< Revelation 5 >

1 And I sawe in the right honde of him that sat in ye trone a boke written with in and on the backside sealyd with vii. seales.
Kisha nikaona katika mkono wa kulia wa yule aliyekuwa amekaa katika kiti cha enzi, gombo lililoandikwa mbele na nyuma, na lilikuwa limetiwa mihuri saba.
2 And I sawe a stronge angell which cryed with a loude voyce: Who is worthy to open the boke and to loose the seales therof.
Nilimwona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kubwa, “Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?”
3 And no man in heven ner in erth nether vnder the erth was able to open the boke nether to loke thereon.
Hakuna mtu mbinguni au duniani au chini ya dunia aliyeweza kulifungua gombo au kulisoma.
4 And I wepte moche because no man was founde worthy to open and to rede the boke nether to loke thereon.
Nililia kwa uchungu kwa kuwa hakupatikana yeyote aliyestahili kulifungua gombo au kulisoma.
5 And one of the elders sayde unto me: wepe not: Beholde a lion beinge of the tribe of Iuda the rote of Dauid hath obtayned to open the boke and to lose the vii. seales therof.
Lakini mmoja wa wazee akaniambia, “Usilie. Tazama! Simba wa kabila ya Yuda, shina la Daudi, ameshinda, na anaweza kulifungua gombo na mihuri yake saba.”
6 And I behelde and loo in the myddes of the seate and of the. iiii. bestes and in the myddes of the elders stode a lambe as though he had bene kylled which had vii. hornes and vii. eyes which are the spretes of God sent into all the worlde.
Kati ya kiti cha enzi na wenye uhai wanne na miongoni mwa wazee, niliona mwanakondoo amesimama, akionekana kama aliye uawa. Alikuwa na pembe saba na macho saba - hizi ni roho saba za Mungu zilizotumwa duniani kote.
7 And he cam and toke the boke oute of the right honde of him that sate apon the seate.
Akaenda akalichukua gombo kutoka katika mkono wa kuume wa yule aliye kaa katika kiti cha enzi.
8 And when he had take the boke the. iiii. bestes and xxiiii. elders fell doune before the labe havynge harpes and golden vialles full of odoures which are the prayers of saynctes
Alipolichukua gombo, wenye uhai wanne na wazee ishirini na wanne wakainama hadi nchi mbele ya mwanakondoo. Kila mmoja alikuwa na kinubi na bakuli ya dhahabu iliyojaa uvumba ambayo ni maombi ya waamini.
9 and they songe a newe songe saynge: thou art worthy to take ye boke and to ope ye seales therof: for thou waste kylled and haste redemed vs by thy bloud out of all kynreddes and tonges and people and nacions
Waliimba wimbo mpya: “Unastahili kulitwaa gombo na kuzifungua muhuri zake. Kwa kuwa ulichinjwa, na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu wa kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
10 and haste made vs vnto oure god kynges and prestes and we shall raygne on the erth.
Ukawafanya ufalme na makuhani kwa ajili ya kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala juu ya nchi.”
11 And I behelde and I herd the voyce of many angylles aboute the trone and about the bestes and the elders and I herde thousand thousandes
Kisha nilitazama na nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kiti cha enzi - idadi yao ilikuwa 200, 000, 000 na wenye uhai na wazee.
12 saynge wt a lowde voyce: Worthy is the lambe that was killed to receave power and riches and wisdom and strenghte and honoure and glory and blyssynge.
Wakasema kwa sauti kuu, “Astahili mwanakondoo ambaye amechinjwa kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, heshima, utukufu, na sifa.”
13 And all creatures which are in heven and on the erth and vnder the erth and in the see and all that are in them herd I sayinge: blyssinge honour glory and power be vnto hym that sytteth apon the seate and vnto the lambe for ever more. (aiōn g165)
Nikasikia kila kilichoumbwa kilichokuwa mbinguni na duniani na chini ya nchi na juu ya bahari, kila kitu ndani yake kikisema, “Kwake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi na kwa mwanakondoo, kuwe sifa, heshima, utukufu na nguvu ya kutawala milele na milele.” (aiōn g165)
14 And the. iiii. bestes sayd: Ame. And the. xxiiii. elders fell apon their faces and worshypped him that lyveth for ever more.
Wenye uhai wanne wakasema, “Amina!” na wazee wakainama chini na kuabudu.

< Revelation 5 >