< Job 9 >

1 Then Job answered and said,
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 I know it is so truthfully: but how should man be just with God?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 If he will contend with him, he cannot answer him one of a thousand.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 He is wise in heart, and mighty in strength: who has hardened himself against him, and has prospered?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Which removes the mountains, and they know not: which overturns them in his anger.
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 Which shakes the earth out of her place, and the pillars thereof tremble.
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 Which commands the sun, and it rises not; and seals up the stars.
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 Which alone spreads out the heavens, and treads upon the waves of the sea.
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 Which makes Arcturus, Orion, and Pleiades, and the chambers of the south.
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 Which does great things past finding out; yea, and wonders without number.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Lo, he goes by me, and I see him not: he passes on also, but I perceive him not.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Behold, he takes away, who can hinder him? who will say unto him, What do you?
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 If God will not withdraw his anger, the proud helpers do stoop under him.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 How much less shall I answer him, and choose out my words to reason with him?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 Whom, though I were righteous, yet would I not answer, but I would make supplication to my judge.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 If I had called, and he had answered me; yet would I not believe that he had hearkened unto my voice.
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 For he breaks me with a tempest, and multiplies my wounds without cause.
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 He will not suffer me to take my breath, but fills me with bitterness.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 If I speak of strength, lo, he is strong: and if of judgment, who shall set me a time to plead?
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 If I justify myself, mine own mouth shall condemn me: if I say, I am perfect, it shall also prove me perverse.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Though I were perfect, yet would I not know my soul: I would despise my life.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 This is one thing, therefore I said it, He destroys the perfect and the wicked.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 If the scourge slay suddenly, he will laugh at the trial of the innocent.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 The earth is given into the hand of the wicked: he covers the faces of the judges thereof; if not, where, and who is he?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 Now my days are swifter than a post: they flee away, they see no good.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 They are passed away as the swift ships: as the eagle that hastes to the prey.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 If I say, I will forget my complaint, I will leave off my heaviness, and comfort myself:
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 I am afraid of all my sorrows, I know that you will not hold me innocent.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 If I be wicked, why then labour I in vain?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 If I wash myself with snow water, and make my hands never so clean;
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 Yet shall you plunge me in the ditch, and mine own clothes shall detest me.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 For he is not a man, as I am, that I should answer him, and we should come together in judgment.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 Neither is there any arbitrator between us, that might lay his hand upon us both.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Let him take his rod away from me, and let not his fear terrify me:
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Then would I speak, and not fear him; but it is not so with me.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >