< Psalms 4 >

1 To the Chief Musician: with stringed instruments. A Melody of David. When I cry, answer me, O mine own righteous God, In a strait place, thou hast made room for me, Show me favour, and hear my prayer.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 Ye sons of the great! how long, turning my glory to contempt, will ye love emptiness, will ye seek falsehood? (Selah)
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Know ye, then, that Yahweh hath set apart the man of lovingkindness for himself: Yahweh, will hear, when I cry to him.
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Be deeply moved, but do not sin, —Ponder in your own heart upon your bed, and be silent. (Selah)
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 Sacrifice the sacrifices of righteousness; and put your trust in Yahweh.
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 Multitudes, are saying, Who will show us prosperity? Lift thou upon us the light of thy countenance, O Yahweh.
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Thou hast put gladness in my heart, —beyond the season when, their corn and their new wine, have increased.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 In peace, will I lay me down and at once sleep; for, thou, Yahweh alone, wilt cause me, in security, to dwell.
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

< Psalms 4 >