< Mark 3 >

1 And he entred agayne into ye synagoge and there was a man there which had a widdred honde.
Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
2 And they watched him to se whether he wolde heale him on the Saboth daye yt they might accuse him.
Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
3 And he sayde vnto ye man which had ye wyddred honde: arise and stonde in ye middes.
Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
4 And he sayd to them: whether is it laufull to do a good dede on ye Saboth dayes or an evyll? to save life or kyll? But they helde their peace.
Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
5 And he loked round aboute on them angerly mournyge on the blindnes of their hertes and sayde to the man: stretch forth thyne honde. And he stretched it oute. And his honde was restored even as whole as the other.
Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
6 And ye Pharises departed and streyght waye gaddred a counsell with the that belonged to Herode agaynst him yt they might destroye him.
Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
7 And Iesus auoyded wt his disciples to ye sea. And a greate multitude folowed him fro Galile and fro Iurie
Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
8 and fro Hierusalem and fro Idumea and fro beyonde Iordane: and they yt dwelled about Tyre and Sidon a greate multitude: which whe they had herde what thinges he dyd came vnto him.
na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
9 And he comaunded his disciples yt a shippe shuld wayte on him because of the people leste they shuld througe him.
Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
10 For he had healed many in somoche that they preased apon him for to touche him as many as had plages.
Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
11 And when the vnclene sprites sawe him they fell doune before him and cryed sayinge: thou arte the sonne of God.
Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
12 And he straygtly charged them that they shuld not vtter him.
Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
13 And he wet vp into a mountayne and called vnto him whom he wolde and they came vnto him.
Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
14 And he ordeyned ye. xii. that they shuld be wt him and that he myght sende the to preache:
Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
15 and that they might have power to heale syknesses and to cast out devyls.
na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
16 And he gave vnto Simon to name Peter.
Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
17 And he called Iames the sonne of zebede and Iohn Iames brother and gave them Bonarges to name which is to saye the sonnes of thounder.
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
18 And Andrew and Philip and Bartlemew and Mathew and Thomas and Iames the sonne of Alphey and Taddeus and Symon of Cane
na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 and Iudas Iscarioth which same also betrayed him. And they came vnto housse
na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
20 and the people assembled togedder agayne so greatly that they had not leesar so moche as to eate breed.
Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
21 And when they that longed vnto him hearde of it they went out to holde him. For they thought he had bene beside him selfe.
Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
22 And ye Scribes which came fro Ierusalem sayde: he hath Belzebub and by ye power of the chefe devyll casteth out devyls.
Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
23 And he called them vnto him and sayde vnto them in similitudes. How can Satan drive out Satan?
Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
24 For yf a realme be devided ageynste it silfe that realme cannot endure.
Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 Or yf a housse be devided agaynste it silfe that housse cannot continue:
Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 So yf Sata make insurreccion agaynste himsilfe and be devided he cannot continue but is at an ende.
Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
27 No man can entre into a stronge mans housse and take awaye hys gooddes excepte he fyrst bynde that stronge man and then spoyle hys housse.
Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
28 Verely I saye vnto you all synnes shalbe forgeven vnto mens chyldren and blasphemy wherwith they blaspheme.
Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
29 But he that blasphemeth ye holy goost shall never have forgevenes: but is in dauger of eternall dapnacion: (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 because they sayde he had an vnclene sprete.
Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
31 Then came his mother and his brethre and stode with out and sent vnto him and called him.
Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
32 And the people sate aboute hym and sayde vnto him: beholde thy mother and thy brethre seke for the with out.
Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
33 And he answered them sayinge: who is my mother and my brethre?
Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
34 And he loked rounde about on his disciples which sate in compasse about hym and sayde: beholde my mother and my brethren.
Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
35 For whosoever doeth ye will of God he is my brother my syster and mother.
Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.

< Mark 3 >