< Luke 6 >

1 It happened on an after saboth that he went thorow the corne felde and that his disciples plucked the eares of corne and ate and rubbed them in their hondes.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 And certayne of the Pharises sayde vnto them: Why do ye that which is not laufull to do on the saboth dayes?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 And Iesus answered them and sayde: Have ye not redde what David dyd when he him sylfe was anhungred and they which were with him:
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 how he went into the housse of God and toke and ate the loves of halowed breed and gave also to them which were with him: which was not laufull to eate but for the prestes only.
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 And he sayde vnto them: The sonne of man is Lorde of the saboth daye.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 And it fortuned in a nother saboth also that he entred in to ye sinagoge and taught. And ther was a ma whose right honde was dryed vp.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 And ye Scribes and Pharises watched him to se whether he wolde heale on the Saboth daye that they myght fynde an accusacion agaynst him.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 But he knewe their thoughtes and sayde to the man which had ye wyddred honde: Ryse vp and stonde forthe in the myddes. And he arose and stepped forthe.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Then sayde Iesus vnto them: I will axe you a question: Whether is it laufull on the saboth dayes to do good or to do evill? to save lyfe or for to destroye it?
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 And he behelde them all in copasse and sayd vnto ye man: Stretche forth thy honde. And he dyd so and his honde was restored and made as whoole as the other.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 And they were filled full of madnes and comuned one with another what they myght do to Iesu.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 And it fortuned in thoose dayes that he went out into a mountayne for to praye and cotinued all nyght in prayer to god.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 And assone as it was daye he called his disciples and of the he chose twelve which also he called apostles.
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simon who he named Peter: and Andrew his brother. Iames and Iho Philip and Bartlemew
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Mathew and Thomas Iames the sonne of Alpheus and Simon called zelotes
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 and Iudas Iames sonne and Iudas Iscarioth which same was the traytour.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 And he came doune with them and stode in the playne felde with the company of his disciples and agreate multitude of people out of all parties of Iurie and Ierusalem and from the see cooste of Tire and Sidon which came to heare hym and to be healed of their diseases:
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 and they also that were vexed with foule spretes and they were healed.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 And all the people preased to touche him: for there went vertue out of him and healed them all.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 And he lifted vp his eyes apon the disciples and sayde: Blessed be ye poore: for yours is the kyngdome of God.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Blessed are ye that honger now: for ye shalbe satisfied. Blessed are ye yt wepe now: for ye shall laugh.
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Blessed are ye when men hate you and thrust you oute of their companye and rayle and abhorre youre name as an evyll thinge for the sonne of manes sake.
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Reioyse ye then and be gladde: for beholde youre rewarde is greate in heven. After this manner their fathers entreated the Prophetes.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 But wo be to you that are ryche: for ye have therin youre consolacion.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Wo be to you yt are full: for ye shall honger. Wo be to you that now laugh: for ye shall wayle and wepe.
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Wo be to you when all men prayse you: for so dyd their fathers to the false prophetes.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 But I saye vnto you which heare: Love youre enemyes. Do good to the which hate you.
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 Blesse the that course you. And praye for the which wrongfully trouble you.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 And vnto him that smyteth the on the one cheke offer also ye other. And him that taketh awaye thy goune forbid not to take thy coote also.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Geve to every man that axeth of the. And of him that taketh awaye thy goodes axe them not agayne.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 And as ye wolde that men shuld doo to you: so do ye to them lyke wyse.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 If ye love the which love you: what thanke are ye worthy of? For the very synners love their lovers.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 And yf ye do for them which do for you: what thanke are ye worthy of? For the very synners do even the same.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 If ye lende to them of whome ye hoope to receave: what thanke shall ye have: for the very synners lende to synners to receave as moch agayne.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 Wherfore love ye youre enemys do good and lende lokynge for nothinge agayne and youre rewarde shalbe greate and ye shalbe the chyldren of the hyest: for he is kynde vnto the vnkynde and to the evyll.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Be ye therfore mercifull as youre father is mercifull.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Iudge not and ye shall not be Iudged. Condemne not: and ye shall not be condemned. Forgeve and ye shalbe forgeven.
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Geve and yt shalbe geven vnto you: good measure pressed doune shaken to geder and runnynge over shall men geve into youre bosomes. For with what measure ye mete with ye same shall men mete to you agayne.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 And he put forthe a similitude vnto the: Can the blynde leade ye blynde? Do they not both then fall into ye dyche?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 The disciple is not above his master. Every ma shalbe perfecte even as his master is.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 Why seyst thou a moote in thy brothers eye considerest not ye beame yt is in thyne awne eye?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Ether how canest thou saye to thy brother: Brother let me pull out ye moote that is in thyne eye: when thou perceavest not the beame that is in thyne awne eye? Ypocrite cast out ye beame out of thyne awne eye fyrst and then shalt thou se perfectly to pull out the moote out of thy brothers eye.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 It is not a good tree that bringeth forthe evyll frute: nether is that an evyll tree that bringeth forthe good frute
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 For every tree is knowen by his frute. Nether of thornes gader men fygges nor of busshes gader they grapes.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 A good man out of the good treasure of his hert bringeth forthe that which is good. And an evyll man out of the evyll treasure of his hert bringeth forthe that which ys evyll. For of the aboundaunce of ye her his mouthe speakethe.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 Why call ye me Master Master: and do not as I bid you?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 whosoever cometh to me and heareth my sayinges and dothe the same I will shewe you to whome he ys lyke.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 He is like a man which bilt an housse: and digged depe and layde the foundacio on a rocke. Whe the waters arose the fludde bet apo that housse and coulde not move yt. For it was grounded apon a rocke.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 But he that heareth and doth not is lyke a man that with out foundacion bylt an housse apon the erth agaynst which the fludde did bet: and it fell by and by. And ye fall of yt housse was greate.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >