< Job 11 >

1 Then answered Zophar the Naamathite, and said,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Should not the multitude of words be answered? and should a man full of talk be justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should your lies make men hold their peace? and when you mock, shall no man make you ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 For you have said, My doctrine is pure, and I am clean in your eyes.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But oh that God would speak, and open his lips against you;
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 And that he would show you the secrets of wisdom, that they are double to that which is! Know therefore that God exacts of you less than your iniquity deserves.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Can you by searching find out God? can you find out the Almighty unto perfection?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 It is as high as heaven; what can you do? deeper than hell; what can you know? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 The measure thereof is longer than the earth, and broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If he cut off, and shut up, or gather together, then who can hinder him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For he knows vain men: he sees wickedness also; will he not then consider it?
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 For vain men would be wise, though man be born like a wild ass's colt.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If you prepare your heart, and stretch out your hands toward him;
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If iniquity be in your hand, put it far away, and let not wickedness dwell in your tabernacles.
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 For then shall you lift up your face without spot; yea, you shall be steadfast, and shall not fear:
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 Because you shall forget your misery, and remember it as waters that pass away:
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 And your age shall be clearer than the noonday: you shall shine forth, you shall be as the morning.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And you shall be secure, because there is hope; yea, you shall dig about you, and you shall take your rest in safety.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Also you shall lie down, and none shall make you afraid; yea, many shall make suit unto you.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked shall fail, and they shall not escape, and their hope shall be as the giving up of the spirit.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >