< Acts 1 >

1 In the former treatise (Deare frende Theophilus) I have written of all that Iesus beganne to do and teache
Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
2 vntyll the daye in the which he was taken vp after that he thorowe the holy goost had geven commaundementes vnto the Apostles which he had chosen:
mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
3 to whom also he shewed him selfe alyve after his passion by many tokens apperynge vnto them fourty dayes and speakynge of the kyngdome of god
Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
4 and gaddered them togeder and commaunded the that they shuld not departe from Ierusalem: but to wayte for ye promys of the father whereof ye have herde of me.
Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
5 For Iohn baptised wt water: but ye shalbe baptised with the holy goost and that with in this feawe dayes.
kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
6 When they were come togeder they axed of him sayinge: Lorde wilt thou at this tyme restore agayne ye kyngdome to Israel?
Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
7 And he sayde vnto them: It is not for you to knowe the tymes or the seasons which ye father hath put in his awne power:
Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
8 but ye shall receave power of the holy goost which shall come on you. And ye shall be witnesses vnto me in Ierusalem and in all Iewrye and in Samary and even vnto the worldes ende.
Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
9 And when he had spoken these thinges whyll they behelde he was take vp and a cloude receaved him vp out of their sight.
Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
10 And while they looked stedfastly vp to heaven as he went beholde two men stode by them in white apparell
Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
11 which also sayde: ye men of Galile why stonde ye gasinge vp into heave? This same Iesus which is taken vp fro you in to heaven shall so come even as ye haue sene him goo into heaven.
Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
12 Then returned they vnto Ierusalem from mount olivete which is nye to Ierusalem coteyninge a Saboth dayes iorney.
Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
13 And when they were come in they went vp into a parler where abode both Peter and Iames Iohn and Andrew Philip and Thomas Bartlemew and Mathew Iames the sonne of Alpheus and Simo Zelotes and Iudas Iames sonne.
Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
14 These all cotinued with one acorde in prayer and supplicacion with the wemen and Mary the mother of Iesu and with his brethren.
Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
15 And in those dayes Peter stode vp in the myddes of the disciples and sayde (the noumbre of names that were to gether were aboute an hondred and twenty)
Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
16 Ye men and brethren this scripture must have nedes ben fulfilled which the holy goost thorow ye mouth of David spake before of Iudas which was gyde to them that tooke Iesus.
Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
17 For he was noubred with vs and had obtayned fellouship in this ministracion.
Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
18 And the same hath now possessed a plot of grounde with the rewarde of iniquite and when he was hanged brast a sondre in ye myddes and all his bowels gusshed oute.
(Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
19 And it is knowe vnto all the inhabiters of Ierusalem: in so moche that that felde is called in their mother tonge Acheldama that is to saye the bloud felde.
Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
20 It is written in the boke of Psalmes: His habitacio be voyde and no man be dwellinge therin: and his bisshoprycke let another take.
“Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
21 Wherfore of these me which have copanyed with vs all ye tyme that the Lorde Iesus wet in and out amonge vs
Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
22 begynninge at the baptyme of Iohn vnto that same daye that he was taken vp from vs must one be ordeyned to be are witnes with vs of his resurreccion.
kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
23 And they appoynted two Ioseph called Barsabas (whose syr name was Iustus) and Mathias.
“Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
24 And they prayed sayinge: thou Lorde which knowest the hertes of all me shewe whether of these two thou hast chosen
Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
25 that the one maye take the roume of this ministracion and apostleshippe from the which Iudas by transgression fell that he myght go to his awne place.
kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
26 And they gave forthe their lottes and the lot fell on Mathias and he was counted with the eleven Apostles.
Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.

< Acts 1 >