< John 6 >

1 After these thinges Iesus wet his waye over the see of Galile nye to a cyte called Tiberias.
Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2 And a greate multitude folowed him because they had sene his myracles which he dyd on them that were diseased.
Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3 And Iesus went vp into a mountayne and there he sate with his disciples.
Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4 And ester a feast of ye Iewes was nye.
Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5 Then Iesus lifte vp his eyes and sawe a greate copany come vnto him and sayde vnto Philip: whence shall we bye breed yt these might eate.
Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, “Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?”
6 This he sayde to prove him: for he him sylfe knewe what he wolde do.
(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7 Philip answered him two hondred peny worthe of breed are not sufficient for them yt every ma have a litell.
Filipo akamjibu, “Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!”
8 Then sayde vnto him one of his disciples Andrew Simon Peters brother.
Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9 There ys a lad here which hath fyve barly loves and two fisshes: but what is that amoge so many?
“Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?”
10 And Iesus sayde. Make the people sit doune: Ther was moche grasse in the place. And the men sate doune in nombre about five thousande.
Yesu akasema, “Waketisheni watu.” Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11 And Iesus toke the breed and gave thankes and gave to the disciples and his disciples to them that were set doune. And lykwyse of the fysshes as moche as they wolde.
Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12 When they had eate ynough he sayd vnto his disciples: gadder vp the broke meate that remayneth: that nothinge be loost.
Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee.”
13 And they gadered it to geder and fylled twelve baskettes with the broken meate of the five barly loves which broken meate remayned vnto the that had eaten.
Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14 Then the men when they had sene the myracle that Iesus dyd sayde: This is of a trueth the Prophet that shuld come into the worlde.
Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, “Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni.”
15 When Iesus perceaved that they wolde come and take him vp to make him kinge he departed agayne into a mountayne him silfe a lone.
Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16 And when eve was come his disciples wet vnto the see
Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17 and entred into a shyppe and went over the see vnto Capernaum. And anone it was darcke and Iesus was not come to them.
wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18 And ye see arose with a greate winde yt blew.
Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19 And when they had rowe aboute a. xxv. or a xxx. furlonges they sawe Iesus walke on ye see and drawe nye vnto the shyp and they were afrayed.
Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20 And he sayde vnto them: It is I be not a frayde.
Yesu akawaambia, “Ni mimi, msiogope!”
21 Then wolde they have receaved him into the shyp and the ship was by and by at the londe whyther they went.
Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22 The daye folowynge the people which stode on the other syde of the see sawe that ther was none other shyp theare save yt one wher in his disciples were entred and that Iesus went not in with his disciples into the ship: but that his disciples were gone awaye alone.
Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23 How be it ther came other shippes from Tiberias nye vnto the place where they ate breed when the Lorde had blessed.
Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24 Then whe the people sawe that Iesus was not there nether his disciples they also toke shippinge and came to Caparnaum sekinge for Iesus.
Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25 And when they had founde him on ye other syde of ye see they sayd vnto him: Rabbi whe camest thou hidder?
Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, “Mwalimu, ulifika lini hapa?”
26 Iesus answered them and sayde: verely verely I saye vnto you: ye seke me not because ye sawe the myracles: but because ye ate of the loves and were filled.
Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27 Laboure not for ye meate which perissheth but for ye meate that endureth vnto everlastynge lyfe whiche meate ye sonne of ma shall geve vnto you. For him hath god ye father sealed. (aiōnios g166)
Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho.” (aiōnios g166)
28 Then sayd they vnto him: what shall we do that we myght worke ye workes of God?
Wao wakamwuliza, “Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?”
29 Iesus answered and sayde vnto them. This is ye worke of God that ye beleve on him who he hath sent.
Yesu akawajibu, “Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma.”
30 They sayde vnto him: what signe shewest thou then that we maye se and beleve the? What doest thou worke?
Hapo wakamwambia, “Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31 Oure fathers dyd eate Manna in the desert as yt is writte: He gave them breed fro heaven to eate.
Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni.”
32 Iesus sayde vnto the: verely verely I saye vnto you: Moses gave you breed fro heave: but my father geveth you the true breed fro heave.
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33 For the breed of God is he which cometh doune from heave and geveth lyfe vnto the worlde.
Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima.”
34 Then sayde they vnto him: Lorde ever moore geve vs this breed.
Basi, wakamwambia, “Mheshimiwa, tupe daima mkate huo.”
35 And Iesus sayde vnto them: I am that breed of life. He that cometh to me shall not honger: and he that beleveth on me shall never thurst.
Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36 But I sayed vnto you: that ye have sene me aud yet beleve not.
Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37 All that the father geveth me shall come to me: and him yt cometh to me I cast not awaye.
Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38 For I came doune fro heaven: not to do myne awne will but his will which hath sent me.
kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39 And this is the fathers will which hath sent me that of all which he hath geven me I shuld loose no thinge: but shuld rayse it vp agayne at the last daye.
Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40 And this is the wyll of him yt sent me: yt every man which seith ye sonne and beleveth on him have everlastinge lyfe. And I will rayse him vp at ye last daye. (aiōnios g166)
Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho.” (aiōnios g166)
41 The Iewes then murmured at him because he sayde: I am that breed which is come doune from heaven.
Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: “Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
42 And they sayde: Is not this Iesus ye sonne of Ioseph whose father and mother we knowe? How ys yt then that he sayeth I came doune from heave?
Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?”
43 Iesus answered and sayde vnto them. Murmur not betwene youre selves.
Yesu akawaambia, “Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44 No man can come to me except the father which hath sent me drawe him. And I will rayse him vp at the last daye.
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45 It is written in the Prophetes yt they shall all be taught of God. Every man therfore that hath hearde and hath learned of the father commeth vnto me.
Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46 Not that eny man hath sene ye father save he which is of God: the same hath sene the father.
Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47 Verely verely I saye vnto you he that beleveth on me hath everlastinge lyfe. (aiōnios g166)
Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios g166)
48 I am that breed of lyfe.
Mimi ni mkate wa uzima.
49 Youre fathers dyd eate Mana in ye wildernes and are deed.
Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50 This is that breed which cometh fro heave yt he which eateth of it shuld also not dye.
Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51 I am that lyvinge breed which came doune from heave. Yf eny man eate of this breed he shall live forever. And the breed that I will geve is my flesshe which I will geve for the lyfe of ye worlde (aiōn g165)
Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn g165)
52 And the Iewes strove amoge them selves sayinge: How can this felowe geve vs his flesshe to eate?
Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53 Then Iesus sayde vnto them: Verely verely I saye vnto you except ye eate ye flesshe of ye sonne of man and drinke his bloude ye shall not have lyfe in you
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54 Whosoever eateth my flesshe and drinketh my bloude hath eternall lyfe: and I will rayse him vp at the last daye. (aiōnios g166)
Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios g166)
55 For my flesshe is meate in dede: and my bloude is drynke in dede.
Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 He that eateth my flesshe and drynketh my bloude dwelleth in me and I in him.
Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57 As the lyvinge father hath sent me even so lyve I by my father: and he that eateth me shall live by me.
Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58 This is the breed which cam from heave: not as youre fathers have eaten Manna and are deed. He that eateth of this breed shall live ever. (aiōn g165)
Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn g165)
59 These thinges sayd he in the synagoge as he taught in Capernaum.
Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60 Many of his disciples when they had herde this sayde: this is an herde sayinge: who can abyde the hearinge of it?
Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, “Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?”
61 Iesus knew in him selfe that his disciples murmured at it and sayde vnto them: Doth this offende you?
Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, “Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62 What and yf ye shall se the sonne of man ascede vp where he was before?
Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63 It is the sprete that quyckeneth the flesshe proffeteth nothinge. The wordes that I speake vnto you are sprete and lyfe.
Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64 But ther are some of you that beleve not. For Iesus knewe from the begynnynge which they were that beleved not and who shuld betraye him.
Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini.” (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65 And he sayde: Therfore sayde I vnto you: that no man can come vnto me except it were geven vnto him of my father.
Kisha akasema, “Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu.”
66 From that tyme many of his disciples wet backe and walked no moore with him.
Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67 Then sayde Iesus to the twelve: will ye alsoo goo awaye?
Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, “Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?”
68 Then Simon Peter answered: Master to whom shall we goo? Thou haste the wordes of eternall lyfe (aiōnios g166)
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele. (aiōnios g166)
69 and we beleve and knowe yt thou arte Christ the sonne of the lyvinge God.
Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu.”
70 Iesus answered them: Have not I chosen you twelve and yet one of you is the devyll?
Yesu akawaambia, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!”
71 He spake it of Iudas Iscariot the sonne of Simon. For he it was yt shuld betraye him and was one of the twelve.
Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.

< John 6 >