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
11 Ye see how large a letter I have written to you with my own hand.
Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
12 As many as desire to make a fair show in the flesh, they constrain you to be circumcised; only lest they should suffer persecution for the cross of Christ.
Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
13 For neither they themselves who are circumcised keep the law; but desire to have you circumcised, that they may glory in your flesh.
Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
14 But may it never be that I should glory, save in the cross of our Lord Jesus Christ, by whom the world is crucified to me, and I to the world.
Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
15 For in Christ Jesus neither circumcision availeth any thing, nor uncircumcision, but a new creature.
Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
16 And as many as walk according to this rule, peace [be] on them, and mercy, and upon the Israel of God.
Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
17 From henceforth let no man trouble me: for I bear in my body the marks of the Lord Jesus.
Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
18 Brethren, the grace of our Lord Jesus Christ [be] with your spirit. Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.

< Galatians 6 >