< Mark 2 >

1 After a feawe dayes he entred into Capernaum agayne and it was noysed that he was in a housse.
Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
2 And anone many gadered to geder in so moche that now there was no roume to receave them: no not so moche as about the dore. And he preached the worde vnto them.
Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
3 And there came vnto him that brought one sicke of the palsie borne of fower men.
Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
4 And because they coulde not come nye vnto him for preace they vncovered ye rofe of the housse where he was. And when they had broken it ope they let doune ye beed where in ye sicke of the palsie laye.
Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
5 When Iesus sawe their fayth he sayde to the sicke of the palsie sonne thy sinnes are forgeven the.
Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 And ther were certayne of ye scribes sittinge there and reasoninge in their hertes:
Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
7 how doeth this felowe so blaspheme? Who can forgeve synnes but God only?
“Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
8 And immediatly whe Iesus perceaved in his sprete yt they so reasoned in the selves he sayde vnto them: why thynke ye soche thinges in youre hertes?
Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
9 Whether is it easyer to saye to ye sicke of ye palsie thy synnes are forgeven the or to saye aryse take vp thy beed and walke?
Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
10 That ye maye knowe yt the sonne of man hath power in erth to forgeve synnes he spake vnto ye sicke of the palsie:
Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
11 I saye vnto ye aryse and take vp thy beed and get ye hense into thyne awne housse.
“Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
12 And by and by he arose toke vp the beed and went forth before them all: in so moche that they were all amased and glorified God sayinge: we never sawe it on this fassion.
Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
13 And he went agayne vnto the see and all the people resorted vnto him and he taught the.
Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
14 And as Iesus passed by he sawe Levy ye sonne of Alphey syt at the receyte of custome and sayde vnto him: folowe me. And he arose and folowed him.
Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
15 And it came to passe as Iesus sate at meate in his housse many publicans and synners sate at meate also with Iesus and his disciples. For there were many that folowed him.
Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
16 And when the Scribes and Pharises sawe him eate with publicas and synnere they sayde vnto his disciples: how is it that he eateth and drynketh with publicas and synners?
Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
17 When Iesus hearde yt he sayde vnto them. The whole have no nede of the phisicio but the sicke. I came not to call the rightwise but the synners to repentaunce.
Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
18 And the disciples of Iohn and the Pharises dyd faste: and therfore came and sayde vnto him. Why do ye disciples of Iohn and of the Pharises faste and thy disciples fast not.
Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
19 And Iesus sayde vnto them: can the chyldren of a weddinge faste while the brydgrome is wt them. As longe as they have the brydgrome with them they cannot faste.
Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
20 But the dayes will come when the brydgrome shalbe taken from them and then shall they faste in those dayes.
Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
21 Also no ma soweth a pece of newe cloth vnto an olde garmet for then taketh he awaye ye newe pece fro the olde and so is the rent worsse.
Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
22 In lyke wyse no man poureth newe wyne into olde vessels: for yf he do the newe wyne breaketh the vessels and the wyne runneth out and the vessels are marred. But new wyne must be poured into new vessels.
Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
23 And it chaunsed that he wet thorow ye corne feldes on the Saboth daye: and his disciples as they went on their waye beganne to plucke the eares of corne.
Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
24 And the Pharises sayde vnto him: beholde why do they on the Saboth dayes yt which is not laufull?
Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
25 And he sayde to them: have ye never rede what David dyd when he had nede and was anhogred bothe he and they that were with him?
Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
26 How he went into the housse of God in the dayes of Abiathar ye hye preste and dyd eate ye halowed loves which is not laufull to eate but for ye prestes only: and gave also to the which were with him?
Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
27 And he sayde to them: the Saboth daye was made for man and not man for the Saboth daye.
Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
28 Wherfore the sonne of man is Lorde eve of the Saboth daye.
Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”

< Mark 2 >