< Romans 1 >

1 Paul the seruaut of Iesus Christ called to be an Apostle put a parte to preache the Gospell of God
Paulo, mtumishi wa Yesu Kristo, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu.
2 which he promysed afore by his Prophetes in the holy scriptures
Hii ndio ile Injili aliyoiahidi zamani kupitia manabii wake katika maandiko matakatifu.
3 that make mension of his sonne the which was begotte of the seed of David as pertayninge to the flesshe:
Ni kuhusu Mwana wake, aliyezaliwa kutoka ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili.
4 and declared to be the sonne of God with power of the holy goost that sanctifieth sence ye tyme that Iesus Christ oure Lorde rose agayne from deeth
Yeye alitangazwa kwa Mwana wa Mungu kwa nguvu ya Roho ya utakatifu kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu.
5 by whom we have receaved grace and apostleshyppe to bringe all maner hethe people vnto obedience of the fayth that is in his name:
Kupitia yeye tumepokea neema na utume kwa utii wa imani kati ya mataifa yote, kwa ajili ya jina lake.
6 of the which hethen are ye a part also which are Iesus christes by vocacio.
Kati ya mataifa haya, ninyi pia mmeitwa kuwa wa Yesu Kristo.
7 To all you of Rome beloved of God and saynctes by callinge. Grace be with you and peace from God oure father and from the Lorde Iesus Christ.
Barua hii ni kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watu watakatifu. Neema na iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8 Fyrst verely I thanke my God thorow Iesus Christ for you all because youre fayth is publisshed through out all the worlde.
Kwanza, namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.
9 For God is my witnes whom I serve with my sprete in the Gospell of his sonne that with out ceasinge I make mencion of you alwayes in my prayers
Kwa maana Mungu ni shahidi wangu, ambaye ninamtumikia kwa roho yangu katika injili ya Mwana wake, jinsi ninavyodumu katika kuwataja.
10 besechinge that at one tyme or another a prosperous iorney (by ye will of god) myght fortune me to come vnto you.
Daima naomba katika sala zangu kwamba kwa njia yoyote nipate mwishowe kuwa na mafanikio sasa kwa mapenzi ya Mungu katika kuja kwenu.
11 For I longe to see you that I myght bestowe amoge you some spirituall gyfte to strength you with all:
Maana natamani kuwaona, ili nipate kuwapa ninyi baadhi ya karama za rohoni, nipate kuwaimarisha.
12 that is that I myght have consolacion together with you through the commen fayth which bothe ye and I have.
Yaani, natazamia kutiwa moyo pamoja nanyi, kwa njia ya imani ya kila mmoja wetu, yenu na yangu.
13 I wolde that ye shuld knowe brethre how that I have often tymes purposed to come vnto you (but have bene let hitherto) to have some frute amonge you as I have amonge other of ye Gentyls.
Sasa ndugu, sitaki mkose kufahamu kwamba, mara nyingi nimekusudia kuja kwenu, lakini nimezuiliwa mpaka sasa. Nilitaka hivi ili kuwa na matunda kwenu kama ilivyo pia miongoni mwa watu wa mataifa.
14 For I am detter both to the Grekes and to them which are no Grekes vnto the learned and also vnto the vnlearned.
Nadaiwa na Wayunani na wageni pia, werevu na wajinga.
15 Lykewyse as moche as in me is I am redy to preache the Gospell to you of Rome also.
Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi niko tayari kutangaza injili kwenu pia ninyi mlio huko Roma.
16 For I am not ashamed of the Gospell of Christ because it is ye power of God vnto salvacio to all yt beleve namely to the Iewe and also to ye getyle.
Kwa maana siionei haya injili, kwa kuwa ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza na kwa Myunani pia.
17 For by it ye rightewesnes which cometh of god is opened fro fayth to fayth. As it is written: The iust shall live by fayth.
Kwa maana haki ya Mungu imedhihirishwa kutoka imani hata imani, kama ilivyo andikwa, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
18 For the wrath of God apereth from heven agaynst all vngodlynes and vnrightewesnes of me which withholde ye trueth in vnrightewesnes
Maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa watu, ambao kwa njia ya udhalimu huificha kweli.
19 seynge what maye be knowen of God that same is manifest amoge them. For God dyd shewe it vnto them.
Hii ni kwa sababu, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao. Maana Mungu amewafahamisha.
20 So that his invisible thinges: that is to saye his eternall power and godhed are vnderstonde and sene by the workes from the creacion of the worlde. So that they are without excuse (aïdios g126)
Maana mambo yake yasioonekana vizuri yamekuwa wazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Yanaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa. Mambo haya ni uwezo wake wa milele na asili ya uungu. Matokeo yake, watu hawa hawana udhuru. (aïdios g126)
21 in as moche as when they knewe god they glorified him not as God nether were thakfull but wexed full of vanities in their imaginacions and their folisshe hertes were blynded.
Hii ni kwa sababu, ingawa walijua kuhusu Mungu, hawakumtukuza yeye kama Mungu, wala hawakumpa shukrani. Badala yake, wamekuwa wapumbavu katika mawazo yao, na mioyo yao yenye ujinga ilitiwa giza.
22 When they couted them selves wyse they became foles
Walijiita kuwa ni werevu, lakini wakawa wajinga.
23 and turned the glory of the immortall god vnto the similitude of the ymage of mortall man and of byrdes and foure foted beastes and of serpentes.
Waliubadili utukufu wa Mungu asie na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, ya wanyama wenye miguu minne, na ya viumbe vitambaavyo.
24 Wherfore god lykewyse gave the vp vnto their hertes lustes vnto vnclennes to defyle their awne boddyes bitwene them selves:
Kwa hiyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa za mioyo yao kwa uchafu, kwa miili yao kufedheheshwa baina yao.
25 which tourned his truthe vnto a lye and worshipped and served the creatures more then ye maker which is blessed for ever. Ame. (aiōn g165)
Ni wao walioibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, na ambao waliabudu na kutumikia viumbe badala ya Muumbaji, ambaye anasifiwa milele. Amina. (aiōn g165)
26 For this cause god gave them vp vnto shamfull lustes. For even their wemen did chaunge the naturall vse vnto the vnnaturall.
Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, kwa kuwa wanawake wao walibadilisha matumizi yao ya asili kwa kile kilicho kinyume na asili.
27 And lyke wyse also the men lefte the naturall vse of the woma and bret in their lustes one on another. And man with man wrought filthynes and receaved in them selves the rewarde of their erroure as it was accordinge.
Hali kadhalika, wanaume pia wakaacha matumizi yao ya asili kwa wanawake na kuwakwa na tamaa dhidi yao wenyewe. Hawa walikuwa wanaume ambao walifanya na wanaume wenzao yasiyo wapasa, na ambao walipokea adhabu iliyostahili upotovu wao.
28 And as it semed not good vnto them to be aknowen of God even so God delivered them vp vnto a leawde mynd yt they shuld do tho thinges which were not comly
Kwa sababu walikataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wafanye mambo yale yasiyofaa.
29 beinge full of all vnrighteous doinge of fornicacio wickednes coveteousnes maliciousnes full of envie morther debate disseyte evill codicioned whisperers
Wamejawa na udhalimu wote, uovu, tamaa na ubaya. Wamejawa na wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu, na nia mbaya.
30 backbyters haters of God doers of wroge proude bosters bringers vp of evyll thinges disobedient to father and mother
Wao pia ni wasengenyaji, wasingiziaji, na wenye kumchukia Mungu. Wenye vurugu, kiburi, na majivuno. Wao ni watunga mabaya, na wasiotii wazazi wao.
31 with out vnderstondinge covenaunte breakers vnlovinge trucebreakers and merciles.
Wao hawana ufahamu; wasioaminika, hawana mapenzi ya asili, na wasio na huruma.
32 Which me though they knew the rightewesnes of God how that they which soche thinges commyt are worthy of deeth yet not only do the same but also have pleasure in them that do them.
Wanaelewa kanuni za Mungu, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo wanastahili kifo. Lakini si tu wanafanya mambo hayo, wao pia wanakubaliana na wale wanaofanya mambo hayo.

< Romans 1 >