< Hebrews 12 >

1 Wherfore let vs also (seynge that we are copased with so great a multitude of witnesses) laye awaye all that presseth doune and the synne that hageth on and let vs rune with paciece vnto the battayle yt is set before vs
Kwahiyo, kwa kuwa tumezungukwa na wingu kubwa la mashaidi, na tutupe kila kitu kinacho tulemea pamoja na dhambi ambayo inatuzingira kwa urahisi. Tupige mbio kwa saburi katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
2 lokynge vnto Iesus the auctor and fynnyssher of oure fayth which for the ioye that was set before him abode the crosse and despysed the shame and is set doune on the right honde of ye trone of God.
Tuyaelekeze macho yetu kwa Yesu, aliye mwanzilishi na mwenye kutimiliza imani yetu, ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake alistahmili msalaba, akiidharau aibu yake, na akakaa chini mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Consider therfore how that he endured suche speakinge agaynst him of synners lest ye shuld be weried and faynte in youre myndes.
Maana mtafakarini yeye aliye stahimili maneno ya chuki kutoka kwa wenye dhambi, dhidi yake mwenyewe ili kwamba msije mkachoka au kuzimia mioyo yenu.
4 For ye have not yet resisted vnto bloud sheddinge stryvinge agaynst synne.
Hamjataabika au kuteseka mkishindana na dhambi kiasi cha kuishiwa damu.
5 And ye have forgotten the consolacion which speaketh vnto you as vnto chyldren: My sonne despyse not the chastenynge of the Lorde nether faynt when thou arte rebuked of him:
Tena mmesahau kule kutiwa moyo ambako kunawaelekeza kama watoto wa kiume: “Mwanangu, usiyachukuwe kwa wepesi marudia ya Bwana, wala usikate tamaa unapo rekebishwa na yeye.”
6 For whom the Lorde loveth him he chasteneth: yee and he scourgeth every sonne that he receaveth.
Kwa kuwa Bwana humrudi yeyote ambaye anampenda, na humwadhibu kila mwana ambaye humpokea.
7 Yf ye endure chastninge God offereth him selfe vnto you as vnto sonnes. What sonne is that whom the father chasteneth not?
Stahimili majaribu kama kurudiwa. Mungu hushughulika nanyi kama anavyoshughulika na watoto, maana ni mtoto yupi ambaye baba yake hawezi kumrudi?
8 If ye be not vnder correccio (where of all are part takers) then are ye bastardes and not sonnes.
Lakini kama hakuna kurudiwa, ambako sisi sote tunashiriki, basi ninyi ni haramu na si watoto wake.
9 Moreover seynge we had fathers of oure flesshe which corrected vs and we gave them reverence: shuld we not moche rather be in subieccion vnto the father of spretuall gyftes that we myght live?
Zaidi ya yote, tulikuwa na baba zetu kidunia wa kuturudi, na tuliwaheshimu. Je haitupasi hata zaidi kumtii Baba wa kiroho na kuishi?
10 And they verely for a feaue dayes nurtred vs after their awne pleasure: but he learneth vs vnto that which is proffitable that we myght receave of his holines.
Kwa hakika baba zetu walituadhibu kwa miaka michache kama ilivyoonekana sawa kwao, lakini Mungu hutuadhibu kwa faida yetu ili tushiriki utakatifu wake.
11 No manner chastisynge for the present tyme semeth to be ioyeous but greveous: neverthelesse afterwarde it bryngeth the quyet frute of rightewesnes vnto them which are therin exercysed.
Hakuna adhabu inayofurahisha kwa wakati huo. Huwa na maumivu. Hata hivyo, baadaye huzaa tunda la amani ya utauwa kwa wale waliofundishwa nayo.
12 Stretch forthe therfore agayne the hondes which were let doune and the weake knees
Kwa hiyo inueni mikono yenu iliyolegea na kufanya magoti yenu yaliyo dhaifu kuwa yenye nguvu tena;
13 and se that ye have strayght steppes vnto youre fete lest eny haltinge turne out of ye waye: yee let it rather be healed.
nyosheni mapito ya nyayo zenu, ili kwamba yeyote aliye mlemavu hataongozwa upotevuni lakini apate kuponywa.
14 Embrace peace with all men and holynes: with out the which no man shall se the Lorde.
Tafuteni amani na watu wote, na pia utakatifu ambao bila huo hakuna atakayemwona Bwana.
15 And looke to that no man be destitue of the grace of God and that no rote of bitternes springe vp and trouble and therby many be defiled:
Muwe waangalifu ili kwamba asiwepo atakayetengwa mbali na neema ya Mungu, na kwamba lisije shina la uchungu litakalochipuka na kusababisha shida na kukengeusha wengi.
16 and that there be no fornicator or vnclene person as Esau which for one breakfast solde his birthright.
Angalieni kuwa hakuna zinaa au mtu asiye mtauwa kama vile Esau, ambaye kwa sababu ya mlo mmoja aliuza haki yake ya kuzaliwa.
17 Ye knowe how that afterwarde when he wolde have inherited the blessinge he was put by and he foude no meanes to come therby agayne: no though he desyred it with teares.
Kwa kuwa mnajua kwamba baadaye, alipotamani kurithi baraka, alikataliwa, kwa sababu hakupata fursa ya kutubu pamoja na baba yake, hata ingawa alitafuta sana kwa machozi.
18 For ye are not come vnto the mounte that can be touched and vnto burninge fyre nor yet to myst and darcknes and tempest of wedder
Kwa kuwa hamkuja katika mlima ambao unaweza kuguswa, Mlima unaowaka moto, giza, kukatisha tamaa na dhoruba.
19 nether vnto the sounde of a trope and the voyce of wordes: which voyce they that hearde it wisshed awaye that the comunicacion shuld not be spoken to them.
Hamkuja kwa sauti za tarumbeta, au kwa maneno yatokanayo na sauti ambayo ilisababisha kila wasikiao wasiombe neno lolote kusemwa kwao.
20 For they were not able to abyde that which was spoken. If a beast had touched the mountayne it must have bene stoned or thrust thorowe with a darte:
Kwa kuwa hawakuweza kuvumilia kile kilichoamuliwa: “Ikiwa hata mnyama agusaye mlima, lazima apigwe kwa mawe.”
21 eve so terreble was ye sight which appered. Moses sayde I feare and quake.
Ya kutisha zaidi aliyoyaona Musa alisema, “Nimeogopa sana kiasi cha kutetemeka”.
22 But ye are come vnto the moute Sion and to the citie of the livinge god the celestiall Ierusalem: and to an innumerable sight of angels
Badala yake, mmekuja mlima Sayuni na katika mji wa Mungu aliye hai, Yerualem ya mbinguni, na kwa malaika elfu kumi wanaosherehekea.
23 and vnto the congregacion of ye fyrst borne sonnes which are writte in heven and to God the iudge of all and to the spretes of iust and parfecte men
Mmekuja katika kusanyiko la wazaliwa wa kwanza wote waliosajiliwa mbinguni, kwa Mungu hakimu wa wote, na kwa roho za watakatifu ambao wamekamilishwa.
24 and to Iesus the mediator of the newe testament and to the spryncklynge of bloud that speaketh better then the bloud of Abell.
Mmekuja kwa Yesu mpatanishi wa agano jipya, na kwa damu iliyonyunyizwa ambayo hunena mema zaidi kuliko damu ya Habili.
25 Se that ye despise not him yt speaketh. For yf they escaped not which refused him that spake on erth: moche more shall we not escape yf we turne awaye fro him yt speaketh fro heve:
Angalia kuwa usije ukamkataa mmoja ambaye anenaye. Kwa kuwa kama hawakuepuka walipomkataa mmoja aliye waonya duniani, kwa hakika hatutaepuka ikiwa tutageuka mbali kutoka kwa yule atuonyaye kutoka mbinguni.
26 whose voyce the shouke the erth and now declareth sayinge: yet once more will I shake not the erth only but also heven.
Kwa wakati huo sauti yake ilitikisa dunia. Lakini sasa ameahidi na kunena, “Bado mara nyingine tena sitatikisa dunia pekee, bali mbingu pia.”
27 No dout yt same that he sayth yet once more signifieth the removinge a waye of those thinges which are shaken as of thinges which have ended their course: that the thynges which are not shaken maye remayne.
Maneno haya, “Mara moja tena,” inaonesha kutoweshwa kwa vitu vile vitetemeshwavyo, hivi ni, vitu vile ambavyo vimeumbwa, ili kwamba vile vitu visivyotetemeshwa vibakie.
28 Wherfore if we receave a kyngdom which is not moved we have grace wherby we maye serve god and please him with reverence and godly feare.
Kwa hiyo, tupokee ufalme ambao hautetemeshwi, tufurahi katika hali ya kumwabudu Mungu kwa kukubali pamoja na kunyenyekea katika kicho,
29 For oure god is a consumynge fyre.
kwa maana Mungu wetu ni moto ulao.

< Hebrews 12 >