< Job 1 >

1 There was a man in the lande of Vz called Iob, and this man was an vpright and iust man, one that feared God, and eschewed euill.
Kulikuwa na mtu katika nchi ya Usi jina lake Ayubu; na Ayubu alikuwa mwenye haki na mkamilifu, mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na
2 And he had seue sonnes, and three daughters.
uovu. Wakazaliwa kwake watoto saba wa kiume na mabinti watatu.
3 His substance also was seuen thousande sheepe, and three thousand camels, and fiue hundreth yoke of oxen, and fiue hundreth shee asses, and his family was very great, so that this man was the greatest of all the men of the East.
Alimiliki kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia moja za maksai, na punda mia tano na idadi kubwa ya watumishi. Mtu huyu alikuwa mtu mkuu wa watu wote wa mashariki.
4 And his sonnes went and banketted in their houses, euery one his day, and sent, and called their three sisters to eate and to drinke with them.
Kwa siku yake kila mtoto wa kiume, hufanya karamu katika nyumba yake. Wakatuma na kuwaita dada zao watatu waje kula na kunywa pamoja nao.
5 And when the dayes of their banketting were gone about, Iob sent, and sanctified them, and rose vp early in the morning, and offred burnt offrings according to the nomber of them all. For Iob thought, It may be that my sonnes haue sinned, and blasphemed God in their hearts: thus did Iob euery day.
Baada ya siku za karamu zilipokuwa zimetimia, Ayubu hutuma kwao na kuwatakasa. Aliamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketezwa kwa kila mtoto wake, kwa kusema, “Yawezekana kwamba wanangu wamefanya dhambi na kumkufuru Mungu mioyoni mwao.” Siku zote Ayubu alifanya hivi.
6 Nowe on a day when the children of God came and stoode before the Lord, Satan came also among them.
Kisha ilikuwa siku ambayo watoto wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA. Shetani pia akaenda pamoja nao.
7 Then the Lord sayde vnto Satan, Whence commest thou? And Satan answered the Lord, saying, From compassing the earth to and from, and from walking in it.
BWANA akamuuliza Shetani, “Umetoka wapi wewe?” Kisha Shetani akamjibu BWANA na kusema, “Natoka kuzunguka zunguka duniani, kutembea huku na huko humo.”
8 And the Lord saide vnto Satan, Hast thou not considered my seruant Iob, how none is like him in the earth? an vpright and iust man, one that feareth God, and escheweth euill?
BWANA akamuuliza Shetani, “Je umemwangalia mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hakuna mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mwenye haki na mkamilifu, mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu.”
9 Then Satan answered the Lord, and sayde, Doeth Iob feare God for nought?
Kisha Shetani akamjibu BWANA na kusema, “Je Ayubu amcha Mungu bila sababu?
10 Hast thou not made an hedge about him and about his house, and about all that he hath on euery side? thou hast blessed the worke of his hands, and his substance is increased in the land.
Wewe hukumwekea kinga pande zote, kuzunguka nyumba yake, na kuzunguka vitu vyote alivyo navyo kutoka kila upande? Wewe umebariki kazi za mikono yake, na mifugo yake imeongezeka katika nchi.
11 But stretch out now thine hand and touch all that he hath, to see if he will not blaspheme thee to thy face.
Lakini sasa nyosha mkono wako na uguse yote hayo aliyonayo, na uone kama hatakufuru mbele ya uso wako.”
12 Then the Lord sayde vnto Satan, Lo, all that he hath is in thine hand: onely vpon himselfe shalt thou not stretch out thine hand. So Satan departed from the presence of the Lord.
BWANA akamwambia Shetani, “Tazama, hayo yote aliyonayo yamo mkononi mwako. Isipokuwa juu yake yeye mwenyewe usinyoshe mkono wako.” Kisha Shetani akatoka mbele za BWANA.
13 And on a day, when his sonnes and his daughters were eating and drinking wine in their eldest brothers house,
Ilitokea siku moja, wana wake wa kiume na binti zake walipokuwa wakila na kunywa mvinyo nyumbani mwa ndugu yao mkubwa.
14 There came a messenger vnto Iob, and said, The oxen were plowing, and the asses feeding in their places,
Mjumbe akamfikia Ayubu na kusema, “Hao maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakichunga karibu nao.
15 And the Shabeans came violently, and tooke them: yea, they haue slayne the seruants with the edge of the sworde: but I onely am escaped alone to tell thee.
Waseba wakawaangukia na kutoweka nao. Kwa wale watumishi, wamewaua kwa makali ya upanga. Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.”
16 And whiles he was yet speaking, another came, and sayde, The fire of God is fallen from the heauen, and hath burnt vp the sheepe and the seruants, and deuoured them: but I onely am escaped alone to tell thee.
Wakati alipokuwa akiendelea kusema, akatokea mwingine pia na kusema, “Moto wa Mungu umeanguka toka mbinguni na kuwateketeza kondoo na watumishi. Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.”
17 And whiles he was yet speaking, another came, and sayd, The Caldeans set on three bands, and fell vpon the camels, and haue taken them, and haue slayne the seruantes with the edge of the sworde: but I onely am escaped alone to tell thee.
Wakati alipokuwa akiendelea kusema, akatokea mwingine pia na kusema, “Wakaldayo walifanya vikundi vitatu, wakawashambulia ngamia, na kuondoka nao. Kwa wale watumishi, wamewaua kwa makali ya upanga. Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.”
18 And whiles he was yet speaking, came an other, and sayd, Thy sonnes, and thy daughters were eating, and drinking wine in their eldest brothers house,
Wakati alipokuwa akiendelea kusema, akatokea mwingine pia na kusema, “Wana wako wa kiume na binti zako walikuwa wakila na kunywa mvinyo nyumbani mwa ndugu yao mkubwa.
19 And behold, there came a great wind from beyonde the wildernesse, and smote the foure corners of the house, which fel vpon the children, and they are dead, and I onely am escaped alone to tell thee.
Upepo wenye nguvu ulitokea jangwani na ukapiga pembe nne za nyumba. Ikawaangukia vijana hao, na wakafa wote. Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.
20 Then Iob arose, and rent his garment, and shaued his head, and fel downe vpon the ground, and worshipped,
Kisha Ayubu akainuka, akalirarua joho lake, akanyoa kichwa chake, akaanguka chini kifudifudi na kumwabudu Mungu.
21 And sayd, Naked came I out of my mothers wombe, and naked shall I returne thither: the Lord hath giuen, and the Lord hath taken it: blessed be the Name of the Lord.
Akasema, “Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu ni uchi, nami nitakuwa uchi wakati nitakaporudi huko. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa. Jina la BWANA libarikiwe.”
22 In all this did not Iob sinne, nor charge God foolishly.
Katika mambo hayo yote, Ayubu hakutenda dhambi, wala hakumwazia Mungu kwa uovu.

< Job 1 >