< Genesis 18 >

1 Againe the Lord appeared vnto him in the plaine of Mamre, as he sate in his tent doore about the heate of the day.
Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
2 And he lift vp his eyes, and looked: and lo, three men stoode by him, and when he sawe them, he ranne to meete them from the tent doore, and bowed himselfe to the grounde.
Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
3 And he said, Lord, if I haue now founde fauour in thy sight, goe not, I pray thee, from thy seruant.
Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
4 Let a litle water, I pray you, be brought, and wash your feete, and rest your selues vnder the tree.
Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
5 And I will bring a morsell of bread, that you may comfort your hearts, afterward ye shall go your wayes: for therefore are ye come to your seruant. And they said, Do euen as thou hast said.
Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
6 Then Abraham made haste into the tent vnto Sarah, and saide, Make ready at once three measures of fine meale: kneade it, and make cakes vpon the hearth.
Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
7 And Abraham ranne to the beastes, and tooke a tender and good calfe, and gaue it to the seruant, who hasted to make it ready.
Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
8 And he tooke butter and milke, and the calfe, which he had prepared, and set before them, and stoode himselfe by them vnder the tree, and they did eate.
Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
9 Then they saide to him, Where is Sarah thy wife? And he answered, Beholde, she is in the tent.
Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
10 And he saide, I will certainely come againe vnto thee according to ye time of life: and loe, Sarah thy wife shall haue a sonne. and Sarah heard in the tent doore, which was behinde him.
akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
11 (Nowe Abraham and Sarah were old and striken in age, and it ceased to be with Sarah after the maner of women)
Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
12 Therefore Sarah laughed within her selfe, saying, After I am waxed olde, and my lord also, shall I haue lust?
Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
13 And ye Lord saide vnto Abraham, Wherefore did Sarah thus laugh, saying, Shall I certainely beare a childe, which am olde?
Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
14 (Shall any thing be hard to the Lord? at the time appointed will I returne vnto thee, euen according to the time of life, and Sarah shall haue a sonne.)
Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
15 But Sarah denied, saying, I laughed not: for she was afraide. And he said, It is not so: for thou laughedst.
Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
16 Afterwarde the men did rise vp from thence and looked toward Sodom: and Abraham went with them to bring them on the way.
Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
17 And the Lord said, Shall I hide from Abraham that thing which I doe,
Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
18 Seeing that Abraham shalbe in deede a great and a mightie nation, and all the nations of the earth shalbe blessed in him?
Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
19 For I knowe him that he will commande his sonnes and his houshold after him, that they keepe the way of the Lord, to doe righteousnesse and iudgement, that the Lord may bring vpon Abraham that he hath spoken vnto him.
Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
20 Then the Lord saide, Because the crie of Sodom and Gomorah is great, and because their sinne is exceeding grieuous,
Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
21 I will goe downe nowe, and see whether they haue done altogether according to that crie which is come vnto me: and if not, that I may knowe.
sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
22 And the men turned thence and went toward Sodom: but Abraham stoode yet before the Lord.
Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
23 Then Abraham drewe neere, and said, Wilt thou also destroy the righteous with the wicked?
Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
24 If there be fiftie righteous within the citie, wilt thou destroy and not spare the place for the fiftie righteous that are therein?
Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
25 Be it farre from thee from doing this thing, to slay the righteous with the wicked: and that the righteous should be euen as the wicked, be it farre from thee. shall not the Iudge of all the worlde doe right?
Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
26 And the Lord answered, If I shall finde in Sodom fiftie righteous within the citie, then will I spare all the place for their sakes.
Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
27 Then Abraham answered and said, Behold nowe, I haue begun to speake vnto my Lord, and I am but dust and ashes.
Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
28 If there shall lacke fiue of fiftie righteous, wilt thou destroy all the citie for fiue? And he saide, If I finde there fiue and fourtie, I will not destroy it.
Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
29 And he yet spake to him againe, and saide, What if there shalbe found fourtie there? Then he answered, I will not doe it for fourties sake.
Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
30 Againe he said, Let not my Lord nowe be angry, that I speake, What if thirtie be founde there? Then he saide, I will not doe it, if I finde thirtie there.
Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
31 Moreouer he said, Behold, now I haue begonne to speake vnto my Lord, What if twentie be founde there? And he answered, I will not destroy it for twenties sake.
Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
32 Then he saide, Let not my Lord be nowe angrie, and I will speake but this once, What if tenne be found there? And he answered, I will not destroy it for tennes sake.
Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
33 And the Lord went his way when he had left communing with Abraham, and Abraham returned vnto his place.
Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.

< Genesis 18 >