< John 4 >

1 Assone as the Lorde had knowledge how the Pharises had hearde that Iesus made and baptised moo disciples then Iohn
Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
2 (though that Iesus him selfe baptised not: but his disciples)
(ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
3 he lefte Iewry and departed agayne into Galile.
alitoka Judea na akaenda Galilaya.
4 And it was so that he must nedes goo thorowe Samaria.
Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
5 Then came he to a cyte of Samaria called Sichar besydes the possession that Iacob gave to his sonne Ioseph.
Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
6 And there was Iacobs well. Iesus then weryed in his iorney sate thus on the well. And it was about the sixte houre:
Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
7 and there came a woman of Samaria to drawe water. And Iesus sayde vnto her: geve me drynke.
Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
8 For his disciples were gone awaye vnto the toune to bye meate.
Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
9 Then sayde the woman of Samaria vnto him: how is it that thou beinge a Iewe axest drinke of me which am a Samaritane? for the Iewes medle not with the Samaritans.
Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
10 Iesus answered and sayde vnto hir: yf thou knewest the gyfte of God and who it is that sayeth to the geve me drynke thou woldest have axed of him and he wolde have geven the water of lyfe.
Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
11 The woman sayde vnto him. Syr thou hast no thinge to drawe with and the well is depe: from whence then hast thou yt water of lyfe?
Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
12 Arte thou greater then oure father Iacob which gave vs the well and he him silfe dranke therof and his chyldren and his catell?
Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
13 Iesus answered and sayde vnto hir: whosoever drinketh of this water shall thurst agayne.
Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
14 But whosoever shall drinke of ye water yt I shall geve him shall never be more a thyrst: but the water that I shall geve him shalbe in him a well of water springinge vp in to everlastinge lyfe. (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woma sayd vnto him: Syr geve me of that water that I thyrst not nether come hedder to drawe.
Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
16 Iesus sayde vnto her. Go and call thy husband and come hydder.
Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
17 The woman answered and sayde to him: I have no husband.
Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
18 Iesus sayde to her. Thou hast well sayd I have no husbande. For thou haste had five husbandes and he whom thou now hast is not thy husband. That saydest thou truely.
kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
19 The woman sayde vnto him: Syr I perceave yt thou arte a prophet.
Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
20 Oure fathers worshipped in this mountayne: and ye saye that in Hierusalem is the place where men ought to worshippe.
Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
21 Iesus sayde vnto her: woman beleve me the houre cometh when ye shall nether in this moutayne nor yet at Ierusalem worshippe the father.
Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
22 Ye worshippe ye wot not what: we knowe what we worshippe. For salvacion cometh of the Iewes.
Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
23 But the houre commeth and nowe is when the true worshippers shall worshippe the father in sprete and in trouthe. For verely suche the father requyreth to worshippe him.
Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
24 God is a sprete and they that worshippe him must worshippe him in sprete and trouthe.
Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
25 The woman sayde vnto him: I wot well Messias shall come which is called Christ. When he is come he will tell vs all thinges.
Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
26 Iesus sayde vnto hir: I that speake vnto the am he.
Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
27 And eve at that poynte came his disciples and marvelled that he talked with the woman. Yet no man sayde vnto him: what meanest thou or why talkest thou with her?
Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
28 The woma then lefte her waterpot and went her waye into the cite and sayde to the men.
Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
29 Come se a man which tolde me all thinges yt ever I dyd. Is not he Christ?
“Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
30 Then they went ont of the cite and came vnto him.
Wakatoka mjini wakaja kwake.
31 And in ye meane while his disciples prayed him sayinge: Master eate.
Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
32 He sayde vnto the: I have meate to eate that ye knowe not of.
lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Then sayd ye disciples bitwene them selves: hath eny ma brought him meate?
Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
34 Iesus sayde vnto them: my meate is to doo the will of him that sent me. And to fynnysshe his worke.
Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
35 Saye not ye: there are yet foure monethes and then cometh harvest? Beholde I saye vnto you lyfte vp youre eyes and loke on ye regios: for they are whyte all redy vnto harvest.
Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
36 And he ye repeth receaveth rewarde and gaddereth frute vnto life eternall: that bothe he that soweth and he yt repeth myght reioyse to gether. (aiōnios g166)
Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 And herin is the sayinge true yt one soweth and another repeth.
Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
38 I sent you to repe yt whero ye bestowed no laboure. Other men laboured and ye are entred into their labours.
Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
39 Many of the Samaritas of that cyte beleved on him for ye sayinge of the woma which testified: he tolde me all thinges yt ever I dyd.
Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
40 Then when the Samaritas were come vnto him they besought him yt he wolde tary wt the. And he aboode there two dayes.
Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
41 And many moo beleved because of his awne wordes
Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
42 and sayd vnto the woman: Now we beleve not because of thy sayinge. For we have herde him oure selves and knowe that this is even in dede Christ the savioure of the worlde.
Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
43 After two dayes he departed thence and wet awaye into Galile.
Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
44 And Iesus him selfe testified that a Prophete hath none honoure in his awne countre.
Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
45 Then assone as he was come into Galile the Galileans receaved him which had sene all the thinges yt he dyd at Ierusalem at ye feast. For they wet also vnto ye feast daye.
Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
46 And Iesus came agayne into Cana of Galile wher he turned water into wyne. And ther was a certayne ruler whose sonne was sicke at Capernaum.
Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
47 Assone as the same herde that Iesus was come out of Iewry into Galile he wet vnto him and besought him yt he wolde descende and heale his sonne: For he was eve readie to dye.
Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
48 Then sayde Iesus vnto him: excepte ye se signes and wodres ye canot beleve.
Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
49 The ruler sayd vnto him: Syr come awaye or ever yt my chylde dye.
Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
50 Iesus sayde vnto him goo thy waye thy sonne liveth. And the ma beleved ye wordes yt Iesus had spoke vnto him and wet his waye.
Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
51 And anone as he went on his waye his servantes met him and tolde him sayinge: thy chylde liveth.
Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
52 Then enquyred he of the the houre when he begane to amende. And they sayde vnto him: Yester daye the sevethe houre the fever lefte him.
Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
53 And the father knew that it was the same houre in which Iesus sayde vnto him: Thy sonne liveth. And he beleved and all his housholde.
Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
54 Thys is agayne the seconde myracle yt Iesus dyd after he was come oute of Iewry into Galile.
Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >