< Acts 6 >

1 In those dayes as the nombre of the disciples grewe ther arose a grudge amonge the Grekes agaynst the Ebrues be cause their wyddowes were despysed in the dayly mynystracion.
Sasa katika siku hizi, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa inaongezeka, lalamiko la Wayahudi wa Kiyunani lilianza dhidi ya Waebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wanasahaulika katika mgao wa kila siku wa chakula.
2 Then the twelve called the multitude of the disciples to gether and sayde: it is not mete that we shuld leave the worde of God and serve at the tables.
Mitume kumi na wawili waliwaita kusanyiko lote la wanafunzi na kusema, “Siyo sahihi kwetu kuliacha neno la Mungu na kuhudumia mezani.
3 Wherfore brethren loke ye out amoge you seven men of honest reporte and full of the holy goost and wysdome which we maye apoynte to this nedfull busynes.
Kwa hiyo, ndugu, chagueni, wanaume saba, kutoka miongoni mwenu, watu wema, waliojaa Roho na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi huduma hii.
4 But we will geve oure selves cotinually to prayer and to the ministracion of ye worde.
Na sisi, tutaendelea daima katika kuomba na katika huduma ya neno.”
5 And the sayinge pleased the whoale multitude. And they chose Steven a man full of fayth and of the holy goost and Philip and Prochorus and Nichanor and Timon and Permenas and Nicholas a converte of Antioche.
Hotuba yao ikaupendeza mkutano wote. Hivyo, wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
6 Which they set before the Apostles and they prayed and layde their hondes on them.
Waumini waliwaleta watu hawa mbele ya mitume, walioomba na badaye wakawawekea mikono yao.
7 And the worde of God encreased and the noubre of the disciples multiplied in Ierusalem greatly and a great company of the prestes were obedient to the faythe.
Hivyo, neno la Mungu lilienea; na idadi ya wanafunzi ilizidi kuongezeka huko Yesrusalem; na idadi kubwa ya makuhani wakaitii imani.
8 And Steven full of faythe and power dyd great wondres and myracles amoge ye people.
Na Stefano, aliyejaa neema na nguvu, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa miongoni mwa watu.
9 Then ther arose certayne of the synagoge which are called Lybertines and Syrenites and of Alexandria and of Cilicia and Asia and disputed with Steven.
Lakini hapo wakainuka baadhi ya watu wafuasi wa Sinagogi liitwalo Sinagogi la Mahuru, na la Wakirene na la Waeskanderia, na baadhi kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa walikuwa wakihojiana na Stefano.
10 And they coulde not resist the wysdome and the sprete with which he spake.
Lakini, hawakuweza kushindana na hekima na Roho ambayo Stefano alikuwa akitumia katika kuzungumza.
11 Then sent they in men which sayd: we have hearde him speake blasphemous wordes agaynst Moses and agaynst God.
Kisha waliwashawishi baadhi ya watu kwa siri kusema, “Tumesikia Stefano akizungumza maneno ya kufuru dhidi ya Musa na dhidi ya Mungu.”
12 And they moved ye people and the elders and the scribes: and came apon him and caught him and brought him to the counsell
Waliwashurutisha watu, wazee, na waandishi, na kumwendea Stefano, wakamkamata, na kumleta mbele ya baraza.
13 and brought forth falce witnesses which sayde. This ma ceasith not to speake blasphemous wordes agaynst this holy place and the lawe:
waliwaleta mashahidi wa uongo, waliosema, “mtu huyu haachi kunena maneno mabaya dhidi ya eneo hili takatifu na sheria.
14 for we hearde him saye: this Iesus of Nazareth shall destroye this place and shall chaunge the ordinaunces which Moses gave vs.
Kwani tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali hapa na kuzibadili desturi tulizokabidhiwa na Musa.”
15 And all that sate in ye counsell loked stedfastly on him and sawe his face as it had bene the face of an angell.
Kila mmoja aliyekuwa katika baraza, akaelekeza macho yake kumwangalia Stefano, nao wakauona uso wake ulikuwa kama uso wa malaika.

< Acts 6 >