< Luke 20 >

1 And yt fortuned in one of those dayes as he taught the people in the temple and preached the gospell: the hye prestes and the scribes came with the elders
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 and spake vnto him sayinge. Tell vs by what auctorite thou doest these thinges? Ether who is he yt gave ye this auctorite?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 He answered and saide vnto the: I also will axe you a questio and answer me.
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 The baptyme of Iohn: was it from heaven or of men?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 And they thought with in them selves sayinge: yf we shall saye from heave: he will saye: why then beleved ye him not?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But and yf we shall saye of men all ye people will stone vs. For they be persuaded that Ihon is a Prophet.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 And they answered that they coulde not tell whence it was.
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 And Iesus sayde vnto them: nether tell I you by what auctorite I do these thinges.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 Then begane he to put forthe to the people this similitude. A certayne man planted a vyneyarde and let it forthe to fermers and went him selfe into a straunge countre for a greate season.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 And when the tyme was come he sent a servaut to his tennauntes that they shuld geve him of the frutes of the vyneyarde. And the tennauntes dyd bet him and sent him awaye empty.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 And agayne he sent yet another servaunt. And they dyd bet him and foule entreated him also and sent him awaye emptye.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 Moreover he sent the thyrde to and him they wouded and cast out.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 Then sayde the lorde of the vyneyarde: what shall I do? I will sende my deare sonne him peradventure they will reverence when they se him.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 But when the fermers sawe him they thought in them selves sayinge: this is the heyre come let vs kyll him that the inheritaunce maye be oures.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 And they cast him out of the vyneyarde and kylled him. Now what shall the Lorde of the vyneyarde do vnto them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroye those fermers and will let out his vyneyarde to other. When they hearde that they sayde: God forbyd.
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 And he behelde them and sayde: what meaneth this then yt is wrytten: The stone that the bylders refused the same is made ye heed corner stone?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 whosoever stomble at that stone shalbe broken: but on whosoever it faul vpon it wyll grynde him to powder.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 And the hye Prestes and the Scribes the same howre went about to laye hondes on him but they feared the people. For they perceaved that he had spoken this similitude agaynst them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 And they watched him and sent forth spies which shuld fayne them selves perfecte to take him in his wordes and to delyvre him vnto the power and auctorite of the debite.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 And they axed him sayinge: Master we knowe that thou sayest and teachest ryght nother cosiderest thou eny manes degre but teachest the waye of God truly.
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Ys it laufull for vs to geve Cesar tribute or no?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 He perceaved their craftynes and sayde vnto them: why tept ye me?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Shewe me a peny. Whose ymage and superscripcio hath it? They answered and sayde: Cesars.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 And he sayde vnto them: Geve then vnto Cesar that which belongeth vnto Cesar: and to God that which pertayneth to God.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 And they coulde not reprove his sayinge before the people. But they marvayled at his answer and helde their peace.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Then came to him certayne of the Saduces which denye that ther is eny resurreccio. And they axed him
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 sayinge: Master Moses wrote vnto vs if eny mannes brother dye havinge a wyfe and the same dye with out yssue: that then his brother shuld take his wyfe and reyse vp seede vnto his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 Ther were seven brethren and the fyrste toke a wyfe and dyed with out children.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 And the seconde toke the wyfe and he dyed chyldlesse.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 And the thyrde toke her and in lyke wyse the resydue of the seven and leeft no chyldren be hynde them and dyed.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 Last of all the woma dyed also.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Now at the resurreccio whose wyfe of them shall she be? For seven had her to wyfe.
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 Iesus answered and sayde vnto them. The chyldre of this worlde mary wyves and are maryed (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 but they which shalbe made worthy to enioye that worlde and the resurreccion from deeth nether mary wyves nether are maryed (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 nor yet can dye eny moare. For they are equall vnto the angels: and are the sonnes of God in as moche as they are the chyldre of the resurreccion.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 And that the deed shall ryse agayne even Moses signified besydes the busshe when he sayde: the Lorde God of Adraham and the God of Isaac and the God of Iacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 For he is not the God of the deed but of them which live. For all live in him.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Then certayne of the Pharises answered and sayde: Master thou hast well sayde.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 And after that durst they not axe him eny question at all.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 Then sayde he vnto them: how saye they that Christ is Davids sonne?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 And David him selfe sayth in the boke of the Psalmes: The Lorde sayde vnto my Lorde syt on my right honde
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 tyll I make thine enemys thy fothe stole.
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 Seinge David calleth him Lorde: How is he then his sonne.
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 Then in the audience of all the people he sayde vnto his disciples
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 beware of the Scribes which desyre to goo in longe clothinge: and love gretynges in the markets and the hyest seates in the synagoges and chefe roumes at feastes
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 which devoure widdowes houses and that vnder a coloure of longe prayinge: the same shall receave greater damnacion.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luke 20 >