< 1 Corinthians 4 >

1 Let men this wyse esteme vs eve as the ministers of Christ and disposers of ye secretes of God.
Hivi ndivyo mtu atuhesabu sisi, kama watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za kweli za Mungu.
2 Furthermore it is requyred of the disposers that they be founde faithfull.
Katika hili, kinachotakiwa kwa uwakili ni kwamba wawe wa kutumainiwa.
3 With me is it but a very smal thinge that I shuld be iudged of you ether of (mans daye) No I iudge not myn awne selfe.
Lakini kwangu mimi ni kitu kidogo sana kuwa ninahukumiwa na ninyi au hukumu ya kibinadamu. Kwa kuwa sijihukumu hata mimi mwenyewe.
4 I know nought by my selfe: yet am I not therby iustified. It is the Lorde that iudgeth me.
Sijihukumu mimi mwenyewe, hii haina maana kuwa mimi ni mwenye haki. Ni Bwana anihukumuye.
5 Therfore iudge no thinge before the tyme vntill the Lorde come which will lighten thinges that are hyd in darcknes and ope the counsels of the hertes. And then shall every man have prayse of God.
Kwa hiyo, msitamke hukumu juu ya lolote kabla ya wakati, kabla ya kuja kwa Bwana. Atayaleta nuruni mambo yaliyofichika gizani na kufunua makusudi ya mioyo. Ndipo kila mmoja atapokea sifa yake kutoka kwa Mungu.
6 These thinges brethre I have described in myn awne person and Apollos for youre sakes that ye myght learne by vs that no man coute of him selfe beyonde that which is above written: that one swell not agaynst another for eny mans cause.
Sasa, kaka na dada zangu, mimi mwenyewe na Apolo nimetumia kanuni hizi kwa ajili yenu. Ili kwamba kutoka kwetu mnaweza kujifunza maana ya usemi, “Usiende zaidi ya kilivyoandikwa.” Hii ni kwamba hakuna mmoja wenu ajivunaye juu ya mwingine.
7 For who preferreth the? What hast thou that thou hast not receaved? Yf thou have receaved it why reioysest thou as though thou haddest not receaved it?
Maana ni nani aonaye tofauti kati yenu na mwingine? Ni nini ulicho nacho hukukipokea bure? Kama umekwisha kupokea bure, kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo?
8 Now ye are full: now ye are made rych: ye raygne as kinges with out vs: and I wold to god ye dyd raygne that we might raygne with you.
Tayari mnavyo vyote ambavyo mngetaka! Tayari mmekuwa na utajiri! Mmeanza kutawala-na kwamba mnamiliki zaidi yetu sisi! Kweli, nawatakia umililki mwema ili kwamba tumiliki pamoja nanyi.
9 Me thinketh that God hath set forth vs which are Apostles for the lowest of all as it were me appoynted to deeth. For we are a gasyngestocke vnto the worlde and to ye angels and to men.
Kwa hiyo ninadhani Mungu ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha wa mwisho katika mustari wa maandamano na kama watu waliohukumiwa kuuawa. Tumekuwa kama tamasha kwa ulimwengu, kwa malaika na kwa wanadamu.
10 We are foles for Christes sake and ye are wyse thorow Christ. We are weake and ye are stroge. Ye are honorable and we are despised.
Sisi ni wajinga kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika Kristo. Tu wanyonge, lakini ninyi mna nguvu. Mnaheshimiwa, lakina sisi tunadharauliwa.
11 Eve vnto this daye we honger and thyrst and are naked and are boffetted wt fistes and have no certayne dwellinge place
Hata saa hii tuna njaa na kiu, hatuna nguo, tuna mapigo, na tena hatuna makazi.
12 and laboure workinge with oure awne hondes. We are revysed and yet we blesse. We are persecuted and suffer it.
Tunafanya kazi kwa bidii, kwa mikono yetu wenyewe. Tunapodharauliwa, twabariki. Wakati tunapoteswa, twavumilia.
13 We are evyll spoken of and we praye. We are made as it were the filthynes of the worlde the ofscowringe of all thinges even vnto this tyme.
Tunapotukanwa, twarudisha kwa upole. Tumekuwa, na tu bado tunahesabiwa kuwa kama kukataliwa na dunia na takataka kwa mambo yote.
14 I write not these thinges to shame you: but as my beloved sonnes I warne you.
Siandiki mambo haya kuwaaibisha ninyi, lakini kuwarudi ninyi kama watoto wangu niwapendao.
15 For though ye have ten thousande instructours in Christ: yet have ye not many fathers. In Christ Iesu I have begotten you thorowe ye gospell.
Hata kama mna waalimu makumi elfu katika Kristo, hamna baba wengi. Kwa kuwa nimekuwa baba yenu katika Yesu Kristo kupitia injili.
16 Wherfore I desyre you to folowe me.
Hivyo ninawasihi mniige mimi.
17 For this cause have I sent vnto you Timotheus which is my deare sonne and faithfull in the Lorde which shall put you in remembrauce of my wayes which I have in Christ eve as I teache every where in all congregacios.
Hiyo ndiyo sababu nilimtuma kwenu Timotheo, mpendwa wangu na mtoto mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia zangu katika Kristo, kama ninavyofundisha kila mahali na kila kanisa.
18 Some swell as though I wolde come no more at you.
Sasa baadhi yenu wanajisifu, wakitenda kana kwamba sitakuja kwenu.
19 But I will come to you shortely yf God will: and will knowe not ye wordes of the which swell but ye power:
Lakini nitakuja kwenu kitambo, kama Bwana akipenda. Ndipo nitajua si maneno yao tu wanaojisifu, lakini nitaona nguvu zao.
20 for ye kyngdome of God is not in wordes but in power.
Kwa kuwa ufalme wa Mungu hauwi katika maneno bali katika nguvu.
21 What will ye? Shall I come vnto you with a rodde or els in love and in the sprete of mekenes?
Mnataka nini? Nije kwenu na fimbo au kwa upendo na katika roho ya upole?

< 1 Corinthians 4 >