< Revelation 7 >

1 And after that I sawe. iiii. angels stonde on the iiii. corners of ye erth holdynge ye iiii. wyndes of the erth that ye wyndes shulde not blowe on the erthe nether on the see nether on eny tree.
Baada ya haya niliona malaika wanne wamesimama kwenye kona nne za dunia, wamezuia pepo nne za nchi kwa nguvu ili kwamba pasiwe na upepo unaovuma katika nchi, juu ya bahari au dhidi ya mti wowote.
2 And I sawe another angell ascende from the rysynge of the sunne: which had the seale of the lyvynge god and he cryed with a loude voyce to the iiii angelles (to whom power was geven to hurt the erth and the see)
Nikaona malaika mwingine akija kutoka mashariki, aliyekuwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akalia kwa sauti kuu kwa malaika wanne ambao walipewa ruhusa ya kudhuru nchi na bahari:
3 saying: Hurt not the erth nether the see nether the trees tyll we have sealed ye servauntes of oure god in their forheddes.
“Msiidhuru nchi, bahari, au miti mpaka tutakapokuwa tumekwishaweka muhuri katika paji za vichwa vya watumishi wa Mungu wetu.”
4 And I herde the nombre of them which were sealed and there were sealed an C. and xliiii. M. of all the trybes of the chyldren of Israhell.
Nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: 144, 000, ambao walitiwa muhuri kutoka kila kabila ya watu wa Israel:
5 Of the trybe of Iuda were sealed xii. M Of the trybe of Ruben were sealed xii. M. of the trybe of Gad were sealed xii. M.
12, 000 kutoka katika kabila ya Yuda walitiwa muhuri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Rubeni, 12, 000 kutoka katika kabila ya Gadi.
6 Of the trybe of Asser were sealed xii. M. Of the trybe of Neptalym were sealed xii. M. Of the trybe of Manasses were sealed xii. M.
12, 000 kutoka katika kabila ya Asheri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Naftali, 12, 000 kutoka katika kabila ya Manase.
7 Of ye trybe of Symeo were sealed xii. M. Of ye tribe of Leuy were sealed xii. M. Of ye trybe of Isacar were sealed xii. M.
12, 000 kutoka kabila ya Simioni, 12, 000 kutoka kabila ya Lawi, 12, 000 kutoka kabila ya Isakari,
8 Of the trybe of zabulon weee sealed xii. M. Of the tribe of Ioseph were sealed xii. M. Of the trybe of Beniamin were sealed xii. thowsande.
12, 000 kutoka kabila ya Zebuloni, 12, 000 kutoka kabila ya Yusufu, na 12, 000 kutoka kabila ya Benyamini walitiwa muhuri.
9 After this I behelde and lo a gret multitude (which noma coulde nombre) of all nacios and people and tonges stode before the seate and before the lambe clothed with longe whyte garmentes and palmes in there hondes
Baada ya mambo haya nilitazama, na kulikuwa na umati mkubwa ambao hapana mtu angeweza kuuhesabu - kutoka kila taifa, kabila, jamaa, na lugha - wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo. Walikuwa wamevaa kanzu nyeupe na wana matawi ya mitende mikononi mwao,
10 and cryed with a lowde voyce sayinge: salvacion be asscribed to him that syttith apon the seate of oure god and vnto the lambe.
na walikuwa wakiita kwa sauti ya juu: “Wokovu ni kwa Mungu ambaye ameketi katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo!”
11 And all the angelles stode in the compase of the seate and of the elders and of the iiii. bestes and fel before the seat on their faces and worshipped god
Malaika wote waliokuwa wamesimama kuzunguka kiti cha enzi na kuwazunguka wale wazee pamoja na wenye uhai wanne, wakainama chini ardhini na wakaweka nyuso zao juu ya ardhi mbele ya kiti cha enzi na wakamwabudu Mungu,
12 sayinge amen: Blessynge and glory wisdome and thankes and honour and power and myght be vnto oure god for evermore Amen. (aiōn g165)
wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukurani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
13 And one of the elders answered sayinge vnto me: what are these which are arayed in longe whyte garmentes and whence cam they?
Kisha mmoja wa wale wazee akaniuliza, “hawa ni akina nani waliovaa kanzu nyeupe, na wametoka wapi?
14 And I sayde vnto him: lorde thou wottest. And he sayde vnto me: these are they which cam oute of gret tribulacion and made their garmetes large and made them whyte in the bloud of the lambe:
Nikamwambia, “Bwana mkubwa, unajua wewe,” na akaniambia, “Hawa ni wale waliotoka katika dhiki kuu. Wamezifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe kwa damu ya Mwanakondoo.
15 therfore are they in the presence of the seate of God and serve him daye and nyght in hys temple and he that sytteth in the seate wyll dwell amonge them.
Kwa sababu hii, wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, na wanamwabudu yeye usiku na mchana katika hekalu lake. Yeye aliye keti juu ya kiti cha enzi atasambaza hema yake juu yao.
16 They shalt honger no more nether thyrst nether shall the sunne lyght on them nether eny heate:
Hawataona njaa tena, wala kiu tena. Jua halitawachoma, wala joto la kuunguza.
17 For the lambe which ys in the myddes of the seate shall fede them and shall ledde them vnto fountaynes of lyuynge water and god shall wype awaye all teares from their eyes.
Kwa kuwa Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, na atawaongoza katika chemchemi ya maji ya uzima, na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”

< Revelation 7 >