< Luke 19 >

1 And he entred in and went thorow Hierico.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 And beholde ther was a ma named Zacheus which was a ruler amoge the Publicans and was riche also.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 And he made meanes to se Iesus what he shuld be: and coulde not for the preace because he was of a lowe stature.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 Wherfore he ran before and asceded vp into a wilde fygge tree to se him: for he shulde come that same waye.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And when Iesus cam to the place he loked vp and sawe him and sayd vnto him: zache attonce come doune for to daye I must abyde at thy housse.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 And he came doune hastelye and receaved him ioyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 And when they sawe that they all groudged sayinge: He is gone in to tary with a man that is a synner.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 And zache stode forth and sayd vnto ye Lorde: beholde Lorde ye haulfe of my gooddes I geve to the povre and if I have done eny ma wroge I will restore him fower folde.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 And Iesus sayd to him: this daye is healthe come vnto this housse for as moche as it also is become the chylde of Abraha.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the sonne of ma is come to seke and to save that which was looste.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 As they hearde these thinges he added ther to a similitude be cause he was nye to Hierusalem and because also they thought that the kyngdome of God shuld shortely appere.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 He sayde therfore: a certayne noble man wet into a farre countre to receave him a kyngdome and then to come agayne.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 And he called his ten servauntes and delyvered them ten pounde sayinge vnto them: by and sell till I come.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his citesens hated him and sent messengers after him sayinge: We will not have this man to raygne over vs.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 And it came to passe when he was come agayne and had receaved his kyngdome he comaunded these servautes to be called to him (to whom he gave his money) to witt what every man had done.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Then came ye fyrst sayinge: Lorde thy pounde hath encreased ten poude.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 And he sayde vnto him: Well good servaute because thou wast faithfull in a very lytell thynge take thou auctorite over ten cities.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 And the other came sayinge: Lorde thy poude hath encreased fyve pounde.
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 And to ye same he sayde: and be thou also ruler ouer fyve cities.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 And the thyrde came and sayde: Lorde beholde here thy pounde which I have kepte in a napkyn
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 for I feared the because thou arte a strayte man: thou takest vp that thou laydest not doune and repest that thou dyddest not sowe.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 And he sayde vnto him: Of thine awne mouth iudge I the thou evyll servaunt. knewest thou that I am a strayte man takinge vp that I layde not doune and repinge that I dyd not sowe?
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Wherfore then gavest not thou my money into the banke that at my cominge I might have required myne awne with vauntage?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 And he sayde to them that stode by: take fro him that pounde and geve it him that hath ten poude.
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 And they sayd vnto him: Lorde he hath ten pounde.
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 I saye vnto you that vnto all the that have it shalbe geve: and from him yt hath not eve that he hath shalbe taken from him.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Moreover those myne enemys which wolde not that I shuld raigne over them bringe hidder and slee them before me.
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 And when he had thus spoken he proceded forthe before a ssendinge vp to Ierusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 And it fortuned when he was come nye to Bethphage and Bethany besydes moute olivete he sent two of his disciples
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 sayinge: Goo ye in to the toune which is over agaynste you. In the which assone as ye are come ye shall finde a colte tyed wheron yet never man sate. Lowse him and bringe him hider.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if eny man axe you why that ye loowse him: thus saye vnto him ye lorde hath nede of him.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 They that were sent went their waye and founde eve as he had sayde vnto the.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 And as they were aloosinge ye coolte the owners sayde vnto the: why lowse ye ye coolte?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 And they sayde: for ye Lorde hath nede of him.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 And they brought him to Iesus. And they cast their raymet on ye colte and set Iesus thero.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 And as he wet they spredde their clothes in ye waye.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when he was now come wheare he shuld goo doune fro the moute olivete ye whole multitude of ye disciples began to reioyce and to lawde God with a loude voyce for all ye miracles yt they had sene
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 sayinge: Blessed be the kynge that cometh in the name of the Lorde: peace in heave and glory in the hyest.
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 And some of ye Pharises of the copany sayde vnto him: Master rebuke thy disciples.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 He answered and sayde vnto the: I tell you yf these shuld holde their peace the stones wold crye.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 And when he was come neare he behelde the citie and wept on it
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 sayinge: Yf thou haddest dest knowen those thinges which belonge vn thy peace eve at this thy tyme. But now are they hydde from thyne eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the dayes shall come vpo the that thy enemys shall cast a banke aboute the and copasse the rounde and kepe the in on every syde
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 and make the even with the grounde with thy chyldren which are in the. And they shall not leve in the one stone vpo another because thou knewest not the tyme of thy visitacion.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And he went in to the temple and begane to cast out them that solde therin and them that bought
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 sayinge vnto them yt is written: my housse is the housse of prayer: but ye have made it a den of theves.
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And he taught dayly in the temple. The hye Prestes and the Scribes and the chefe of the people went about to destroye him:
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 but coulde not finde what to do. For all the people stacke by him and gave him audience.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >