< John 16 >

1 These thinges have I sayde vnto you because ye shuld not be offended.
“Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
2 They shall excomunicat you: ye ye tyme shall come that whosoever killeth you will thinke that he doth God service.
Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
3 And suche thinges will they do vnto you because they have not knowen the father nether yet me.
Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
4 But these thinges have I tolde you that when that houre is come ye myght remember them that I tolde you so. These thinges sayde I not unto you at the begynninge because I was present with you.
Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I goo my waye to him that sent me and none of you axeth me: whither goest thou?
Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
6 But because I have sayde suche thinges vnto you youre hertes are full of sorowe.
Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
7 Neverthelesse I tell you the trueth it is expedient for you that I goo awaye. For yf I goo not awaye that comforter will not come vnto you. But yf I departe I will sende him vnto you.
Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
8 And when he is come he will rebuke ye worlde of synne and of rightwesnes and of iudgement.
Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9 Of synne because they beleve not on me:
Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10 Of rightwesnes because I go to my father and ye shall se me no moare:
kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11 and of iudgement because the chefe ruler of this worlde is iudged all ready.
kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12 I have yet many thinges to saye vnto you: but ye canot beare them awaye now.
“Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
13 How be it when he is come (I meane the sprete of truthe) he will leade yon into all trueth. He shall not speake of him selfe: but whatsoever he shall heare that shall he speake and he will shewe you thinges to come.
Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
14 He shall glorify me for he shall receave of myne and shall shewe vnto you.
Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15 All thinges that ye father hath aremyne. Therfore sayd I vnto you that he shall take of myne and shewe vnto you.
Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
16 After a whyle ye shall not se me and agayne after a whyle ye shall se me: For I goo to the father.
“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!”
17 Then sayd some of his disciples bitwene them selves: what is this yt he sayth vnto vs after a whyle ye shall not se me and agayne after a whyle ye shall se me: and that I go to the father.
Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, “Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!”
18 They sayd therfore: what is this that he sayth after a whyle? we canot tell what he sayth.
Basi, wakawa wanaulizana, “Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini.”
19 Iesus perceaved yt they wolde axe him and sayd vnto them: This is it that ye enquyre of bitwene youre selves that I sayd after a whyle ye shall not se me and agayne after a whyle ye shall se me.
Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, “Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
20 Verely verely I saye vnto you: ye shall wepe and lamet and the worlde shall reioyce. Ye shall sorowe: but youre sorowe shalbe tourned to ioye.
Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman when she traveyleth hath sorowe because her houre is come: but assone as she is delivered of the chylde she remembreth no moare the anguysshe for ioye that a man is borne in to the worlde
Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
22 And ye now are in sorowe: but I will se you agayne and youre hertes shall reioyce and youre ioye shall no ma take fro you.
Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
23 And in that daye shall ye axe me no question. Verely verely I saye vnto you whatsoever ye shall axe the father in my name he will geve it you
Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
24 Hitherto have ye axed nothinge in my name. Axe and ye shall receave it: that youre ioye maye be full.
Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
25 These thinges have I spoken vnto you in proverbes. The tyme will come when I shall no moare speake to you in proverbes: but I shall shewe you playnly from my father.
“Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
26 At that daye shall ye axe in myne name. And I saye not vnto you that I will speake vnto my father for you
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
27 For ye father him selfe loveth you because ye have loved me and have beleved that I came out from God.
maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 I went out from the father and came into the worlde: and I leve the worlde agayne and go to ye father.
Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba.”
29 His disciples sayd vnto him: loo now speakest thou playnly and thou vsest no proverbe.
Basi, wanafunzi wake wakamwambia, “Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
30 Nowe knowe we that thou vnderstondest all thinges and nedest not yt eny man shuld axe the eny question. Therfore beleve we that thou camst fro god.
Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu.”
31 Iesus answered them: Now ye do beleve.
Yesu akawajibu, “Je, mnaamini sasa?
32 Beholde ye houre draweth nye and is already come yt ye shalbe scatered every man his wayes and shall leave me alone. And yet am I not alone. For ye father is with me.
Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
33 These wordes have I spoke vnto you yt in me ye might have peace. For in ye worlde shall ye have tribulacio: but be of good cheare I have over come the worlde.
Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!”

< John 16 >