< Luke 21 >

1 As he behelde he sawe the ryche men how they cast in their offeringes into the treasury.
Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2 And he sawe also a certayne povre widdowe which cast in thyther two mites.
akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3 And he sayde: of a trueth I saye vnto you this poore wyddowe hath put in moare then they all.
Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4 For they all have of their superfluyte added vnto the offerynge of God: but she of her penury hath cast in all the substaunce that she had.
Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
5 As some spake of the teple how it was garnesshed with goodly stones and iewels he sayde.
Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6 The dayes will come whe of these thynges which ye se shall not be lefte stone apon stone that shall not be throwen doune.
“Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
7 And they axed him sayinge: Master whe shall these thinges be and what signe will therbe whe suche thinges shall come to passe.
Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
8 And he sayd: take hede that ye be not deceaved. For many will come in my name saying: I am he: and the tyme draweth neare. Folowe ye not them therfore.
Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9 But when ye heare of warre and of dissencion: be not afrayd. For these thinges must fyrst come: but the ende foloweth not by and by.
Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
10 Then sayd he vnto the: Nacion shall ryse agaynst nacion and kingdom agaynst kyngdome
Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11 and greate erthquakes shall be in all quarters and honger and pestilence: and fearfull thinges. And greate signes shall therbe from heven.
Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12 But before all these they shall laye their hondes on you and persecute you delyueringe you vp to the sinagoges and into preson and bringe you before kynges and rulers for my names sake.
Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13 And this shall chaunce you for a testimoniall.
Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14 Let it sticke therfore faste in youre hertes not once to stody before what ye shall answere:
Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15 for I will geve you a mouth and wisdome where agaynste all youre adversarys shall not be able to speake nor resist.
kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16 Ye and ye shalbe betrayed of youre fathers and mothers and of youre brethren and kynsmen and lovers aud some of you shall they put to deeth.
Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17 And hated shall ye be of all men for my names sake.
Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18 Yet ther shall not one heer of youre heedes perisshe.
Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19 With youre pacience possesse youre soules.
Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20 And when ye se Ierusalem beseged with an hoste then vnderstonde that the desolacio of the same is nye.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21 Then let them which are in Iewrye flye to the mountaynes. And let them which are in the middes of it departe oute. And let not them that are in other countreis enter ther in.
Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22 For these be the dayes of vengeance to fulfill all that are writte.
Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23 But wo be to them that be with chylde and to them that geve sucke in those dayes: for ther shalbe greate trouble in the londe and wrath over all this people.
Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24 And they shall fall on the edge of the swearde and shalbe leed captive into all nacions. And Ierusalem shalbe trooden vnder fote of the gentyls vntyll the tyme of the gentyls be fulfilled.
Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25 And ther shalbe signes in the sunne ad in the mone and in the starres: and in ye erth the people shalbe in soche perplexite yt they shall not tell which waye to turne them selves. The see and the waters shall roore
“Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26 and menes hertes shall fayle them for feare and for lokinge after thoose thinges which shall come on the erth. For the powers of heve shall move.
Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 And then shall they se the sonne of ma come in a clowde with power and greate glory.
Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28 When these thinges begyn to come to passe: then loke vp and lifte vp youre heddes for youre redemcion draweth neye.
Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
29 And he shewed the a similitude: beholde ye fygge tree and all other trees
Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
30 when they shute forth their buddes ye se and knowe of youre awne selves that sommer is then nye at hod.
Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31 So lyke wyse ye (when ye se these thinges come to passe) vnderstonde that the kyngdome of God is neye.
Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Verely I saye vnto you: this generacion shall not passe tyll all be fulfilled.
Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33 Heaven and erth shall passe: but my wordes shall not passe.
Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34 Take hede to youre selves lest youre hertes be overcome with surfettinge and dronkennes and cares of this worlde: and that that daye come on you vnwares.
“Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35 For as a snare shall it come on all them that sit on the face of the erthe.
Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36 Watche therfore continually and praye that ye maye obtayne grace to flye all this that shall come and that ye maye stonde before the sonne of man.
Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
37 In the daye tyme he taught in the temple and at night he went out and had abydinge in the mount olivete.
Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38 And all the people came in the morninge to him in the temple for to heare him.
Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.

< Luke 21 >