< Daniel 6 >

1 It pleased Darius to set over the kingdom a hundred and twenty satraps, who should be throughout the whole kingdom;
Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
2 and over them three presidents, of whom Daniel was one; that these satraps might give account unto them, and that the king should have no damage.
pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
3 Then this Daniel distinguished himself above the presidents and the satraps, because a surpassing spirit was in him; and the king thought to set him over the whole realm.
Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
4 Then the presidents and the satraps sought to find occasion against Daniel as touching the kingdom; but they could find no occasion nor fault; forasmuch as he was faithful, neither was there any error or fault found in him.
Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
5 Then said these men: 'We shall not find any occasion against this Daniel, except we find it against him in the matter of the law of his God.'
Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
6 Then these presidents and satraps came tumultuously to the king, and said thus unto him: 'King Darius, live for ever!
Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
7 All the presidents of the kingdom, the prefects and the satraps, the ministers and the governors, have consulted together that the king should establish a statute, and make a strong interdict, that whosoever shall ask a petition of any god or man for thirty days, save of thee, O king, he shall be cast into the den of lions.
Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
8 Now, O king, establish the interdict, and sign the writing, that it be not changed, according to the law of the Medes and Persians, which altereth not.'
Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
9 Wherefore king Darius signed the writing and the interdict.
Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
10 And when Daniel knew that the writing was signed, he went into his house — now his windows were open in his upper chamber toward Jerusalem — and he kneeled upon his knees three times a day, and prayed, and gave thanks before his God, as he did aforetime.
Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
11 Then these men came tumultuously, and found Daniel making petition and supplication before his God.
Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
12 Then they came near, and spoke before the king concerning the king's interdict: 'Hast thou not signed an interdict, that every man that shall make petition unto any god or man within thirty days, save of thee, O king, shall be cast into the den of lions?' The king answered and said: 'The thing is true, according to the law of the Medes and Persians, which altereth not.'
Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
13 Then answered they and said before the king: 'That Daniel, who is of the children of the captivity of Judah, regardeth not thee, O king, nor the interdict that thou hast signed, but maketh his petition three times a day.'
Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
14 Then the king, when he heard these words, was sore displeased, and set his heart on Daniel to deliver him; and he laboured till the going down of the sun to deliver him.
Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
15 Then these men came tumultuously unto the king, and said unto the king: 'Know, O king, that it is a law of the Medes and Persians, that no interdict nor statute which the king establisheth may be changed.'
Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
16 Then the king commanded, and they brought Daniel, and cast him into the den of lions. Now the king spoke and said unto Daniel: 'Thy God whom thou servest continually, He will deliver thee.'
Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
17 And a stone was brought, and laid upon the mouth of the den; and the king sealed it with his own signet, and with the signet of his lords; that nothing might be changed concerning Daniel.
Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
18 Then the king went to his palace, and passed the night fasting; neither were diversions brought before him; and his sleep fled from him.
Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
19 Then the king arose very early in the morning, and went in haste unto the den of lions.
Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
20 And when he came near unto the den to Daniel, he cried with a pained voice; the king spoke and said to Daniel: 'O Daniel, servant of the living God, is thy God, whom thou servest continually, able to deliver thee from the lions?'
Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
21 Then said Daniel unto the king: 'O king, live for ever!
Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
22 My God hath sent His angel, and hath shut the lions' mouths, and they have not hurt me; forasmuch as before Him innocency was found in me; and also before thee, O king, have I done no hurt.'
Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
23 Then was the king exceeding glad, and commanded that they should take Daniel up out of the den. So Daniel was taken up out of the den, and no manner of hurt was found upon him, because he had trusted in his God.
Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
24 And the king commanded, and they brought those men that had accused Daniel, and they cast them into the den of lions, them, their children, and their wives; and they had not come to the bottom of the den, when the lions had the mastery of them, and broke all their bones in pieces.
Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
25 Then king Darius wrote unto all the peoples, nations, and languages, that dwell in all the earth: 'Peace be multiplied unto you.
Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
26 I make a decree, that in all the dominion of my kingdom men tremble and fear before the God of Daniel; for He is the living God, and stedfast for ever, and His kingdom that which shall not be destroyed, and His dominion shall be even unto the end;
“Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
27 He delivereth and rescueth, and He worketh signs and wonders in heaven and in earth; who hath delivered Daniel from the power of the lions.'
Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
28 So this Daniel prospered in the reign of Darius, and in the reign of Cyrus the Persian.
Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.

< Daniel 6 >