< Luke 7 >

1 When he had ended all his sainges in the audience of the people he entred into Capernau
Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
2 And a certayne Centurions seruaunte was sicke and redy to dye whom he made moche of.
Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
3 And when he hearde of Iesu he sent vnto him the elders of the Iewes besechinge him yt he wolde come and heale his servaunt.
Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
4 And they came to Iesus and besought him instantly sayinge: He is worthi that thou shuldest do this for him.
Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: “Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
5 For he loveth oure nacion and hath bilt vs a sinagoge
maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi.”
6 And Iesus went with them. And when he was not farre fro the housse the Centurio sent frendes to him sayinge vnto him: Lorde trouble not thy silfe: for I am not worthy yt thou shuldest enter vnder my roffe.
Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: “Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
7 Wherfore I thought not my silfe worthy to come vnto the: but saye the worde and my servaunt shalbe whoole.
Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
8 For I lyke wyse am a man vnder power and have vnder me soudiers and I saye vnto won goo: and he goeth. And to another come: and he cometh. And to my servaunt do this: and he doeth it.
Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya.”
9 When Iesus herde this he merveyled at him and turned him about and sayd to the people that folowed him: I saye vnto you I have not founde so greate faith noo not in Israel.
Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
10 And they yt were sent turned backe home agayne and founde the servaunt that was sicke whoole.
Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
11 And it fortuned after that that he went into a cite called Naim and many of his disciples went wt him and moche people.
Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
12 When he came nye to the gate of the cite: beholde ther was a deed man caried out which was ye only sonne of his mother and she was a widowe and moche people of the cite was with her.
Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
13 And when ye lorde sawe her he had compassion on her and sayde vnto her: wepe not.
Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, “Usilie.”
14 And he went and touched the coffyn and they yt bare him stode still. And he sayde: Yonge man I saye vnto the aryse.
Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, “Kijana! Nakuamuru, amka!”
15 And ye deed sate vp and beganne to speake. And he delyvered him to his mother.
Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16 And ther ca a feare on the all. And they glorified god sayinge: a greate prophet is rysen amoge vs and god hath visited his people
Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: “Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
17 And this rumor of him wet forthe throughout all Iurie and thorowout all the regions which lye rounde about.
Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
18 And ye disciples of Iohn shewed him of all these thinges.
Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
19 And Iohn called vnto him. ii. of his disciples and sent the to Iesus sayinge: Arte thou he that shall come: or shall we loke for another?
aliwatuma kwa Bwana wamwulize: “Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?”
20 When the men were come vnto him they sayde: Iohn baptiste sent vs vnto ye sayinge: Arte thou he that shall come: or shall we wayte for another?
Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, “Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?”
21 And at yt same tyme he cured many of their infirmites and plages and of evyll spretes and vnto many that were blynde he gave sight
Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
22 And Iesus answered and sayd vnto them: Goo youre wayes and shewe Iohn what thinges ye have sene and harde: how yt the blynde se the halt goo the lepers are clensed the deafe heare the deed aryse to the poore is the glad tydinges preached
Basi, Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
23 and happy is he that is not offended by me.
Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!”
24 When ye messengers of Iohn were departed he began to speake vnto ye people of Iohn What wet ye oute into ye wildernes for to se? went ye to se arede shaken wt ye wynde?
Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: “Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
25 But what went ye out for tose? A ma clothed in soofte rayment? Beholde they which are gorgeously apparelled and lyve delicatly are in kynges courtes.
Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
26 But what went ye forth to se? A prophete? Ye I saye to you and moare then a prophete
Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
27 This is he of who it is wrytte: Beholde I sende my messenger before thy face to prepare thy waye before the.
Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia.”
28 For I saye vnto you: a greater prophete then Iohn amoge wemes chyldre is ther none. Neverthelesse one yt is lesse in ye kyngdo of god is greater the he
Yesu akamalizia kwa kusema, “Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye.”
29 And all the people that hearde and the publicans iustified God and were baptised with the baptim of Iohn.
Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
30 But the pharises and scribes despised ye counsell of god agaynst them selves and were not baptised of him.
Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
31 And ye lorde sayd: Wher vnto shall I lyke the men of this generacion and what thinge are they lyke?
Yesu akaendelea kusema, “Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
32 They are lyke vnto chyldre sittynge in ye market place and cryinge one to another and sayinge: We have pyped vnto you and ye hahave not daunsed: we have mourned to you and ye have not wept.
Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
33 For Iohn baptist cam nether eatynge breed ner drinkynge wyne and ye saye: he hath the devyll.
Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
34 The sonne of man is come and eateth and drinketh and ye saye: beholde a man which is a glotton and a drinker of wyne a frende of publicans and synners.
Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
35 Yet is wysdome iustified of all her chyldren.
Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali.”
36 And one of the pharises desyred him that he wolde eate with him. And he went into ye pharises housse and sate doune to meate.
Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
37 And beholde a woman in that cite which was a synner assone as she knewe that. Iesus sate at meate in the pharises housse she brought an alablaster boxe of oyntmet
Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
38 and she stode at his fete behynde him wepynge and beganne to wesshe his fete with teares and dyd wipe the with the heares of her heed and kyssed his fete and anoynted them with oyntment.
Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
39 When the pharise which bade him sawe that he spake with in him sylfe sayinge: If this man were a prophete he wolde surely have knowen who and what maner woman this is which toucheth him for she is a synner.
Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, “Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.”
40 And Iesus answered and sayde vnto him: Simon I have some what to saye vnto ye. And he sayd master saye on.
Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, “Simoni, ninacho kitu cha kukwambia.” Naye Simoni akamwambia, “Ndio Mwalimu, sema.” Yesu akasema,
41 There was a certayne lender which had two detters ye one ought five hondred pence and the other fyfty.
“Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
42 When they had nothinge to paye he forgave the boothe. Which of them tell me will love him moost?
Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?”
43 Simon answered and sayde: I suppose that he to whom he forgave moost. And he sayde vnto him: Thou hast truly iudged.
Simoni akamjibu, “Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana.” Yesu akamwambia, “Sawa.”
44 And he turned to the woman and sayde vnto Simon: Seist thou this woman? I entred into thy housse and thou gavest me noo water to my fete but she hath wesshed my fete with teares and wiped the with the heeres of her heed.
Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, “Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
45 Thou gavest me no kysse: but she sence ye tyme I came in hath not ceased to kysse my fete
Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
46 Myne heed wt oyle thou dydest not anoynte: but she hath annoynted my fete wt oyntmet.
Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
47 Wherefore I saye vnto the: many synnes are forgeve her for she loved moche. To whom lesse is forgeven the same doeth lesse love.
Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo.”
48 And he sayde vnto her thy synnes are forgeven ye
Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, “Umesamehewa dhambi zako.”
49 And they yt sate at meate with him beganne to saye within them selves: Who is this which forgeveth synnes also?
Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, “Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?”
50 And he sayde to ye woman: Thy faith hath saved the Goo in peace.
Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”

< Luke 7 >