< Daniel 8 >

1 In the third year of the reign of king Belshazzar a vision appeared unto me, even unto me Daniel, after that which appeared unto me at the first.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 And I saw in the vision; now it was so, that when I saw, I was in Shushan the castle, which is in the province of Elam; and I saw in the vision, and I was by the stream Ulai.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 And I lifted up mine eyes, and saw, and, behold, there stood before the stream a ram which had two horns; and the two horns were high; but one was higher than the other, and the higher came up last.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 I saw the ram pushing westward, and northward, and southward; and no beasts could stand before him, neither was there any that could deliver out of his hand; but he did according to his will, and magnified himself.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 And as I was considering, behold, a he-goat came from the west over the face of the whole earth, and touched not the ground; and the goat had a conspicuous horn between his eyes.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 And he came to the ram that had the two horns, which I saw standing before the stream, and ran at him in the fury of his power.
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 And I saw him come close unto the ram, and he was moved with choler against him, and smote the ram, and broke his two horns; and there was no power in the ram to stand before him; but he cast him down to the ground, and trampled upon him; and there was none that could deliver the ram out of his hand.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 And the he-goat magnified himself exceedingly; and when he was strong, the great horn was broken; and instead of it there came up the appearance of four horns toward the four winds of heaven.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 And out of one of them came forth a little horn, which waxed exceeding great, toward the south, and toward the east, and toward the beauteous land.
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 And it waxed great, even to the host of heaven; and some of the host and of the stars it cast down to the ground, and trampled upon them.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 Yea, it magnified itself, even to the prince of the host; and from him the continual burnt-offering was taken away, and the place of his sanctuary was cast down.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 And the host was given over to it together with the continual burnt-offering through transgression; and it cast down truth to the ground, and it wrought, and prospered.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Then I heard a holy one speaking; and another holy one said unto that certain one who spoke: 'How long shall be the vision concerning the continual burnt-offering, and the transgression that causes appalment, to give both the sanctuary and the host to be trampled under foot?'
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 And he said unto me: 'Unto two thousand and three hundred evenings and mornings; then shall the sanctuary be victorious.'
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 And it came to pass, when I, even I Daniel, had seen the vision, that I sought to understand it; and, behold, there stood before me as the appearance of a man.
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 And I heard the voice of a man between the banks of Ulai, who called, and said: 'Gabriel, make this man to understand the vision.'
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 So he came near where I stood; and when he came, I was terrified, and fell upon my face; but he said unto me: 'Understand, O son of man; for the vision belongeth to the time of the end.'
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 Now as he was speaking with me, I fell into a deep sleep with my face toward the ground; but he touched me, and set me upright.
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 And he said: 'Behold, I will make thee know what shall be in the latter time of the indignation; for it belongeth to the appointed time of the end.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 The ram which thou sawest having the two horns, they are the kings of Media and Persia.
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 And the rough he-goat is the king of Greece; and the great horn that is between his eyes is the first king.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 And as for that which was broken, in the place whereof four stood up, four kingdoms shall stand up out of the nation, but not with his power.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 And in the latter time of their kingdom, when the transgressors have completed their transgression, there shall stand up a king of fierce countenance, and understanding stratagems.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 And his power shall be mighty, but not by his own power; and he shall destroy wonderfully, and shall prosper and do; and he shall destroy them that are mighty and the people of the saints.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 And through his cunning he shall cause craft to prosper in his hand; and he shall magnify himself in his heart, and in time of security shall he destroy many; he shall also stand up against the prince of princes; but he shall be broken without hand.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 And the vision of the evenings and mornings which hath been told is true; but thou, shut thou up the vision; for it belongeth to many days to come.'
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 And I Daniel fainted, and was sick certain days; then I rose up, and did the king's business; and I was appalled at the vision, but understood it not.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >