< Genesis 19 >

1 And in the euening there came two Angels to Sodom: and Lot sate at the gate of Sodom, and Lot sawe them, and rose vp to meete them, and he bowed himselfe with his face to the ground.
Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
2 And he saide, See my Lords, I pray you turne in nowe into your seruants house, and tarie all night, and wash your feete, and ye shall rise vp early and goe your wayes. Who saide, Nay, but we will abide in the streete all night.
Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
3 Then he preassed vpon them earnestly, and they turned in to him, and came to his house, and he made them a feast, and did bake vnleauened bread, and they did eate.
Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
4 But before they went to bed, the men of the citie, euen the men of Sodom compassed the house rounde about from the yong euen to the olde, all the people from all quarters.
Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
5 Who crying vnto Lot said to him, Where are the men, which came to thee this night? bring them out vnto vs that we may knowe them.
Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
6 Then Lot went out at the doore vnto them, and shut the doore after him,
Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
7 And said, I pray you, my brethren, do not so wickedly.
Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
8 Beholde nowe, I haue two daughters, which haue not knowen man: them will I bring out now vnto you, and doe to them as seemeth you good: onely vnto these men doe nothing: for therefore are they come vnder the shadowe of my roofe.
Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
9 Then they said, Away hence, and they said, He is come alone as a stranger, and shall he iudge and rule? we will nowe deale worse with thee then with them. So they preassed sore vpon Lot himselfe, and came to breake the doore.
Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
10 But the men put forth their hand and pulled Lot into the house to them and shut to ye doore.
Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
11 Then they smote the men that were at the doore of the house with blindnes both small and great, so that they were wearie in seeking the doore.
Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
12 Then the men said vnto Lot, Whom hast thou yet here? either sonne in lawe, or thy sonnes, or thy daughters, or whatsoeuer thou hast in the citie, bring it out of this place.
Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
13 For we will destroy this place, because the crye of them is great before the Lord, and the Lord hath sent vs to destroy it.
Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
14 Then Lot went out and spake vnto his sonnes in lawe, which maried his daughters, and said, Arise, get you out of this place: for the Lord will destroy the citie: but he seemed to his sonnes in lawe as though he had mocked.
Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
15 And when the morning arose, the Angels hasted Lot, saying, Arise, take thy wife and thy two daughters which are here, lest thou be destroyed in the punishment of the citie.
Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
16 And as he prolonged the time, the men caught both him and his wife, and his two daughters by the hands (the Lord being mercifull vnto him) and they brought him foorth, and set him without the citie.
Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
17 And when they had brought them out, the Angel said, Escape for thy life: looke not behinde thee, neither tarie thou in all the plaine: escape into ye mountaine, least thou be destroyed.
Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
18 And Lot saide vnto them, Not so, I pray thee, my Lord.
Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
19 Behold now, thy seruant hath found grace in thy sight, and thou hast magnified thy mercie, which thou hast shewed vnto me in sauing my life: and I cannot escape in the mountaine, least some euill take me, and I die.
Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
20 See nowe this citie hereby to flee vnto, which is a litle one: Oh let me escape thither: is it not a litle one, and my soule shall liue?
Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
21 Then he said vnto him, Beholde, I haue receiued thy request also concerning this thing, that I will not ouerthrow this citie, for the which thou hast spoken.
Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
22 Haste thee, saue thee there: for I can doe nothing till thou be come thither. Therefore the name of the citie was called Zoar.
Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
23 The sunne did rise vpon the earth, when Lot entred into Zoar.
Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
24 Then the Lord rained vpon Sodom and vpon Gomorah brimstone, and fire from the Lord out of heauen,
Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
25 And ouerthrewe those cities and all the plaine, and all the inhabitants of the cities; and that that grewe vpon the earth.
Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
26 Now his wife behind him looked backe, and she became a pillar of salt.
Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
27 And Abraham rising vp earely in ye morning went to the place, where he had stand before the Lord,
Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
28 And looking towarde Sodom and Gomorah and toward all the land of the plaine, behold, he sawe the smoke of the lande mounting vp as the smoke of a fornace.
Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
29 But yet when God destroyed the cities of the plaine, God thought vpon Abraham, and sent Lot out from the middes of the destruction, when he ouerthrewe the cities, wherein Lot dwelled.
Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
30 Then Lot went vp from Zoar, and dwelt in the mountaine with his two daughters: for he feared to tarie in Zoar, but dwelt in a caue, he, and his two daughters.
Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
31 And the elder saide vnto the yonger, Our father is old, and there is not a man in the earth, to come in vnto vs after the maner of all ye earth.
Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
32 Come, wee will make our father drinke wine, and lie with him, that we may preserue seede of our father.
Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
33 So they made their father drinke wine that night, and the elder went and lay with her father: but he perceiued not, neither whe she lay downe, neither when she rose vp.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
34 And on the morowe the elder saide to the yonger, Behold, yester night lay I with my father: let vs make him drinke wine this night also, and goe thou and lie with him, that we may preserue seede of our father.
Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
35 So they made their father drinke wine that night also, and the yonger arose, and lay with him, but he perceiued not, when she lay downe, neither when she rose vp.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
36 Thus were both the daughters of Lot with childe by their father.
Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
37 And the elder bare a sonne, and she called his name Moab: the same is the father of the Moabites vnto this day.
Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
38 And the yonger bare a sonne also, and she called his name Ben-ammi: the same is the father of the Ammonites vnto this day.
Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.

< Genesis 19 >