< Job 10 >

1 My soul is weary of my life; I will leave my complaint upon myself; I will speak in the bitterness of my soul.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 I will say unto God, Do not condemn me; show me wherefore you contend with me.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Is it good unto you that you should oppress, that you should despise the work of your hands, and shine upon the counsel of the wicked?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Have you eyes of flesh? or see you as man sees?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Are your days as the days of man? are your years as man's days,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 That you enquire after mine iniquity, and search after my sin?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 You know that I am not wicked; and there is none that can deliver out of your hand.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 your hands have made me and fashioned me together round about; yet you do destroy me.
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Remember, I plead to you, that you have made me as the clay; and will you bring me into dust again?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Have you not poured me out as milk, and curdled me like cheese?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 You have clothed me with skin and flesh, and have fenced me with bones and sinews.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 You have granted me life and favour, and your visitation has preserved my spirit.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 And these things have you hid in your heart: I know that this is with you.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 If I sin, then you mark me, and you will not acquit me from mine iniquity.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 If I be wicked, woe unto me; and if I be righteous, yet will I not lift up my head. I am full of confusion; therefore see you mine affliction;
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 For it increases. You hunt me as a fierce lion: and again you show yourself marvellous upon me.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 You renew your witnesses against me, and increase your indignation upon me; changes and war are against me.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 Wherefore then have you brought me forth out of the womb? Oh that I had given up the spirit, and no eye had seen me!
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 I should have been as though I had not been; I should have been carried from the womb to the grave.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Are not my days few? cease then, and let me alone, that I may take comfort a little,
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 Before I go whence I shall not return, even to the land of darkness and the shadow of death;
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 A land of darkness, as darkness itself; and of the shadow of death, without any order, and where the light is as darkness.
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >