< Genesis 20 >

1 Afterward Abraham departed thence toward the South countrey and dwelled betweene Cadesh and Shur, and soiourned in Gerar.
Abraham akasafiri kutoka pale hadi nchi ya Negebu, na akakaa kati ya Kadeshi na Shuri. Akawa mgeni akiishi Gerari.
2 And Abraham said of Sarah his wife, She is my sister. Then Abimelech King of Gerar sent and tooke Sarah.
Abraham akasema kususu mkewe Sara, “ni dada yangu.” Kwa hiyo Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma watu wake kumchukua Sara.
3 But God came to Abimelech in a dreame by night, and said to him, Beholde, thou art but dead, because of the woman, which thou hast taken: for she is a mans wife.
Lakini Mungu akamtokea Abimeleki usiku katika ndoto, akamwambia, “Tazama, wewe ni mfu kutokana na mwanamke uliye mchukua, kwa kuwa ni mke wa mtu.”
4 (Notwithstanding Abimelech had not yet come neere her) And he said, Lord, wilt thou slay euen the righteous nation?
Basi Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia hivyo akasema, “Bwana, Je utaua hata taifa lenye haki?
5 Said not he vnto me, She is my sister? yea, and she her selfe said, He is my brother: with an vpright minde, and innocent handes haue I done this.
Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.' Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.”
6 And God saide vnto him by a dreame, I knowe that thou diddest this euen with an vpright minde, and I kept thee also that thou shouldest not sinne against me: therefore suffered I thee not to touche her.
Kisha Mungu akasema naye katika ndoto, “Kweli, ninajua pia kwamba umefanya hili katika uadilifu wa moyo wako, na pia nilikuzuia usitende dhambi dhidi yangu mimi. Ndiyo maana sikuruhusu umshike.
7 Now then deliuer the man his wife againe: for he is a Prophet, and he shall pray for thee that thou mayest liue: but if thou deliuer her not againe, be sure that thou shalt die the death, thou, and all that thou hast.
Kwa hiyo, mrudishe huyo mke wa mtu, kwa kuwa ni nabii. Atakuombea, na utaishi. Lakini usipo mrudisha, ujuwe kwamba wewe pamoja na wote walio wa kwako mtakufa hakika.
8 Then Abimelech rising vp early in ye morning, called all his seruants, and tolde all these things vnto them, and the men were sore afraid.
Abimeleki akaamka asubuhi na mapema akawaita watumishi wake wote waje kwake. Akawasimulia mambo haya yote, na watu wale wakaogopa sana.
9 Afterward Abimelech called Abraham, and said vnto him, What hast thou done vnto vs? and what haue I offeded thee, that thou hast brought on me and on my kingdome this great sinne? thou hast done things vnto me that ought not to be done.
Kisha Abimeleki akamwita Abraham na kumwambia, “Umetufanyia jambo gani? Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa? Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa.”
10 So Abimelech said vnto Abraham, What sawest thou that thou hast done this thing?
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini kilikushawishi wewe kutenda jambo hili?”
11 Then Abraham answered, Because I thought thus, Surely the feare of God is not in this place, and they will slay me for my wiues sake.
Abraham akasema, “Ni kwasababu nilifikiri hakika hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii, na kwamba wataniua kwa ajili ya mke wangu.'
12 Yet in very deede she is my sister: for she is the daughter of my father, but not the daughter of my mother, and she is my wife.
Licha ya kwamba kweli ni dada yangu, binti wa baba yangu, ingawa si binti wa mama yangu; na ndiye alifanyika kuwa mke wangu.
13 Nowe when God caused me to wander out of my fathers house, I said then to her, This is thy kindnes that thou shalt shewe vnto me in all places where we come, Say thou of me, He is my brother.
Wakati Mungu aliponiondoa katika nyumba ya baba yangu na kusafiri kutoka mahali kwenda mahali pengine, nilimwambia mke wangu, kwa kila sehemu tutakayo kwenda, unioneshe uaminifu wako kama mke wangu: Kila mahali tutakapo kwenda, useme juu yangu kuwa, “Ni kaka yangu.”'''
14 Then tooke Abimelech sheepe and beeues, and men seruants, and women seruants, and gaue them vnto Abraham, and restored him Sarah his wife.
Ndipo Abimeleki akatwaa kondoo, maksai, watumwa wa kiume na wa kike akampatia Abraham. Basi Abimeleki akamrudisha Sara, mke wa Abraham.
15 And Abimelech saide, Beholde, my land is before thee: dwell where it pleaseth thee.
Abimeleki akasema, Tazama, Nchi yangu i mbele yako. Kaa mahali utakapopendezewa.”
16 Likewise to Sarah he said, Beholde, I haue giuen thy brother a thousand pieces of siluer: behold, he is the vaile of thine eyes to all that are with thee, and to all others: and she was thus reproued.
Na kwa Sara akasema, Tazama, nimempatia kaka yako vipande elfu vya fedha. Navyo ni kwa ajili ya kufunika kosa lolote dhidi yako machoni pa wote walio pamoja na wewe, na mbele ya kila mtu ambaye umemfanya kuwa na haki.”
17 Then Abraham prayed vnto God, and God healed Abimelech, and his wife, and his women seruants: and they bare children.
Kisha Abraham akaomba kwa Mungu, Na Mungu akamponya Abimeleki, mkewe, na watumwa wake wa kike kiasi kwamba wakaweza kupata watoto.
18 For the Lord had shut vp euery wombe of the house of Abimelech, because of Sarah Abrahams wife.
Kwa kuwa Yahwe alikuwa amewafanya wanawake wote wa nyumaba ya Abimeleki kuwa tasa kabisa, kwa sababu ya Sara, mke wa Abraham.

< Genesis 20 >