< Psalms 68 >

1 For the leader. Of David. A psalm. A song. God arises, his enemies scatter: they who hate him flee before him.
Mungu ainuke, maadui zake watawanyike; pia wale wamchukiao wakimbie mbele zake.
2 As smoke before wind is driven, as wax melts before fire, so before God vanish the wicked.
Kama moshi uondoshwavyo, hivyo uwaondoshe wao; kama nta iyeyukavo mbele ya moto, hivyo waovu waangamizwe uweponi mwa Mungu.
3 But the righteous rejoice in God’s presence, they exult with exceeding joy.
Bali wenye haki wafurahi; washangilie mbele za Mungu; washangilie na kufurahi.
4 Sing to God, make music to his name, his name is the Lord, praise him who rides on the clouds, and exult in his presence.
Mwimbieni Mungu! Lisifuni jina lake! Msifuni yule aendeshaye farasi kwenye tambarare ya bonde la Mto Yordani! Yahwe ni jina lake! Shangilieni mbele zake!
5 Father of orphans, defender of widows, is God in his holy abode.
Baba wa yatima, na mwamuzi wa wajane, ni Mungu anayeishi mahali patakatifu.
6 God brings home the lonely, he leads forth the prisoner to comfort, so that none but the rebel lives cheerless.
Mungu huwaweka wakiwa katika familia; yeye huwafungua wafungwa kwa kuimba bali waasi huishi katika ardhi kavu.
7 God, when you went in front of your people in your march through the desert, (Selah)
Mungu, wewe ulipoenda mbele ya watu wako, ulipotembea kupitia jangwani, (Selah)
8 earth shook, the heavens poured rain at the presence of God, Sinai’s God at the presence of God, Israel’s God.
nchi ilitetemeka; mbingu pia zilidondosha mvua katika uwepo wa Mungu, uweponi mwa Mungu wakati alipokuja Sinai, uweponi mwa Mungu, Mungu wa Israeli.
9 Rain in abundance, God, you did sprinkle, restoring the languishing land of your heritage.
Wewe, Mungu, ulituma mvua nyingi; uliuimarisha urithi wako wakati ulipokuwa umechoka.
10 A dwelling therein your people found: in your goodness, O God, you did care for the poor.
Watu wako waliishi humo; Wewe, Mungu, uliutoa kwa wema wako kwa maskini.
11 The Lord spoke the glad tidings of victory, a great army of women proclaim it:
Bwana alitoa amri, na wale walio zitangaza walikuwa ni jeshi kuu.
12 ‘Kings of armies they flee, they flee, and the housewife divides the spoil:
Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia, na wanawake wakisubiri nyumbani kuvigawana wao na familia zao vilivyotekwa nyara.
13 dove’s wings covered with silver and pinions with shimmer of gold,
Njiwa walio vikwa fedha wakiwa na mabawa ya njano ya dhahabu. Wakati baadhi ya watu wakikaa kati ya mifugo ya kondoo, kwa nini umefanya haya?
14 set with stones, like snow upon Zalmon.’
Mwenyezi Mungu aliwatawanya Wafalme huko, ilikuwa kama vile wakati wa theluji juu ya Mlima Salmoni.
15 A mountain of God is the mountain of Bashan, a mountain of peaks is the mountain of Bashan.
Mlima mkubwa ni milima wa mji wa Bashani; mlima mrefu ni mlima wa mji wa Bashani.
16 You high-peaked mountains, why look you askance at the mountain which God has desired for his home whereon the Lord will live forever?
Ewe mlima mrefu wa nchi, kwa nini unatazama kwa jicho la husuda, kwenye mlima ambao Mungu ameutaka kwa ajili ya mahali ambapo yeye ataishi? Hakika, Yahwe ataishi humo milele.
17 The chariots of God are twice ten thousand: the Lord came from Sinai, his holy place.
Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu juu ya maelfu; Bwana yu kati yao katika mahari patakatifu, kama katika Sinai.
18 You did mount the height with trains of your captives, and gifts that you had received from the people. The rebels shall live with the Lord God.
Wewe umepaa juu; uliwaongoza mateka; umepokea zawadi kutoka kati ya watu, hata kutoka kwa wale waliopigana dhidi yako, ili kwamba wewe, Yahwe Mungu, uweze kuishi huko.
19 Blest be the Lord who sustains us daily, the God who is also our saviour. (Selah)
Abarikiwe Bwana, atubebeaye mizigo yetu, Mungu ambaye ni wokovu wetu. (Selah)
20 Our God is a God who is saviour. The ways of escape from death are known to the Lord God.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye; Yahwe Bwana ni yule awezaye kutuokoa sisi dhidi ya kifo.
21 Yes, God will shatter the head of his foes the rough scalp of those who strut on in their sins.
Lakini Bwana atapiga vichwa vya adui zake, mpaka kwenye ngozi ya kichwa yenye nywele ya wale watembeao katika makosa dhidi yake.
22 The Lord said: ‘I will bring you home from Bashan, home from the depths of the sea,
Bwana alisema, “Nitawarudisha adui zangu kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka katika kina cha bahari
23 that your feet you may bathe in blood, and your dogs lick their share of the foe.’
ili kwamba upate kuwaangamiza adui zako, ukichovya mguu wako katika damu, na ili kwamba ndimi za mbwa wako zipate mlo wao kutoka kwa adui zenu.”
24 In the temple appear God’s triumphal processions, processions in praise of my king and my God,
Mungu, wameona maandamano yako, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kwenye mahali patakatifu.
25 with singers in front, and minstrels behind, and maidens with timbrels between them, singing,
Waimbaji walitangulia, walifuatiwa na wapiga muziki, na katikati walikuwa wanawali wakicheza ngoma.
26 ‘You of the well-spring of Israel, bless the Lord God in the dance.’
Mtukuzeni Mungu katika kusanyiko; msifuni Yahwe, ninyi ukoo wa kweli wa Israeli.
27 There, in front, is Benjamin the little, the princes of Judah beside them, the princes of Zebulon, princes of Naphtali.
Kuna Benjamini kwanza, kabila dogo, kisha viongozi wa Yuda na watu wao, viongozi wa Zabuloni na viongozi wa Naftali.
28 God, show your strength, your godlike might, as you did in the past,
Mungu wenu, Israeli, ameamuru nguvu zenu; uzifunue kwetu nguvu zako, Mungu, kama ulivyo zifunua wakati uliopita.
29 from your temple that crowns Jerusalem. Kings shall bring tribute to you.
Uzifunue nguvu zako kwetu toka katika hekalu la Yerusalemu, ambako wafalme huleta zawadi kwako.
30 Rebuke the beast of the reed, the herd of bulls, with the calves of the peoples. Trample down the lovers of lies. Scatter the nations whose joy is in war.
Pigeni kelele katika vita dhidi ya wanyama wa porini katika mianzi, dhidi ya watu, lile kundi la mafahari na ndama. Wafedhehesheni na kuwalazimisha wawaletee zawadi; watawanyeni watu wapendao kupigana vita.
31 May they come from Egypt with gifts of oil, Ethiopia haste with full hands to God.
Wakuu watatoka katika Misri; Ethiopia itafanya haraka kuufikisha mkono wake kwa Mungu.
32 Sing to God, O you kingdoms of earth, make melody to the Lord. (Selah)
Mwimbieni Mungu, enyi falme za nchi; (Selah) mwimbieni sifa Yahwe.
33 Praise him who rides on the ancient heavens. See! He utters his voice, his mighty voice.
Kwake yeye apitaye juu ya mbingu za mbingu, zilizokuwepo tangu zama za kale; tazama, yeye hupiga kelele kwa nguvu
34 Ascribe strength to the God over Israel, whose strength and majesty live in the skies.
Tangazeni kuwa Mungu ni mwenye nguvu; enzi yake iko juu ya Israeli, na nguvu zake ziko angani.
35 Awe-inspiring is God in his holy place, it is Israel’s God who gives strength and might to his people. Blessed be God.
Mungu, mahali pako patakatifu panatisha; Mungu wa Israeli, yeye huwapa watu wake nguvu na uweza. Atukuzwe Mungu.

< Psalms 68 >