< Hebrews 11 >

1 Fayth is a sure confidence of thynges which are hoped for and a certayntie of thynges which are not sene.
Sasa imani ni hakika aliyo nayo mtu wakati atarajiapo kitu fulani kwa ujasiri. Ni hakika ya kitu ambacho bado hakijaonekana.
2 By it ye elders were well reported of.
Kwa sababu hii mababu zetu walithibitika kwa imani yao.
3 Thorow fayth we vnderstonde that the worlde was ordeyned by the worde of god: and that thynges which are sene were made of thynges which are not sene. (aiōn g165)
Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu, ili kwamba kile kinachoonekana hakikutengenezwa kutokana na vitu ambavyo vilikuwa vinaonekana. (aiōn g165)
4 By fayth Abell offered vnto god a more plenteous sacrifice then Cayn: by which he obteyned witnes that he was righteous god testifyinge of his gyftes: by which also he beynge deed yet speaketh.
Ilikuwa kwa sababu ya imani kwamba Habili alimtolea Mungu sadaka ya kufaa kuliko alivyofanya Kaini. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba alisifiwa kuwa mwenye haki. Mungu alimsifu kwa sababu ya zawadi alizoleta. Kwa sababu hiyo, Habili bado ananena, ingawa amekufa.
5 By fayth was Enoch traslated yt he shuld not se deeth: nether was he founde: for God had taken him awaye. Before he was taken awaye he was reported of that he had pleased God:
Ilikuwa kwa imani kwamba Enoko alichukuliwa juu na hakuona mauti. “Hakuonekana, kwa sababu Mungu alimchukua” kwa vile ilinenwa juu yake kuwa alimpendeza Mungu kabla ya kuchukuliwa juu.
6 but with out fayth it is vnpossible to please him. For he that commeth to God must beleve that God is and that he is a rewarder of them that seke him.
Pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa kuwa ajaye kwa Mungu lazima aamini kwamba Mungu anaishi na kwamba huwapatia zawadi wale wamtafutao.
7 By fayth Noe honored God after that he was warned of thinges which were not sene and prepared the arcke to the savinge of his houssholde thorowe the which arcke he condempned the worlde and became heyre of the rightewesnes which commeth by fayth.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Nuhu, akiwa ameonywa na Mungu kuhusiana na mambo ambayo hayakuwa yameonekana, kwa heshima ya ki Mungu alitengeneza safina kwa ajili ya kuiokoa familia yake. Kwa kufanya hivi, aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ambayo huja kupitia imani.
8 By fayth Abraha whe he was called obeyed to goo out into a place which he shuld afterwarde receave to inheritaunce and he wet out not knowynge whether he shuld goo.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, alipoitwa alitii na kwenda mahali ambapo alipaswa kupokea kama urithi. Alitoka bila kujua mahali gani alikuwa anakwenda.
9 By fayth he removed into the londe yt was promysed him as into a straunge countre and dwelt in tabernacles: and so dyd Isaac and Iacob heyres with him of the same promes.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishi katika nchi ya ahadi kama mgeni. Aliishi katika mahema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi wenzake wa ahadi ile ile.
10 For he loked for a citie havinge a foundacio whose bylder and maker is God.
Hii ni kwa sababu alitarajia kuupata mji ambao mwenye kuubuni na mjenzi wake angelikuwa ni Mungu.
11 Thorow fayth Sara also receaved stregth to be with chylde and was delivered of a chylde when she was past age because she iudged him faythfull which had promysed.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu, na Sara mwenyewe, walipokea nguvu ya kutunga mimba ingawa walikuwa wazee sana, kwa kuwa walimuona Mungu kuwa mwaminifu, ambaye aliwaahidia mtoto wa kiume.
12 And therfore spronge therof one (and of one which was as good as deed) so many in multitude as the starres of ye skye and as the sond of the see shore which is innumerable.
Kwa hiyo pia kutoka kwa mtu huyu mmoja ambaye alikuwa amekaribia kufa wakazaliwa watoto wasiohesabika. Walikuwa wengi kama nyota za angani na wengi kama mbegu za mchanga katika ufukwe wa bahari.
13 And they all dyed in fayth and receaved not the promyses: but sawe them a farre of and beleved them and saluted them: and confessed that they were straungers and pilgrems on the erthe.
Hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea ahadi. Isipokuwa, wakiwa wameziona na kuzikaribisha kwa mbali, walikiri kwamba walikuwa wageni na wapitaji juu ya nchi.
14 They that saye soche thinges declare that they seke a coutre.
Kwa wale wasemao mambo kama haya wanaweka bayana kuwa wanatafuta nchi yao wenyewe.
15 Also yf they had bene myndfull of that countre from whence they came oute they had leasure to have returned agayne.
Kwa kweli, kama wangekuwa wakiifikiria nchi ambayo kwayo walitoka, wangelikuwa na nafasi ya kurejea.
16 But now they desyre a better that is to saye a hevenlye. Wherfore God is not ashamed of them even to be called their God: for he hath prepared for them a citie.
Lakini kama ilivyo, wanatamani nchi iliyo bora, ambayo, ni ya kimbingu. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa ametayarisha mji kwa ajili yao.
17 In fayth Abraham offered vp Isaac whe he was tempted and he offered him beinge his only begotten sonne which had receaved the promyses
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Ibrahimu baada ya kujaribiwa, alimtoa Isaka. Ndiyo, yeye ambaye alipokea kwa furaha ahadi, alimtoa mwanawe wa pekee,
18 of who it was sayde in Isaac shall thy seed be called:
ambaye juu yake ilinenwa, “Kutoka kwa Isaka uzao wako utaitwa.”
19 for he cosidered that God was able to rayse vp agayne fro deeth. Wherfore receaved he him for an ensample.
IbrahImU alijua kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kumfufua Isaka kutoka katika wafu, na kwa kuzungumza kwa lugha ya maumbo, alimpokea.
20 In fayth Isaac blessed Iacob and Esau concerninge thinges to come.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Isaka alimbariki Yakobo na Esau kuhusu mambo yajayo.
21 By fayth Iacob when he was a dyinge blessed both the sonnes of Ioseph and bowed him selfe towarde the toppe of his cepter.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yakobo alipokuwa katika hali ya kufa, alimbariki kila mmoja wa watoto wa Yusufu. Yakobo akaabudu, akiegemea juu ya fimbo yake.
22 By fayth Ioseph when he dyed remebred the departinge of the chyldren of Israel and gave commaundement of his bones.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Yusufu wakati wake wa mwisho ulipokaribia, alinena juu ya kutoka kwa wana wa Israel Misri na akawaagiza kuchukua pamoja nao mifupa yake.
23 By fayth Moses when he was borne was hid thre monethes of his father and mother be cause they sawe he was a proper chylde: nether feared they the kynges commaundemet.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipozaliwa, alifichwa kwa miezi mitatu na wazazi wake kwa sababu walimuona kuwa ni mtoto mchanga aliyekuwa mzuri, na hawakutishwa na amri ya mfalme.
24 By fayth Moses when he was great refused to be called ye sonne of Pharaos doughter
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa, alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mtoto wa binti Farao.
25 and chose rather to suffre adversitie wt the people of God then to enioye the pleasurs of synne for a ceason
Badala yake, alichagua kushiriki mateso pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia anasa za dhambi kwa kitambo.
26 and estemed the rebuke of Christ greater ryches then the treasure of Egypt. For he had a respect vnto ye rewarde.
Alifikiri aibu ya kumfuata Kristo kuwa ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri kwa kuwa alikaza macho yake katika zawadi ya wakati wake ujao.
27 By fayth he forsoke Egypt and feared not the fearcenes of the kynge. For he endured even as he had sene him which is invisible.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Musa alitoka Misri. Hakuhofia hasira ya Mfalme, kwa kuwa alivumilia kwa kutazama kwa asiyeonekana.
28 Thorow fayth he ordeyned the ester lambe and the effusion of bloud lest he that destroyed the fyrst borne shuld touche them.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba aliishika pasaka na kunyunyiza damu, ili kwamba mharibu wa mzaliwa wa kwanza asiweze kuwagusa wazaliwa wa kwanza wa kiume wa waisrael.
29 By fayth they passed thorow the reed see as by drye londe which when the Egypcians had assayed to do they were drouned.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba walipita katika bahari ya shamu kama katika nchi kavu. Wakati wamisri walipojaribu kupita, walimezwa.
30 By fayth the walles of Ierico fell doune after they were copased about seven dayes.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba ukuta wa Yeriko ulianguka chini, baada ya kuuzunguka kwa siku saba.
31 By fayth ye harlot Raab perisshed not with the vnbelevers whe she had receaved the spyes to lodgynge peaseably.
Ilikuwa ni kwa imani kwamba Rahabu yule kahaba hakuangamia pamoja na wale ambao hawakuwa watiifu, kwa sababu alikuwa amewapokea wapelelezi na kuwahifadhi salama.
32 And what shall I more saye ye tyme wold be to short for me to tell of Gedeo of Barach and of Samson and of Iephthae: also of David and Samuel and of the Prophetes:
Na niseme nini zaidi? Maana muda hautoshi kusimulia ya Gideoni, Barak, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samwel na za manabii,
33 which thorowe fayth subdued kyngdomes wrought righteousnes obteyned the promyses stopped the mouthes of lyons
ambao kupitia imani walizishinda falme, walitenda haki, na wakapokea ahadi. Walizuia vinywa vya simba,
34 queched the violence of fyre escaped the edge of the swearde of weake were made stroge waxed valient in fight turned to flyght the armyes of the alientes.
walizima nguvu za moto, walikwepa ncha ya upanga, waliponywa kutoka katika magonjwa, walikuwa mashujaa vitani, na walisababisha majeshi wageni kukimbia.
35 And the wemen receaved their deed raysed to lyfe agayne. Other were racked and wolde not be delyvered that they myght receave a better resurreccion.
Wanawake walipokea wafu wao kwa njia ya ufufuo. Wengine waliteswa, bila kukubali kuachwa huru ili kwamba waweze kupata uzoefu wa ufufuo ulio bora zaidi.
36 Other tasted of mockynges and scourginginges morover of bondes and presonmet:
Wengine waliteswa kwa dhihaka na kwa vichapo, naam, hata kwa vifungo na kwa kutiwa gerezani.
37 were stoned were hewen a sunder were tepted were slayne with sweardes walked vppe and doune in shepes skynnes in gotes skynnes in nede tribulacio and vexacio
Walipondwa mawe. Walikatwa vipande kwa misumeno. Waliuawa kwa upanga. Walikwenda kwa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi walikuwa wahitaji, wakiendelea katika maumivu na wakitendewa mabaya
38 which ye worlde was not worthy of: they wadred in wildernes in moutaynes in dennes and caves of the erth.
(ambayo ulimwengu haukustahili kuwa nao), wakitangatanga nyikani, milimani, katika mapango na katika mashimo ya ardhini.
39 And these all thorow fayth obtayned good reporte and receaved not the promes
Ingawa watu wote hawa walikubaliwa na Mungu kwa sababu ya imani yao, hawakupokea alichoahidi.
40 God provydinge a better thinge for vs that they with out vs shuld not be made parfecte.
Mungu alitangulia kutupatia kitu kilichobora, ili kwamba bila sisi wasingeweza kukamilishwa.

< Hebrews 11 >