< Psalms 1 >

1 Blessed is the man that doeth not walke in the counsell of the wicked, nor stand in the way of sinners, nor sit in ye seate of the scornefull:
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 But his delite is in the Lawe of the Lord, and in his Lawe doeth he meditate day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 For he shall be like a tree planted by the riuers of waters, that will bring foorth her fruite in due season: whose leafe shall not fade: so whatsoeuer he shall doe, shall prosper.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 The wicked are not so, but as the chaffe, which the winde driueth away.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stande in the iudgement, nor sinners in the assemblie of the righteous.
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the Lord knoweth the way of the righteous, and the way of the wicked shall perish.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.

< Psalms 1 >