< Psalms 69 >

1 For the leader. On shoshannim. Of David. Save me, O God; for the waters are threatening my life.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 I am sunk in depths of mire, where ground there is none. I am come into deep deep waters, the flood overwhelms me.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 I am weary of crying, my throat is parched, my eyes are wasted with waiting for God.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 More than the hairs of my head are those who wantonly hate me. More than my bones in number are those who are falsely my foes. That which I never robbed, how am I then to restore?
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 O God, you know my folly, my guilt is not hidden from you.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Through me let not any be shamed, who wait for you, Lord God of hosts. Through me let not those be confounded who seek you, O God of Israel.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 It’s in your cause that I have borne taunts, and my face has been covered with shame;
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 I became to my kindred a foreigner, to my mother’s sons a stranger.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 It was zeal for your house that consumed me, and the insults they hurled at you fell upon me.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 When I chastened myself with fasting, they took occasion to taunt me.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 When I put on a garment of sackcloth, they made me the theme of a taunt-song.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Those who sit in the gate make sport of me in the music of drunken songs.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 But I pray to you, Lord, for a time of favour. In your great love answer me; with your loyal help, save me
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 from sinking down in the mire. Lift me out of the deep deep waters,
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 that the rushing flood may not drown me, that the deep may not swallow me up, nor the pit close her mouth upon me.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Answer me, Lord, in your gracious kindness, turn to me in your great compassion.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Hide not your face from your servant, for I am in trouble; O answer me speedily.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Draw near to me, redeem me; because of my enemies, ransom me.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 You know how I am insulted; in your sight are all my foes.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 Insult has broken my heart, past cure are my shame and confusion. For pity I looked – there was none! And for comforters, but I found none.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Poison they gave me for food, and to slake my thirst they gave vinegar.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 May their table, outspread, be a trap to them, and their peace-offerings be a snare.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 May their eyes be darkened and blind, make them shake without ceasing.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Pour your indignation upon them, let your burning wrath overtake them.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 May their camp be a desolation, in their tents be there none to live.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 For those whom you struck, they persecute, and those whom you wounded, they pain yet more.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Charge them with sin upon sin, may they not be acquitted by you.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 From the book of life be they blotted, may their names not be written with the righteous.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Lift me, O God, by your help above my pain and misery.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Then will I praise God in song and magnify him with thanksgiving,
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 which shall please the Lord better than ox, or than bullock with horns and hoofs.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 The oppressed shall rejoice at the sight. You who seek after God, let your heart revive.
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 For the Lord listens to the poor, he does not despise his prisoners.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Let the heavens and the earth sing his praises, the seas, and all creatures that move in them.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 For God will bring help to Zion, and build up the cities of Judah, his people shall live there in possession.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 His servants’ children shall have it for heritage, and those who love him shall live therein.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Psalms 69 >