< John 5 >

1 After that ther was a feast of the Iewes and Iesus went vp to Ierusalem.
Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
2 And ther is at Ierusalem by ye slaughterhousse a pole called in ye Ebrue toge Bethseda havinge five porches
Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
3 in which laye a greate multitude of sicke folke of blinde halt and wyddered waytinge for the movinge of the water.
Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
4 For an angell wet doune at a certayne ceason into ye pole and troubled ye water. Whosoever then fyrst after the steringe of the water stepped in was made whoale of what soever disease he had.
Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
5 And a certayne ma was theare which had bene diseased. xxxviii. yeares
Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
6 When Iesus sawe him lye and knewe that he now longe tyme had bene diseased he sayde vnto him. Wilt thou be made whoale?
Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
7 The sicke answered him: Syr I have no man whe the water is troubled to put me into the pole. But in the meane tyme whill I am about to come another steppeth doune before me.
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
8 And Iesus sayde vnto him: ryse take vp thy beed and walke.
Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
9 And immediatly the man was made whole and toke vp his beed and went. And the same daye was the Saboth daye
Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
10 The Iewes therfore sayde vnto him that was made whole. It is ye Saboth daye it is not laufull for the to cary thy beed
Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
11 He answered them: he that made me whole sayde vnto me: take vp thy beed and get the hence.
Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
12 Then axed they him: what man is that which sayde vnto the take vp thy beed and walke.
Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
13 And he yt was healed wist not who it was. For Iesus had gotte him selfe awaye be cause yt ther was preace of people in ye place.
Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
14 And after that Iesus founde him in the teple and sayd vnto him: beholde thou arte made whole synne no moore lest a worsse thinge happe vnto the.
Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
15 The man departed and tolde ye Iewes that yt was Iesus whiche had made him whole.
Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
16 And therfore the Iewes dyd persecute Iesus and sought the meanes to slee him because he had done these thinges on the Saboth daye.
Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
17 And Iesus answered them: my father worketh hidder to and I worke.
Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
18 Therfore the Iewes sought the moare to kill him not only because he had broken the Saboth: but sayde also that God was his father and made him selfe equall with God.
Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
19 Then answered Iesus and sayde vnto them: verely verely I saye vnto you: the sonne can do no thinge of him selfe but that he seeth ye father do. For whatsoever he doeth yt doeth the sonne also.
Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
20 For the father loveth ye sonne and sheweth him all thinges whatsoever he him selfe doeth. And he will shewe him greter workes then these because ye shoulde marvayle.
Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
21 For lykwyse as the father rayseth vp ye deed and quickeneth them even so the sonne quyckeneth whom he will.
Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
22 Nether iudgeth ye father eny ma: but hath comitted all iudgemet vnto the sonne
Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
23 because that all men shuld honoure the sonne eve as they honoure the father. He that honoureth not ye sonne the same honoureth not the father which hath sent him.
ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
24 Verely verely I saye vnto you: He that heareth my wordes and beleveth on him that sent me hath everlastinge lyfe and shall not come into damnacion: but is scaped fro deth vnto lyfe. (aiōnios g166)
Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios g166)
25 Verely verely I saye vnto you: the tyme shall come and now is when the deed shall heare the voyce of the sonne of God. And they yt heare shall live.
Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
26 For as the father hath life in him silfe: so lyke wyse hath he geven to ye sonne to have lyfe in him silfe:
Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
27 and hath geven him power also to iudge in that he is the sonne of man.
kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
28 Marvayle not at this ye houre shall come in the which all yt are in the graves shall heare his voice
Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
29 and shall come forthe: they that have done good vnto the resurreccion of lyfe: and they that have done evyll vnto the resurreccion of dampnacion.
nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
30 I can of myne awne selfe do nothinge at all. As I heare I iudge and my iudgemet is iust because I seke not myne awne will but the will of ye father which hath sent me.
Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
31 Yf I beare witnes of my selfe my witnes is not true.
Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
32 Ther is a nother that beareth witnes of me and I am sure that the witnes whiche he beareth of me is true.
Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
33 Ye sent vnto Iohn and he bare witnes vnto the truthe.
Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
34 But I receave not the recorde of man. Neverthelesse these thinges I saye that ye might be safe.
Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
35 He was a burninge and a shyninge light and ye wolde for a season have reioysed in his light.
Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
36 But I have greater witnes then the witnes of Iohn. For ye workes which ye father hath geve me to fynisshe: the same workes which I do beare witnes of me that ye father sent me.
Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
37 And the father him silfe which hath sent me beareth witnes of me. Ye have not hearde his voyce at eny tyme nor ye have sene his shape:
Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38 therto his wordes have ye not abydinge in you. For whome he hath sent: him ye beleve not.
Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39 Searche the scriptures for in them ye thinke ye have eternall lyfe: and they are they which testify of me. (aiōnios g166)
Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios g166)
40 And yet will ye not come to me that ye might have lyfe.
hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
41 I receave not prayse of men.
Sipokei sifa kutoka kwa watu,
42 But I knowe you that ye have not the love of God in you
lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
43 I am come in my fathers name and ye receave me not. Yf another shall come in his awne name him will ye receave.
Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
44 How can ye beleve which receave honoure one of another and seke not the honoure that commeth of God only?
Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
45 Doo not thinke that I wyll accuse you to my father. Ther is one that accuseth you eve Moses in whom ye trust.
Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
46 For had ye beleved Moses ye wold have beleved me: for he wrote of me.
Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
47 But now ye beleve not his writinge: how shall ye beleve my wordes.
Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?

< John 5 >