< Daniel 5 >

1 Belshazzar the king made a great feast to a thousand of his lords, and drank wine before the thousand.
Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao.
2 Belshazzar, while he tasted the wine, commanded to bring the golden and silver vessels which Nebuchadnezzar his father had taken out of the temple which was in Jerusalem; that the king and his lords, his consorts and his concubines, might drink therein.
Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea.
3 Then they brought the golden vessels that were taken out of the temple of the house of God which was at Jerusalem; and the king, and his lords, his consorts and his concubines, drank in them.
Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea.
4 They drank wine, and praised the gods of gold, and of silver, of brass, of iron, of wood, and of stone.
Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.
5 In the same hour came forth fingers of a man's hand, and wrote over against the candlestick upon the plaster of the wall of the king's palace; and the king saw the palm of the hand that wrote.
Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika.
6 Then the king's countenance was changed in him, and his thoughts affrighted him; and the joints of his loins were loosed, and his knees smote one against another.
Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.
7 The king cried aloud to bring in the enchanters, the Chaldeans, and the astrologers. The king spoke and said to the wise men of Babylon: 'Whosoever shall read this writing, and declare unto me the interpretation thereof, shall be clothed with purple, and have a chain of gold about his neck, and shall rule as one of three in the kingdom.'
Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”
8 Then came in all the king's wise men: but they could not read the writing, nor make known to the king the interpretation.
Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake.
9 Then was king Belshazzar greatly affrighted, and his countenance was changed in him, and his lords were perplexed.
Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.
10 Now the queen by reason of the words of the king and his lords came into the banquet house; the queen spoke and said: 'O king, live for ever! let not thy thoughts affright thee, nor let thy countenance be changed;
Malkia aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho!
11 there is a man in thy kingdom, in whom is the spirit of the holy gods; and in the days of thy father light and understanding and wisdom, like the wisdom of the gods, was found in him; and the king Nebuchadnezzar thy father, the king, I say, thy father, made him master of the magicians, enchanters, Chaldeans, and astrologers;
Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi.
12 forasmuch as a surpassing spirit, and knowledge, and understanding, interpreting of dreams, and declaring of riddles, and loosing of knots, were found in the same Daniel, whom the king named Belteshazzar. Now let Daniel be called, and he will declare the interpretation.'
Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”
13 Then was Daniel brought in before the king. The king spoke and said unto Daniel: 'Art thou Daniel, who is of the children of the captivity of Judah, whom the king my father brought out of Judah?
Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda?
14 I have heard of thee, that the spirit of the gods is in thee, and that light and understanding and surpassing wisdom is found in thee.
Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee.
15 And now the wise men, the enchanters, have been brought in before me, that they should read this writing, and make known unto me the interpretation thereof; but they could not declare the interpretation of the thing.
Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia.
16 But I have heard of thee, that thou canst give interpretations, and loose knots; now if thou canst read the writing, and make known to me the interpretation thereof, thou shalt be clothed with purple, and have a chain of gold about thy neck, and shalt rule as one of three in the kingdom.'
Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”
17 Then Daniel answered and said before the king: 'Let thy gifts be to thyself, and give thy rewards to another; nevertheless I will read the writing unto the king, and make known to him the interpretation.
Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.
18 O thou king, God Most High gave Nebuchadnezzar thy father the kingdom, and greatness, and glory, and majesty;
“Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari.
19 and because of the greatness that He gave him, all the peoples, nations, and languages trembled and feared before him: whom he would he slew, and whom he would he kept alive; and whom he would he raised up, and whom he would he put down.
Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha.
20 But when his heart was lifted up, and his spirit was hardened that he dealt proudly, he was deposed from his kingly throne, and his glory was taken from him;
Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake.
21 and he was driven from the sons of men, and his heart was made like the beasts, and his dwelling was with the wild asses; he was fed with grass like oxen, and his body was wet with the dew of heaven; until he knew that God Most High ruleth in the kingdom of men, and that He setteth up over it whomsoever He will.
Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.
22 And thou his son, O Belshazzar, hast not humbled thy heart, though thou knewest all this;
“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.
23 but hast lifted up thyself against the Lord of heaven; and they have brought the vessels of His house before thee, and thou and thy lords, thy consorts and thy concubines, have drunk wine in them; and thou hast praised the gods of silver, and gold, of brass, iron, wood, and stone, which see not, nor hear, nor know; and the God in whose hand thy breath is, and whose are all thy ways, hast thou not glorified;
Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake.
24 then was the palm of the hand sent from before Him, and this writing was inscribed.
Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.
25 And this is the writing that was inscribed: MENE MENE, TEKEL UPHARSIN.
“Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa: mene, mene, tekeli na peresi
26 This is the interpretation of the thing: MENE, God hath numbered thy kingdom, and brought it to an end.
“Hii ndiyo maana ya maneno haya: “Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
27 TEKEL, Thou art weighed in the balances, and art found wanting.
Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
28 PERES, thy kingdom is divided, and given to the Medes and Persians.'
Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
29 Then commanded Belshazzar, and they clothed Daniel with purple, and put a chain of gold about his neck, and made proclamation concerning him, that he should rule as one of three in the kingdom.
Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.
30 In that night Belshazzar the Chaldean king was slain.
Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa,
31 And Darius the Mede received the kingdom, being about threescore and two years old.
naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.

< Daniel 5 >